Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:- Je, ni kiasi gani cha fedha kinatolewa kwa Wilaya ambazo zinapakana au zilizo na Hifadhi za Taifa ikiwamo Wilaya ya Kilolo katika Hifadhi ya Udzungwa?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ambayo yanatofautiana na swali langu, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimkumbushe kidogo Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Milima ya Uluguru wanakaa Waluguru, Milima ya Usambaa wanakaa Wasambaa wanaotoka Tanga na Milima ya Udzungwa wanakaa Wadzungwa na Udzungwa iko Wilaya ya Kilolo kwa asilimia 70.
Mheshimiwa Naibu Spika, jibu nililopewa hapa, inaonekana kwamba Kilolo wanapewa kama hisani, siyo haki yao. Kwa hiyo, ninachoomba kwa kuwa tayari yalikuwepo makubaliano ya kuhamisha Makao Makuu ya Udzungwa kwenye Kilolo Udekwa, lifanyike ili wananchi wale wanufaike kwamba ile Udzungwa ni ya Wadzungwa siyo ya Waluguru. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa mara nyingi yamekuwa yakitokea maafa, kwa mfano vijiji vya Msosa, Ikula, Ruaha Mbuyuni, Mahenge na Mtandika wananchi wanauawa na tembo bila kulipwa fidia; na fidia ambayo wanalipwa ni fedha ndogo sana, ni pamoja na uharibufu wa mazao yao.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutunga au kuja kuleta hapa tubadilishe sheria ili wananchi hawa wawe na thamani zaidi ya wanyama ambao ndiyo wanawaua? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akifanya katika Jimbo lake. Amekuwa akifuatilia sana na amekuwa akiwatetea sana wananchi wa Jimbo la Kilolo. Kwa kweli hongera sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba hili suala la kuhamisha Makao Makuu, tutalishughulikia. Yapo mambo mengi ya kuzingatia tunapotaka kuhamisha makao makuu na jitihada sasa hivi zinafanywa katika kuangalia miundombinu kama itawezekana kwenda kufikika katika hayo maeneo ambayo yalikuwa yamekubalika pale awali. Baada ya hilo kukamilika, basi tutalifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu fidia ya wananchi ambao wanakuwa wameadhirika na wanyamapori hususan tembo na wanyama wengine, hili suala lipo kwa mujibu wa sheria na kwa mujibu wa tararibu zetu. Ni kweli kabisa taratibu ambazo zipo zinabainisha ni aina gani ya kifuta machozi ambacho kinatolewa kwa wananchi wanaokuwa wameathirika na haya matatizo. Sasa namuomba Mheshimiwa Mbunge kwamba katika hao wananchi ambao amewasema, hiki kiasi japo ni kidogo, hakilingani na thamani ya binadamu anayekuwa amepotea, lakini bado tutaendelea kutoa kwa wakati, nitaomba tuwasiliane nipate hayo majina ili niweze kuyafanyia kazi mara moja. Hilo nitalishughulikia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba nimhakikishie kwamba tuko kwenye harakati ya kuweza kupitia upya sera yetu pamoja na sheria ili tuakikishe kwamba tunahuisha na kuweka viwango vile ambavyo vitakuwa vinatosheleza na vinasaidia katika kupunguza haya matatizo. Nashukuru.