Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne alipofanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana mwaka 2014 aliahidi kupatia x-ray. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya Rais hasa ikizingatiwa kuwa hospitali hiyo kwa sasa haina kifaa hata kimoja katika kitengo cha mionzi?

Supplementary Question 1


MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa kulichukulia kwa uzito suala hili na kutenga fedha hiyo. Imani yangu ni kwamba kifaa hiki kitakamilika na kitafika kwa wakati kwenye Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana. Sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana inao ujenzi wa jengo kubwa lenye ghorofa mbili kwa ajili ya wodi ya wanaume. Nataka commitment ya Serikali, je, watakuwa tayari baada tu ya jengo hili kukamilika mapema mwakani mwezi wa tatu kutusaidia kwa ajili ya kupata vitanda na vifaa tiba vingine ili kutoa huduma iliyo bora kuendana na kasi ya Awamu ya Tano?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Wilaya ya Ilemela haina Hospitali ya Wilaya ya Ilemela lakini ni wilaya mpya na ujenzi wa hospitali yake umeanza kwa kusuasua sana. kwenye bajeti ya shilingi bilioni nne sasa hivi imeshapata milioni 500 peke yake. Nataka kujua je, Serikali itakuwa tayari kuhakikisha fedha zipatikane na kwenda kukamilisha ujenzi wa hospitali hii ya Wilaya kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa Jimbo la Ilemela?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na upatikanaji wa vifaa ni dhahiri kwamba Serikali ina nia ya dhatikuhakikisha kwamba vifaa vinapatikana ili hospitali hiyo iweze kufanya kazi iliyotarajiwa na hivi sasa ninavyoongea tayari vitanda 25 vimeshapelekwa Nyamagana pamoja na magodoro yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba hospitali zote za Wilaya zinafanya kazi kwa kiwango cha hali ya juu kabisa. Tutakuwa tayari mara hospitali hii itakavyokuwa imekamilika tuhakikishe vifaa vyote vinapelekwa ili iweze kufanya kazi kwa ajili ya kusaidia Watanzania wa Nyamagana.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne alipofanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana mwaka 2014 aliahidi kupatia x-ray. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya Rais hasa ikizingatiwa kuwa hospitali hiyo kwa sasa haina kifaa hata kimoja katika kitengo cha mionzi?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna changamoto nyingi sana za Mikoa mipya na Wilaya mpya ambazo nyingi hazina Hospitali za Wilaya. Nini kauli ya Serikali ikiwemo wilaya ya kwangu ya Tanganyika ambayo haina Hospitali ya Wilaya. Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la ukosefu wa Hospitali za Wilaya katika maeneo yote nchini ambayo hayana Hospitali za Wilaya? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, nia ya Serikali ni kuhakikisha kwamba afya kwa wananchi wa Tanzania kama ilivyo kipaumbele na ndiyo maana bajeti imeongezeka kutoka shilingi bilioni 31 mpaka shilingi bilioni 269. Hii inaonesha jinsi ambavyo Serikali itahakikisha kwamba huduma hii inawafikia wananchi na kwa kuwepo Hospitali za Wilaya maeneo yote ambayo Hospitali za Wilaya hazipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizitake halmashauri zote zianze kwa kutenga maeneo lakini pia kwa kutumia own source na wao waanza ili Serikali iweze kuunga mkono jitihada hizo. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Primary Question

STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne alipofanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana mwaka 2014 aliahidi kupatia x-ray. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya Rais hasa ikizingatiwa kuwa hospitali hiyo kwa sasa haina kifaa hata kimoja katika kitengo cha mionzi?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niuliza kwamba Wilaya ya Siha inafanana sana na Nyamagana tuna hospitali mpya ya Wilaya ambayo Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Jafo alikuja akashirikiana na sisi kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha hospitali hiyo inaweza
kulaza na kufanya upasuaji. Lakini sasa tuna changamoto, pamoja na vifaa lakini tuna upungufu wa asilimia 74 ya watumishi. Je, Waziri atakuwa tayari tukae na yeye kujadili kwa namna ya dharura namna ya kusaidia hospitali hiyo? (Makofi

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mollel kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilifika Siha na ni kweli hata takriban wiki moja na nusu nilikuwa naongea na Mkuu wa Wilaya yako ya Siha na bahati nzuri katika kazi kubwa tunayoenda kuifanya katika umaliziaji wa hospitali tatu za awali ikiwepo Mvomero na Hospitali ya Siha na maeneo mengine tunaenda kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo hilo hata bila kukaa tumeshalimaliza tayari kwa ajili ya maslahi mapana ya wananchi wa Tanzania. (Makofi)