Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 85 2017-11-15

Name

Lameck Okambo Airo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) Aliuliza:-
Wakati Rais akiwa kwenye ziara Wilayani Rorya aliahidi ujenzi wa Daraja la Mto Mori linalounganisha Tarafa ya Suba Luoimbo na Nyancha, lakini kwenye bajeti ya mwaka 2016/ 2017 ujenzi wa daraja hilo haukuwepo.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga daraja hilo ili kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lameck Okambo Airo, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mto Mori unapita katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Rorya hali inayosababisha kuwepo kwa uhitaji wa madaraja mawili ili kurahisisha usafiri katika maeneo hayo mawili. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kupitia Mfuko wa Barabara imetengewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Mto Mori kwa upande wa Tarime. Taratibu za manunuzi zinaendelea, ili kumpata mkandarasi wa kujenga daraja hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Rorya usanifu wa awali umefanyika ili kujua gharama za ujenzi wa daraja hilo ambazo zinakadiriwa kuwa shilingi milioni 300. Halmashauri ya Wilaya ya Rorya imepanga kuweka kipaumbele na kutenga fedha katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 ili kukamilisha ujenzi huo.