Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO (K.n.y. MHE. GODFREY MGIMWA) aliuliza:- Tatizo la umeme bado ni kubwa licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali. Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili na hatimaye kuvipatia umeme Vijiji vya Kipera, Lupalama, Itagutwa na Lyamgungwe?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Pamoja na majibu hayo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Kalenga pamoja na kazi nzuri inayofanyika wakandarasi hawa wanapeleka umeme lakini hawafikishi kwenye Taasisi za umma kama zahanati shule.
Je, Serikali inatoa msisitizo gani na kuwafariji hawa wanchi wa Kalenga juu ya utekelezaji wa mradi huo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika Jimbo ya Njombe Mjijini yupo mkandarasi anayetekeleza mradi wa Makambako - Songea. Mradi hule ulikuwa-designed miaka mingi sana, matokeo yake ni kwamba mitaa imepanuka na maeneo yamepanuka na yule anatumia mchoro wa miaka mingi iliyopita.
Je, Serikali inatusaidiaje sasa ili kusudi mradi ule wa Makambako - Songea inaopisha umeme katika vijiji, umeme ule uweze kufika vitongoji vyote na taasisi za umma?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza lilijielekeza kwenye taasisi za umma ambazo hazifikiwi na Mradi wa REA unaoendelea. Ningependa kumtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye Mkoa wa Iringa kuna mradi wa densification unaotekelezwa kwa ajili ya maeneo ambayo yalirukwa kwenye Awamu wa Pili. Inaangalia maeneo ya umma, taasisi mbalimbali, iwe hospitali, ziwe shule za msingi na kadhalika. Kwa hiyo nimuhakikishie kwamba mradi wa densification unafanya hiyo kazi katika Mkoa wa Iringa na mkandarasi anaendela na kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, aliulizia juu ya mradi wa Makambako - Songea. Naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwamba katika mradi huu wa Makambako Songea ujenzi wa laini wa msongo wa KV 220 kwanza kazi inaendela vizuri lakini pia swali lake alikuwa anauliza je maeneo ambayo vijiji vinavyopitiwa na msongo huo usambazaji wa umeme ukoje. Nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi ya kusambaza umeme itaendelae na maeneo ambayo yataachwa REA III itaendelea kuya-cover kwasababu mpango wa Serikali ya Awamu Tano ni kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata umeme ifikapo 2020/2021. (Makofi)

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO (K.n.y. MHE. GODFREY MGIMWA) aliuliza:- Tatizo la umeme bado ni kubwa licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali. Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili na hatimaye kuvipatia umeme Vijiji vya Kipera, Lupalama, Itagutwa na Lyamgungwe?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mradi wa REA III tayari umeanza na vijiji vingi vimepimwa, lakini sasa hivi kuna baadhi ya vijiji ambavyo vilisahaulika na baadaye tukaleta kuomba tena viingizwe.
Sasa Serikali inatuambiaje hasa katika Wilaya ya Kilolo, je, vijiji ambavyo vilisahaulika vitaongezwa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kama nilivyosema, mradi wa REA una awamu mbili, na lengo lake ni kuvifikia vijiji 7,823. Awamu ya kwanza vijiji 3,559 na awamu ya pili vijiji 4,313. Nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vijiji vyote vitafikiwa umeme ifikapo mwaka 2020/2021. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO (K.n.y. MHE. GODFREY MGIMWA) aliuliza:- Tatizo la umeme bado ni kubwa licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali. Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili na hatimaye kuvipatia umeme Vijiji vya Kipera, Lupalama, Itagutwa na Lyamgungwe?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, maeneo ya Kakelege na eneo la uwanja wa ndege Kata ya Nkilizia yapo katikati ya mji wa Nansio. Lakini maeneo haya yamerukwa na huduma ya umeme, jambo linalofanya wananchi wa maeneo haya waone kama wametengwa. na Mheshimiwa Waziri nimekuwa namuwasilishia tatizo hili mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali langu nataka kujua Serikali imefikia hatua ipi kuhakikisha kwamba maeneo haya yaliyo katikati ya mji wa Nansio yote yanapata huduma za umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika maelezo yangu ya awali Serikali inatekeleza mradi pia wa densification ambao sasa hivi Awamu ya Kwanza na ni kwa Mikoa sita. Baada ya kukamilika kwa mikoa hiyo Serikali itaendelea pamoja na wafadhili wa Norway kutekeleza awamu ya pili. Nia ya mradi huu ni kusambaza umeme katika maeneo kaya, vitongoji na taasisi za umma zilizorukwa. Kwa hiyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba Awamu ya Pili ya mradi huu itafikiwa katika maeneo ambayo ameyataja.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO (K.n.y. MHE. GODFREY MGIMWA) aliuliza:- Tatizo la umeme bado ni kubwa licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali. Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili na hatimaye kuvipatia umeme Vijiji vya Kipera, Lupalama, Itagutwa na Lyamgungwe?

Supplementary Question 4

MHE. DUNSTAN. L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Serikali ilihaidi kwamba Kata ya Mwakijembe ambayo iko mpakani na Kenya vijiji vyake vilisahaulika lakini kuna umuhimu wa kiulinzi vijiji vile kupata umeme. Serikali ilihaidi kwamba kabla mkandarasi hajaondoka kufanya survey wataagizwa ili jambo hilo lifanyike. Je, ni lini jambo hili litakamilika?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kata anayoitaja Mheshimiwa Mbunge ya Mwakijembe ni kata ambayo iko mpakani, laikini kama alivyosema aliliwasilisha ombi lake hilo. Kwa kutambua umuhimu wa maeneo ambayo yako mpakani suala lake linashughulikiwa na mkandarasi wa Mkoa wa Tanga katika maeneo ambao Wilaya ya Mkinga na Wilaya zinginezo ni Delimiki Electric Company Limited yupo site anaendelea na hiyo kazi. Kwa hiyo nimtoe wasi wasi Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali inashughulikia. Na kwa kuwa nia yetu ni kusambaza umeme katika maeneo yetu hilo jambo litafanikiwa, ahsante.