Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) Aliuliza:- Wakati Rais akiwa kwenye ziara Wilayani Rorya aliahidi ujenzi wa Daraja la Mto Mori linalounganisha Tarafa ya Suba Luoimbo na Nyancha, lakini kwenye bajeti ya mwaka 2016/ 2017 ujenzi wa daraja hilo haukuwepo. Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga daraja hilo ili kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wakati fulani ni vizuri haya majibu nayo tukawa tunayaona vizuri kwa sababu, Mheshimiwa Mbunge anauliza Daraja la Mto Mori, Rorya. Majibu ya matumaini yanakuja Daraja la Mto Mori, Tarime inakuwa inapoteza ile ladha ya swali na hasa mtu anapokuwa ameuliza swali kwa muda mrefu katika Bunge hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka kujua Halmashauri hazina uwezo wa kujenga hili daraja ndio maana zimeomba Serikali Kuu isaidie kwa maana ya TAMISEMI. Ni lini sasa Serikali Kuu itatoa fedha za kusaidia daraja hilo kwa sababu Halmashauri ya Wilaya ya Rorya uchumi wake ni mdogo haiwezi kujenga hilo daraja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Jimbo la Bunda ambalo natoka mimi kuna daraja la Mto Chamtikiti ambalo limeharibika muda mrefu na hivi karibuni tumesikia kwamba kuna fedha ilitoka kwa ajili ya kutengeneza daraja, lakini mpaka leo mvua inanyesha wanafunzi hawaendi shuleni kwa sababu ya hilo daraja. Ni lini Waziri atakuja Bunda kuliona hilo daraja kwa ajili ya kusaidia hali hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niseme ni kweli nafahamu na mimi Mheshimiwa Getere unafahamu nilikuwa kule Rorya na pale changamoto ni kubwa. Na ni kwamba Halmashauri tunafahamu wazi kwamba kwa sasa haitaweza isipokuwa ni kwa kupitia mamlaka yetu tuliyoiunda ya TARURA.
Kwa hiyo, naomba niwahakikishie kwamba, suala zima la daraja hili na kwa sababu eneo hili ni eneo la kipaumbele, nitawaagiza wataalam wangu wafike katika daraja hilo, lakini na eneo lingine ambalo Mheshimiwa Getere ulilizungumza, lengo kubwa ni kwamba waende kufanya tathmini tujue thamani ya kazi halafu tutaangalia tutalitengeneza kwa kifungu gani. Aidha, kupitia DFAD kwamba eneo hilo saa nyingine ni eneo la vikwazo au kupitia Mfuko wa Barabara kwa kadiri itakavyoonekana inafaa, lakini nikuhakikishie kwamba, nitawatuma wataalam wangu wataenda kufanya study ya kutosha, lengo kubwa kuwasaidia wananchi katika maeneo hayo.

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) Aliuliza:- Wakati Rais akiwa kwenye ziara Wilayani Rorya aliahidi ujenzi wa Daraja la Mto Mori linalounganisha Tarafa ya Suba Luoimbo na Nyancha, lakini kwenye bajeti ya mwaka 2016/ 2017 ujenzi wa daraja hilo haukuwepo. Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga daraja hilo ili kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi napenda kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itasitisha tozo katika Daraja la Kigamboni ili liweze kutumika kama madaraja mengine yalivyo ya Ruvu na Wami?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kwanza niwashukuru Waziri wa TAMISEMI na Naibu Waziri kwa majibu mazuri yaliyoulizwa na Waheshimiwa Wabunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Daraja la Kigamboni limejengwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF. Ni kivuko ambacho kinafanya kazi kama vivuko vingine tulivyonavyo nchini na vivuko vingine vilivyopo nchini pia vimeweka mfumo wa utozaji wa tozo kidogo ili kuhakikisha kwamba vivuko vile vinaendelea kulindwa na vinaendelea kukarabatiwa viweze kuendelea kufanya kazi.
Kwa hiyo, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge tozo iliyowekwa kwenye Kivuko cha Kigamboni na NSSF imefuata utaratibu wa kisheria na wa kikanuni na hivyo, itaendelea kuwepo, lakini itaendelea kuwa ikibadilishwa kulingana na mazingira na taratibu za kisheria ambazo zinaongoza tozo zote katika nchi yetu ya Tanzania katika vivuko vyote nchini.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) Aliuliza:- Wakati Rais akiwa kwenye ziara Wilayani Rorya aliahidi ujenzi wa Daraja la Mto Mori linalounganisha Tarafa ya Suba Luoimbo na Nyancha, lakini kwenye bajeti ya mwaka 2016/ 2017 ujenzi wa daraja hilo haukuwepo. Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga daraja hilo ili kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa Mheshimiwa Rais aliahidi maeneo mengi hasa wakati wa kampeni katika Jimbo la Mbulu Vijijini aliahidi ujenzi wa barabara kilometa tano katika Mji wa Haydom na Dongobesh kilometa mbili. Je, ni lini sasa ahadi hizi za Mheshimiwa Rais zitatekelezwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilizungumza hapa siku za nyuma zilizopita kwamba kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kwamba uratibu wa ahadi zote za Mheshimiwa Rais umefanyiwa kazi na nikuhakikishie Mheshimiwa Flatei kwamba commitment yetu ni kwamba, tutakapofika mwaka 2020 tuhakikishe kwamba, zile ahadi zote za barabara hizi ambazo zimelengwa ziweze kukamilika. Na kupitia Wakala wetu wa TARURA tumewapa hayo maelekezo kwamba, wahakikishe kwanza jambo la kwanza wana-identify ahadi za Mheshimiwa Rais na ahadi za viongozi wakuu katika maeneo hayo lengo kubwa kwamba waweke mpango kazi jinsi gani tutafanya tukifika mwaka 2020 maeneo hayo yote tuwe tumeweza kukamilisha jambo hili.