Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2000-2005 Session 12 Sitting 5 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 64 2018-02-05

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-
Sehemu kubwa ya Jimbo la Ulanga imezungukwa na Hifadhi ya Selous Game Reserve hivyo kufanya wananchi wa Kata za Mbuga, Ilonga, Kataketa na Lukunde kukosa maeneo ya kilimo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo maeneo ya kilimo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Goodluck Mlinga, Mbunge wa Ulanga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Pori la Akiba Selous lilianzishwa kati ya mwaka 1896 na 1912 na Serikali ya Kikoloni ya Wajerumani. Wajerumani waliligawa pori hilo katika maeneo manne ambayo ni Ulanga, Kusini, Muhoro na Matandu. Mnamo mwaka 1951 pori hili lilisajiliwa rasmi kwa GN Na. 17 chini ya Fauna Consveration Ordinance CAP. 302.
Mheshimiwa Naibu Spika, Pori la Akiba la Selous ni muhimu sana kiuchumi, kiikolojia na kiutamaduni siyo tu kwa Taifa letu bali pia Kimataifa. Pori linaliingizia Taifa fedha za Kitanzania na za kigeni kupitia utalii, lina misitu ya Ilindima inayosaidia upatikanaji wa maji, linachangia kudhibiti mabadiliko ya tabia ya nchi na makazi na mazalia ya viumbe hai wakiwemo wanyamapori, samaki na viumbe wengine. Kutokana na umuhimu huo Umoja wa Mataifa umelitambua eneo hili kuwa urithi wa dunia. Sambamba na hilo Serikali ya Kikoloni ilianzisha pori tengefu la Kilombero mwaka 1952 ili kuunganisha mfumo wa kiikolojia katika maeneo hayo awili.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutatua changamoto za matumizi ya ardhi katika maeneo yaliyotajwa, Serikali inatekeleza mpango wa Kilombero na Lower Rufiji Wetlands Ecosystem Management Project, mradi huu unahusisha kutatua matatizo ya mipaka ya vijiji na mapori ya hifadhi yaliyo katika Wilaya ya Ulanga, Malinyi na Kilombero pamoja na kuwawezesha wananchi kumiliki ardhi kupitia hati miliki za kimila.
Aidha, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia mradi wake wa Land Tenure Support Programme (LTSP) inaendelea kuhakiki mpaka wa pori tengefu la Kilombero ambalo ni sehemu ya Wilaya ya Ulanga na kupima ardhi ya vijiji kwa ajili ya urasimishaji wa ardhi kwa wananchi na hatimaye kupata hati za kumiliki. Serikali inaamini kuwa kupitia miradi hii miwili changamoto ya matumizi ya ardhi kwa shughuli za kilimo, ufugaji na makazi zitatatuliwa kikamilifu.