Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Msalala kwa kusaidiana na Mbunge wao wameanza ujenzi wa Vituo vya Afya Bugarama, Mega, Ngaya na Isaka na miradi hiyo ipo katika hatua nzuri. (a) Je, Serikali imejipangaje kusaidia miradi hiyo ya ujenzi wa Vituo vya Afya? (b) Je, Serikali imejipangaje kukamilisha maboma zaidi ya 28 ya zahanati kwenye vijiji mbalimbli Jimboni Msalala?

Supplementary Question 1

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini naomba kwa sababu ndiyo nazungumza mara ya kwanza baada ya sakata la makinikia kuwa limepata mwelekeo, nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa hatua alizochukua. Hatua ambazo zimekuwa ni kilio changu na kilio cha wananchi wa Msalala kwa miaka yote toka Mgodi wa Bulyanhulu ulipokuwepo pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa sababu, wananchi kama ambavyo Mheshimiwa Waziri amesema, wameitikia vizuri sana katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa huduma za afya katika Halmashauri na jimbo lao na kwa sababu, changamoto ambayo ipo ni upatikanaji wa fedha Serikalini na kwa bahati nzuri tayari tumeshapata uhakika kwamba, tutalipwa zaidi ya bilioni 700 kutika kwenye makinikia.
Je, Serikali inaweza sasa ikakubaliana na ombi langu kwamba ni vizuri tukapata angalao shilingi bilioni 3.4 ambazo zinatakiwa kuyakamilisha maboma yote haya, ili wananchi hawa wasione nguvu zao zikiharibika kwa sababu mengine yana zaidi ya miaka saba toka yalipoanzishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa tayari tumeshaletewa shilingi milioni 400 kwa ajili ya uboreshaji wa Kituo cha Afya cha Chela, fedha ambazo pamoja na kwamba ni nyingi, lakini bado hazitoshi kwa sababu, malengo ni makubwa zaidi. Je, Serikali inaweza ikakubaliana na ushauri wangu kwamba, kwa sababu lengo nikupeleka huduma kwa wananchi wengi zaidi na kuna maboma tayari kwenye Vituo vya Afya vya Isaka, Mega na Lunguya ambavyo kama alivyoeleza Mheshimiwa Waziri kwamba viko kwenye hatua mbalimbali. Je, Waziri anaweza akatukubalia ombi letu kwamba fedha hizi tuzigawanye kwenye hivi vituo, ili angalao navyo viweze kufunguliwa halafu uboreshaji utakuwa unaendelea awamu kwa awamu kadri fedha zinavyopatikana kuliko kukaa na kituo kimoja na vingine vikaishia kwenye maboma kama ilivyo sasa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya ombi la uwezekano wa kutizama hii bilioni 3.4 zitumike ili kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya pamoja na zahanati; kimsingi hitaji ni kubwa sana, lakini si rahisi kabla ya kufanya hesabu kujua katika mahitaji mengine kiasi gani kiende upande wa afya, kwani vipaumbele ni vingi. Kwa hiyo, ni vizuri, ni wazo jema likachukuliwa likafikiriwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya shilingi milioni 400 ambazo zimepelekwa, Mheshimiwa Mbunge anaomba kwamba ziruhusiwe zihame kwenda kwenye maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi ili tuweze kukamilisha kituo cha afya kwa mujibu wa standard, lazima tuwe na uhakika chumba cha upasuaji kipo, wodi ya wazazi kwa maana ya akina mama na watoto, wodi ya akina baba ipo, maabara, nyumba za watumishi za kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachowaomba na niziagize halmashauri zote, pale ambapo pesa zimeletwa na Serikali si lazima, eti pesa hiyo iishie hapo, itumike busara kuhakikisha kwamba, kwa utaratibu wa Force Account tunatumia pesa ili ikibaki tukiwa na serving hakuna dhambi ya kuhakikisha kwamba, pesa hizo zinaweza zikahamia kwenda kumaliza matatizo mengine. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Msalala kwa kusaidiana na Mbunge wao wameanza ujenzi wa Vituo vya Afya Bugarama, Mega, Ngaya na Isaka na miradi hiyo ipo katika hatua nzuri. (a) Je, Serikali imejipangaje kusaidia miradi hiyo ya ujenzi wa Vituo vya Afya? (b) Je, Serikali imejipangaje kukamilisha maboma zaidi ya 28 ya zahanati kwenye vijiji mbalimbli Jimboni Msalala?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni sera ya Serikali kuwa na hospitali katika ngazi ya Wilaya ili kutoa huduma ya afya kwa wananchi wetu. Wilaya ya Karatu ina umri wa zaidi ya miaka 20 na haina Hospitali ya Wilaya. Ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Karatu? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi naomba niziase Halmashauri zote, ni wajibu wetu wa kuhakikisha kwanza tunaanza kwa kutenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za afya, lakini kama hiyo haitoshi, kwa kushirikisha wananchi ni vizuri tukaanza halafu Serikali ikaleta nguvu yake. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Msalala kwa kusaidiana na Mbunge wao wameanza ujenzi wa Vituo vya Afya Bugarama, Mega, Ngaya na Isaka na miradi hiyo ipo katika hatua nzuri. (a) Je, Serikali imejipangaje kusaidia miradi hiyo ya ujenzi wa Vituo vya Afya? (b) Je, Serikali imejipangaje kukamilisha maboma zaidi ya 28 ya zahanati kwenye vijiji mbalimbli Jimboni Msalala?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kata ya Marangu Magharibi yenye vijiji saba haina zahanati hata moja na hasa vijiji vya Kiraracha na Kitowo wako kwenye hali mbaya sana. Mbunge kwa kushirikiana na wananchi wameweka nguvu zao wanajenga zahanati kwa sasa na imefikia hatua za mwisho.
Nini commitment ya Serikali angalau milioni 20 ya dharura, ili kata hii iweze kupata kituo cha afya cha kisasa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika fursa niliyopata ya kutembelea Mkoa wa Kilimanjaro nilijionea. Nilienda Moshi Vijijini nikakutana na wananchi wa Kiafeni, nikakuta kwamba hawakai wakasubiri Serikali ifanye, kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge na yeye anakiri na wana utaratibu mzuri, wanasema siku ya utawala wanakwenda kushiriki wananchi kwa ujumla wake. Nguvu ambayo inatolewa na wananchi ukishirikisha na nguvu ya Serikali nina imani hata hiyo kazi ambayo imefanywa na wananchi anaosema Mheshimiwa Mbatia, hakika kwa kutumia uwezo wao wa ndani, kwa maana ya commitment kutoka katika Halmashauri, naomba niitake Halmashauri ihakikishe kwamba wanajibana ili huduma ambayo inahitajika kwa wananchi iweze kufikiwa kwa kumalizia zahanati.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:- Wananchi wa Jimbo la Msalala kwa kusaidiana na Mbunge wao wameanza ujenzi wa Vituo vya Afya Bugarama, Mega, Ngaya na Isaka na miradi hiyo ipo katika hatua nzuri. (a) Je, Serikali imejipangaje kusaidia miradi hiyo ya ujenzi wa Vituo vya Afya? (b) Je, Serikali imejipangaje kukamilisha maboma zaidi ya 28 ya zahanati kwenye vijiji mbalimbli Jimboni Msalala?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante na mimi napenda kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Mtwara Vijijini, Kata ya Mambo Pacha Nne na Kata ya Tangazo, Kijiji cha Kilambo, wameanza mchakato wa kujenga vituo vya afya na michango ya wananchi inaenda kwa kasi kubwa.
Je, Serikali itatusaidiaje katika kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya katika Kata ya Tangazo, Kijiji cha Kilambo na Kata ya Mango, Pacha Nne?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa sababu, miongoni mwa maeneo ambayo alileta kama request katika Jimbo lile la Mtwara ni eneo hilo kwa sababu liko linapakana na Msumbiji.
Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika vipaumbele vyetu vya sasa katika programu tunayoanza nayo kabla ya mwezi wa pili, maeneo yale tumeyapa kipaumbele na tumeyaingiza katika mpango wetu wa bajeti ya muda katika hizi funds ambazo tunazipata kutoka kwa wafadhili mbalimbali. (Makofi)