Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE.DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Migogoro ya ardhi na mipaka ya vijiji na hifadhi bado imeendelea kuwa tatizo sugu licha ya kuwepo kwa ahadi na kauli mbalimbali na Serikali. Je, mgogoro wa Pori la Akiba Kijereshi na Sayanka katika Wilaya ya Busega utatatuliwa lini?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na napenda nipongeze majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, majibu haya yamejikita kuelezea taarifa ambayo siyo sahihi, kwa sababu migogoro mingi imekuwa ikichochewa na uhamishaji wa mipaka na ndiyo malalamiko ya wananchi katika maeneo husika, kwa vile Serikali imekuwa ikihaidi muda mrefu kwamba kuwe na mpango shirikishi kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii, TAMISEMI na Wizara ya Ardhi ili kuainisha mipaka vizuri zaidi, kitu ambacho kitaondoa migogoro na migongano iliyopo.
Je, ni lini sasa Serikali kupitia majibu haya, kwa sababu suala hili siyo mara ya kwanza au ya pili kuuliza hapa Bungeni, ni lini Serikali itakaa na wananchi wa maeneo husika ili kutatua mgogoro wa namna hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Mheshimiwa Naibu Waziri aliyekuwepo wakati ule Engineer Ramo Makani alitembelea maeneo husika yaliyotajwa kwa maana kwamba pori la Akiba la Kijereshi kwa wananchi wa kijiji cha Kijereshi, Mwakiloba, Lukungu na Mwamalole na akajione mwenyewe kwamba wananchi wana haki kwa kile wanachokizungumza, vilevile alikwenda Pori la Akiba la Sayanka akajionea mipaka imehamishwa wananchi wamekuwa miaka yote wanalima kabla ya mipaka kuwekwa. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari sasa kuja ujionee uhalisia huu na uondokane na taarifa potofu ambazo zinazotolewa na wataalam wako? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kujibu naomba niitumie nafasi hii kumpongeza sana kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya kwa kweli akina Masunga na Hasunga nadhani ni machachari sana, hongera sana Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nijibu maswali yake. Kuhusu matatizo na migogoro mbalimbali ambayo ipo katika maeneo mengi, ni kweli kabisa tumebaini kwamba kuna migogoro mingi ambayo aidha, imesababishwa na kutokushirikisha vizuri wananchi ama kutokana na sababu mbalimbali ama kuongezeka kwa idadi ya watu katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua mbalimbali katika maeneo mengi, kwanza tuliunda Kamati ya Kitaifa shirikishi ambayo ilishirikisha Wizara mbalimbali ambayo sasa imebainisha maeneo mbalimbali yenye migogoro na hivi sasa ipo katika hatua ya mwisho ya kubainisha na kutoa ushauri ili tuweze kufanya uamuzi ni maeneo yapi Serikali iweze kuyaachia kwa wananchi na maeneo yapi yabaki chini ya hifadhi. Baada ya taarifa hiyo kukamilika hivi karibuni nadhani kwamba taarifa hii itatolewa Bungeni na Wabunge wote watapata nafasi ya kuweza kujua.
Kuhusu kukaa na wananchi wa Jimbo la Mheshimiwa Chegeni mimi naomba nimuambie tu kwamba Serikali tuko tayari kukaa na wananchi ili kuweza kupitia mipaka hatua hadi hatua, mimi nimuahidi baada ya Bunge hili tutakaa naye tutapanga kwamba ni lini twende tukawatembelee ili na nijiridhishe kabisa kwamba madai anayoyasema na wananchi wanayoyasema kweli yanahusu hiyo mipaka na kama mipaka imesogezwa basi tuweze kuchukua hatua stahiki katika maeneo haya aliyoyataja. (Makofi)

Name

Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Migogoro ya ardhi na mipaka ya vijiji na hifadhi bado imeendelea kuwa tatizo sugu licha ya kuwepo kwa ahadi na kauli mbalimbali na Serikali. Je, mgogoro wa Pori la Akiba Kijereshi na Sayanka katika Wilaya ya Busega utatatuliwa lini?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu ya Naibu Waziri amesema Kamati ya Kitaifa iliyoundwa, ninapenda kujua ni lini Kamati hiyo itakamilisha taarifa hiyo na kuileta ndani ya Bunge ili matatizo hayo yaweze kukoma?(Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwamba Kamati ya Kitaifa ambayo ilikuwa inashirikisha zaidi ya Wizara tano iliundwa kupitia maeneo mbalimbali na kupitia nchi nzima kuona migogoro ambayo iko katika maeneo mbalimbali. Kamati hiyo imeshatoa tayari matokeo ya awali ambayo yamebainisha kila kitu ni maeneo gani ambayo yapo kwenye matatizo, baadhi ya maeneo ambayo yamebainishwa ni pamoja na vijiji 366 viko ndani ya hifadhi.
Kwa hiyo, basi juzi tumekaa na hiyo Kamati imetoa tena draft nyingine tumetoa maelekezo ni imani yangu ndani ya kipindi cha miezi miwili, Kamati hiyo itakamilisha kabisa hiyo taarifa na itawasilishwa kwa Waheshimiwa Wabunge na kutoa taarifa kamili.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE.DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Migogoro ya ardhi na mipaka ya vijiji na hifadhi bado imeendelea kuwa tatizo sugu licha ya kuwepo kwa ahadi na kauli mbalimbali na Serikali. Je, mgogoro wa Pori la Akiba Kijereshi na Sayanka katika Wilaya ya Busega utatatuliwa lini?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Bunda na Vijiji vya Honyari, Kihumbu, Maliwanda, Sarakwa, Kyandege mpaka wao kati ya pori la Akiba la Gruneti na Mheshimiwa Naibu Waziri amesema hapa kutoka mpaka wa Mto Lubana kwenda kwa wananchi ni mita 500 ningependa kujua kutoka mpaka mto Lubana kwenda porini ni mita ngapi?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika hili eneo la Gruneti kuna mipaka ambayo ipo lakini itakuwa ni vigumu sana kumpa taarifa kamili umbali uliopo kati ya huo mto na hilo eneo analolisema. Kwa hiyo naomba nitumie nafasi hii kuwambia kuwa nitakaa nae, tutaenda kutembelea hilo eneo ili tuone kwamba kuna umbali wa mita ngapi ambazo zinahusisha. (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE.DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Migogoro ya ardhi na mipaka ya vijiji na hifadhi bado imeendelea kuwa tatizo sugu licha ya kuwepo kwa ahadi na kauli mbalimbali na Serikali. Je, mgogoro wa Pori la Akiba Kijereshi na Sayanka katika Wilaya ya Busega utatatuliwa lini?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kuna mgogoro kati ya Pori la Akiba la Kimisi na maeneo ya Rweizinga – Mguruka katika Kata ya Bwelanyange, mwaka jana Bunge liliielekeza Serikali iende katika hayo maeneo na kutatua migogoro hii, lakini mpaka hivi sasa Serikali haijafika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kujua ni lini Mheshimiwa Waziri utaambatana na mimi ili tuende kwenye Kata ya Bwelanyange maeneo ya Rweizinga na Mguruka ili kushirikisha wananchi katika kuweka mipaka mipya kati ya pori la Akiba la Kimisi na Kata ya Bwelanyange? Nashukuru.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika maeneo aliyoyataja kulikuwa kuna matatizo na wananchi walikuwa na malalamiko kuhusu mipaka na naomba nimhakikishie kwamba niko tayari wakati wowote mwezi wa Machi, mwaka huu nitatembelea katika Mkoa wa Kagera na tutakapokuwa huko basi tutapata nafasi ya kwenda kupitia na kuongea na wananchi juu ya mipaka hiyo yote aliyoitaja katika maeneo ya Bwelanyange na maeneo mengine yote aliyoyataja.