Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Madini ya Tanzanite yanachimbwa Mkoani Manyara katika Wilaya ya Simanjiro, lakini madini hayo huchakatwa na kuuzwa Mkoani Arusha hali inayosababisha wananchi wa Manyara kutofaidika kiuchumi. (a) Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu kujenga kiwanda cha kuchakata madini hayo Mkoani Manyara? (b) Je, ni kiasi gani cha fedha kimeshachangiwa na madini haya katika mapato ya Mkoa wa Manyara?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba uniruhusu nimshukuru sana na kumpongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuamua kujenga ukuta katika eneo lote ambalo Tanzanite inachimbwa katika Mkoa wa Manyara hususan eneo la Simanjiro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niruhusu nimshukuru na kumpongeza sana Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Job Ndugai ambaye alimua kwa dhati kabisa kuunda Kamati Maalum kwa ajili ya kuchunguza upotevu wa fedha kupitia madini hayo ya Tanzanite yanayopatikana peke yake duniani eneo la Simanjiro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yangu ya nyongeza ni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, uzoefu unaonesha kumekuwa na upotevu wa pesa kwa sababu wageni wanaotoka nje wanaokuja kununua Tanzanite hawalipi VAT, lakini wazawa waliopo pale eneo la Simanjiro, ama Arusha na Manyara wao ndio wanaolipa VAT. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu jambo hili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa muda mrefu kumekuwa na mgogoro unaohusiana na mitobozano hususan kwa wachimbaji wadogo wadogo katika eneo hilo la Mererani, ni nini sasa kauli ya Serikali ili kuzuia migogoro hiyo isiyo ya lazima? Ahsante.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza linalohusiana na VAT, kwa kawaida VAT huwa hatozwi mtu mgeni. Vilevile ni kweli kabisa kwamba katika mnada huu, wageni walikuwa wanunua Tanzanite kwenye mnada bila kutozwa VAT, lakini kwa wale wenyeji walikuwa wanatozwa VAT. Mfano ukienda sehemu nyingine ni kwamba VAT unatozwa kule unakonunua bidhaa, kisha unaenda kurudishiwa kwenye kituo cha ndege (airport).
Mheshimiwa Mwenyekiti, na sisi kama Serikali tunaangalia namna mpya ya kuhakikisha kwamba katika mnada ule, watu wote wanaonunua Tanzanite, sasa hivi tutaanza kuwatoza kodi ya VAT halafu mgeni aende akarudishiwe kule airport. Huo ndiyo msimamo wa Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa suala la pili, kuhusu mitobozano. Ni kwamba mitobozano ni mgogoro wa muda mrefu pale Mererani na kuna kamati nyingi zimeundwa kuhakikisha kwamba wanakwenda wanatatua tatizo la mitobozano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie kwamba sasa hivi Umoja wa Wachimbaji wa Tanzanite pale pale Mererani wameweka mkakati wa namna wa kutatua mgogoro wa mitobozano. Kuna mkakati wameutengeneza na wamekubaliana kwa pamoja. Kwa hiyo, mkakati huo, ambao tuna hakika kwamba tukiufuata na utataribu ambao wameuweka mgogoro wa mitobozano utakwisha. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Madini ya Tanzanite yanachimbwa Mkoani Manyara katika Wilaya ya Simanjiro, lakini madini hayo huchakatwa na kuuzwa Mkoani Arusha hali inayosababisha wananchi wa Manyara kutofaidika kiuchumi. (a) Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu kujenga kiwanda cha kuchakata madini hayo Mkoani Manyara? (b) Je, ni kiasi gani cha fedha kimeshachangiwa na madini haya katika mapato ya Mkoa wa Manyara?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mbali na madini ya Tanzanite kuwa chanzo cha mapato kikubwa kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Arusha na Mkoa wa Manyara, lakini pia kuna madini ya aina ya Rubi yanapatikana katika Kijiji cha Mundarara, Wilayani Longido Mkoani Arusha.
Ningependa kujua Serikali, inajipanga vipi ili madini haya aina ya Rubi iweze kuwanufaisha wananchi wa Longido? (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namshukuru na ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kutetea wachimbaji wadogo wadogo Mkoani Arusha na kazi nzuri anayoifanya na wananchi wa Arusha wanaiona. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, madini ya Rubi yanapatikana katika Kijiji cha Mundarara katika Wilaya ya Longido Mkoani Arusha. Madini hayo yanapatikana na eneo hilo kwa pembeni yake kuna leseni ya mtu anayeitwa Mheshimiwa Mareale. Sasa hivi ni kwamba kuna wachimbaji wadogo wanavamia eneo lile. Sisi kama Serikali tunawapenda wachimbaji wadogo, lakini tunataka wafuate taratibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachokitizama sasa hivi ni kwamba lile eneo ambalo ni la mtu ambaye anayelimiliki na haliendelezi, tutaangalia namna bora ambayo tunaweza tukawatafutia wale wachimbaji wadogo waweze kuchimba na tuwatambue na wachimbe katika vikundi ili tuweze kuwatambua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wanapochimba, basi tuweze kama Serikali kupata kodi zetu pale, tupate mrahaba pale, Halmashauri ya Longido ineemeke na Serikali kwa ujumla ineemeke na zile fedha tupeleke kwa wananchi wengine ambao wako nje na maeneo ya uchimbaji, waweze kuneemeka kupata huduma za maji, barabara na huduma za afya. (Makofi)