Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatambua uwepo wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. (a) Je, kwa nini ripoti za Tume hiyo hazitolewi kwa muda muafaka kila mwaka kama masharti ya Katiba yanavyosema? (b) Je, ripoti ya mwisho ya Tume hiyo ilitolewa mwaka gani na lini imewasilishwa Bungeni? (c) Je, kwa nini harakati za Tume hiyo katika kushughulikia migogoro ya ardhi, ukaguzi wa vituo vya polisi, magereza pamoja na matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu umezorota kinyume na miaka ya nyuma?

Supplementary Question 1

MHE.USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo ninalo. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni tatizo gani lililopelekea ripoti zenye umuhimu mkubwa kama huu wa haki za binadamu zisichapishwe kwa wakati ili Wabunge na Watanzania wote kwa ujumla wakaweza kujua hali za haki za binadamu katika nchi yao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Wabunge kwa upande wa Zanzibar hawapati fursa ya kukagua vituo vya polisi wala vyuo vya mafunzo ili kuwatembelea waliozuiliwa na waliofungwa kujua kama utekekelezaji wa haki za binadamu unafanyika kwa kiwango ambacho kinatakiwa. Je, Serikali iko tayari kuwatengenezea Wabunge wa Zanzibar utaratibu wa kuweza kuvikagua vituo vya polisi na vyuo vya mafunzo ili kuona haki ya binadamu inatendeka kwa kiasi gani? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza amezungumzia kuhusu uchapishwaji wa hizi ripoti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ni kwamba, ni kweli taarifa hizi zinapaswa kuwasilishwa Bungeni kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameuliza na ndiyo maana tumetoa maelezo yetu kama Serikali kwamba ziko ambazo zimekamilika lakini ziko ambazo zinasubiri ukaguzi wa mahesabu ndipo ziweze kuchapwa na kuletwa Bungeni kwa sababu ndiyo itakuwa taarifa kamili.
Kwa hiyo, nimuondoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafahamu umuhimu wa taarifa hizi kuwasilishwa mbele ya Bunge na ndiyo maana Tume inaendelea kufanya kazi hiyo kuhakikisha kwamba taarifa hizi zinafika kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la nyongeza la pili ameulizia kuhusu kuwashirikisha Wabunge wa Zanzibar. Kwa mujibu wa Ibara ya 130(1) na kifungu cha 6 cha Sheria Namba 7 ya Tume ya mwaka 2001, Tume imepewa majukumu kufanya kazi hiyo ya kwenda kufanya ukaguzi yenyewe. Kwa hiyo, kazi hii kimsingi ni kazi ya Tume, lakini ambacho tunaweza tukakifanya kwa sababu ya kuombwa ushiriki wa Waheshimiwa Wabunge katika jambo hili na sisi pia tuko tayari kushirikiana nao ili wapate fursa kufahamu hali zilizoko katika maeneo ya magereza na vituo vya polisi.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatambua uwepo wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. (a) Je, kwa nini ripoti za Tume hiyo hazitolewi kwa muda muafaka kila mwaka kama masharti ya Katiba yanavyosema? (b) Je, ripoti ya mwisho ya Tume hiyo ilitolewa mwaka gani na lini imewasilishwa Bungeni? (c) Je, kwa nini harakati za Tume hiyo katika kushughulikia migogoro ya ardhi, ukaguzi wa vituo vya polisi, magereza pamoja na matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu umezorota kinyume na miaka ya nyuma?

Supplementary Question 2

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini katika ukiukwaji wa haki za binadamu katika nchi yetu katika kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Tano umeongezeka sana.
Je, ni lini Tume hii itatoa ripoti kwa sababu polisi wamekuwa wakikaa na watu mahabusu zaidi ya saa 24 kinyume cha sheria kitu ambacho kinakiuka haki za binadamu. Mimi binafsi nasema haya kwa uzoefu nilionao, mara nyingi nimekuwa nakwenda kwenye custody nayaona haya na naongea kama Mbunge kwamba kuna ukiukwaji wa haki za binadamu, kuna watu wanakaa zaidi ya miezi miwili katika vituo vya poilisi wanakuwa tortured, wanapigwa na wanaumizwa.
Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusiana na tatizo hili ambapo kumekuwa na ukiukwaji wa haki za binadamu katika vituo vya polisi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la msingi la Mhehimiwa Msigwa hapa imebeba hoja, ni lini Tume italeta taarifa kuhusiana na vitendo ambavyo vinavyanywa na Jeshi la Polisi.
Mheshimiwa Mwneyekiti, kazi ya Tume hii inajikita katika maeneo tofauti tofauti, ukiacha masuala ambayo yanahusisha polisi, lakini Tume hii ina kazi nyingi za kufanya kwa maana ya kutoa elimu lakini vilevile kwenda kutembelea katika shule za maadilisho, mahabusu za watoto na kila Tume inapokwenda kufanya kazi hiyo imekuwa ikiandaa taarifa na kuziwasilisha katika taasisi husika na mojawapo ikiwa ni kutoa maangalizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa tu ya Mheshimiwa Mbunge, Tume imekuwa ikifanya kazi hii. Kwa mfano, kipindi cha mwaka jana ilitolewa kauli moja kutoka kule Zanzibar na Jeshi la Polisi la kuzuia baadhi ya wafuasi wasiwakilishwe mahakamani na Tume ilitoa maelekezo na kulionya Jeshi la Polisi kwamba hizo ni haki za kimsingi kwa sababu ukisoma kwenye Sheria ya Mwenedo wa Makosa ya Jinai, kifungu cha 40 kinaelekeza kabisa kwamba kila mtu ana haki ya kuwasilishwa katika kesi za jinai.
Kwa hiyo, Tume imefanya kazi yake kuhakikisha kwamba likitokea jambo lolote lile kuhusu taasisi mbalimbali za Serikali au binafsi ambazo zinaonekana kama zinakiuka haki basi wamekuwa kwakitoa taarifa zake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa kumalizia ni kwamba pamoja na ukaguzi unaofanyika taarifa hizi zimekuwa zikiandaliwa na wahusika wamekuwa wakiwasilishiwa na hapa Bungeni taarifa itakuja rasmi kwa sababu ya ile taarifa ambayo tunaitegemea ya Tume ambayo itawasilishwa kwa Waziri mwenye dhamana.

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatambua uwepo wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. (a) Je, kwa nini ripoti za Tume hiyo hazitolewi kwa muda muafaka kila mwaka kama masharti ya Katiba yanavyosema? (b) Je, ripoti ya mwisho ya Tume hiyo ilitolewa mwaka gani na lini imewasilishwa Bungeni? (c) Je, kwa nini harakati za Tume hiyo katika kushughulikia migogoro ya ardhi, ukaguzi wa vituo vya polisi, magereza pamoja na matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu umezorota kinyume na miaka ya nyuma?

Supplementary Question 3

MHE. JAKU H. AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza lenye kifungu (a) na (b).
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri alipokuwa akijibu swali la msingi alisema Tume imekuwa ikiongeza jitihada kila mwaka kukagua vituo vya polisi na magereza. Je, katika kukagua vituo hivyo hasa vya polisi wameona makosa gani na hatua gani zimechukuliwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili Kikatiba wanafunzi walioko magerezani…

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, Mheshimiwa Jaku anataka kufahamu baada ya kaguzi hizi ni makosa gani yameonekana. Nirudie tu majibu yangu ya msingi niliyoyasema kwamba ripoti hii ikikamilika itawasilishwa. Nachelea kusema moja kwa moja kwa sababu iko ndani ya ripoti na ripoti hii itawasilishwa. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge avute subira ripoti hii ikiwasilishwa ataona ukaguzi uliofanyika na matokeo ya ukaguzi huo.