Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 60 2017-11-13

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO (K.n.y. MHE. GODFREY MGIMWA) aliuliza:-
Tatizo la umeme bado ni kubwa licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali.
Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili na hatimaye kuvipatia umeme Vijiji vya Kipera, Lupalama, Itagutwa na Lyamgungwe?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kuvipatia umeme Vijiji vya Kipela, Lupalama, Itagutwa, Ikongwe na Lyamgungwe katika Awamu ya Tatu ya uetekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini (REA III) inayoendelea kwa sasa. Aidha, kwa Mkoa wa Iringa miradi hiyo inatekelezwa na mkandarasi Kampuni ya Sengerema Engineering Group na tayari yupo katika eneo (site) akifanya upimaji wa awali kwenye vijiji tajwa pamoja na vijiji vingine 145 vya Mkoa wa Iringa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo tajwa inajumuisha ujenzi wa njia za umeme wa msongo wa kilovolti 33 na 11 zenye urefu wa kilometa 22; msongo wa kilovolti 0.4 yenye urefu wa kilometa 18; na uwekaji wa transfoma tisa pamoja na kuwaunganisha umeme wateja 215. Gharama ya kutekeleza miradi hiyo ni jumla ya shilingi bilioni 2.3.