Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 83 2017-11-15

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-
Rais wa Awamu ya Nne alipofanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana mwaka 2014 aliahidi kupatia x-ray.
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya Rais hasa ikizingatiwa kuwa hospitali hiyo kwa sasa haina kifaa hata kimoja katika kitengo cha mionzi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ahadi hiyo ilitolewa na Mheshimiwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne mwaka 2014 wakati wa ufunguzi wa jengo la upasuaji katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana. Katika mwaka wa fedha 2017/ 2018, Serikali imetenga jumla ya shilingi 133,136,000 kwa ajili ya kununua mashine ya x-ray mpya ikiwa ni utekelezaji wa ahadi hiy iliyotolewa na Mheshimiwa Rais inayolenga kuboresha huduma za afya kwa wananchi.