Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA (K.n.y. MHE. AISHAROSE N. MATEMBE) aliuliza:- Watumishi wa sekta ya afya hususani madaktari wanatakiwa kuishi kwenye maeneo ya kazi ili inapotokea akahitajika inakuwa rahisi kuwahi kwenda kutoa huduma kwa wagonjwa. Hata hivyo, katika Mkoa wa Singida watumishi wengi wa sekta ya afya wanaishi mbali na eneo la kazi hivyo kuwa na changamoto kubwa na wakati mwingine kusababisha vifo vya wagonjwa wakiwemo wajawazito. Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha watumishi wa sekta ya afya wanakuwa na makazi kwenye maeneo jirani ikiwa ni pamoja na kuboresha nyumba chache zilizopo pamoja na kujenga zingine mpya?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Waziri kwa majibu mazuri naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa mwaka jana tuliomba fedha kwa ajili ya ukarabati Hospitali yetu ya Rufaa takribani shilingi bilioni 1.7 na tumekwishapata shilingi bilioni moja, je, fedha iliyobaki itakuja lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili, nimuombe Mheshimiwa Waziri aseme kama atakuwa tayari kuambatana nami kwenda kuangalia hali ya Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa na Kituo cha Afya cha Sokoine. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika mpango wa bajeti ilitengwa karibuni shilingi bilioni 1.7 na ndiyo maana kwa mujibu wa Serikali kwa sababu mipango yake ni kuhakikisha miradi hii inatekelezeka tayari tumeshapeleka shilingi bilioni moja. Nishukuru sana wakati naongea na Sekretarieti ya Mkoa mwezi mmoja uliopita walikuwa katika michakato ya kuona ni jinsi gani fedha zile ziweze kutumika vizuri zaidi kuhakikisha kwamba jengo lile linakamilika. Hata hivyo, ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba hospitali hii inakamilika. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajitahidi kadri iwezekanavyo fedha zipatikane, mpango ule wa ujenzi wa Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa wa Singida iweze kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili kwamba ikiwezekana tuweze kuongozana, nimwambie Mheshimiwa Mbunge tujipange ikiwezekana hata kesho mchana, tutoke hapa mara moja tukafanye kazi turudi tuendelee na kazi za Bunge kwa sababu ni lazima tuhakikishe kwamba tunawafikia wananchi kuweza kuwahudumia kwa karibu zaidi.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA (K.n.y. MHE. AISHAROSE N. MATEMBE) aliuliza:- Watumishi wa sekta ya afya hususani madaktari wanatakiwa kuishi kwenye maeneo ya kazi ili inapotokea akahitajika inakuwa rahisi kuwahi kwenda kutoa huduma kwa wagonjwa. Hata hivyo, katika Mkoa wa Singida watumishi wengi wa sekta ya afya wanaishi mbali na eneo la kazi hivyo kuwa na changamoto kubwa na wakati mwingine kusababisha vifo vya wagonjwa wakiwemo wajawazito. Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha watumishi wa sekta ya afya wanakuwa na makazi kwenye maeneo jirani ikiwa ni pamoja na kuboresha nyumba chache zilizopo pamoja na kujenga zingine mpya?

Supplementary Question 2

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tabora Manispaa mara mbili tulitenga pesa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya, tulianza majengo hayo miaka mitatu iliyopita, lakini na mwaka huu wa fedha tumetenga tena bajeti hiyo ya shilingi milioni 120 kwa ajili ya kuendeleza majengo hayo.
Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutupa pesa ili tuweze kumalizia Hospitali hiyo ya Wilaya ili tuweze kutatua kero kubwa inayoikabili Hospitali yetu ya Rufaa kwa population kubwa iliyopo Tabora Manispaa ili wananchi waanzie kwenye Hospitali yao ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Munde kwa sababu muda mwingi sana amekuwa ukipigia kelele Mkoa wake wa Tabora na ndiyo maana kwa mapenzi makubwa mpaka Mheshimiwa Rais akaona amkabidhi ambulance kwa ajili ya wananchi wake wa Tabora katika sekta ya afya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hili, naomba nimhakikishie kwamba mwaka wa fedha bado haujaisha, japokuwa tumepeleka fedha za Local Government Development Grants katika Halmashauri mbalimbali waweke vipaumbele tutaangalia kwa Tabora nini kimewekezwa. Naomba nimhakikishie kwa sababu mwaka haujaisha tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo bajeti ile iweze kufika ili mpango wa bajeti wa Manispaa ya Tabora uweze kukamilika kama ulivyokusudiwa katika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA (K.n.y. MHE. AISHAROSE N. MATEMBE) aliuliza:- Watumishi wa sekta ya afya hususani madaktari wanatakiwa kuishi kwenye maeneo ya kazi ili inapotokea akahitajika inakuwa rahisi kuwahi kwenda kutoa huduma kwa wagonjwa. Hata hivyo, katika Mkoa wa Singida watumishi wengi wa sekta ya afya wanaishi mbali na eneo la kazi hivyo kuwa na changamoto kubwa na wakati mwingine kusababisha vifo vya wagonjwa wakiwemo wajawazito. Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha watumishi wa sekta ya afya wanakuwa na makazi kwenye maeneo jirani ikiwa ni pamoja na kuboresha nyumba chache zilizopo pamoja na kujenga zingine mpya?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa swali la msingi linafanana kabisa na tatizo tulilonalo katika Hospitali yetu ya Mkoa, karibu asilimia 85 ya Madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa wanaishi nje kabisa ya hospitali ile na kusababisha wagonjwa kupata matatizo makubwa wanapokuja usiku kwa ajili ya matibabu. Tatizo kubwa lililoko katika Hospitali ya Mkoa kuna mwingiliano wa Magereza na Hospitali. Tulishauri mara nyingi kwamba Waziri wetu wa Afya pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani waweze kukaa pamoja waone kwamba lile gereza liweze kutoka ili madaktari wengi waweze kukaa karibu na Hospitali ile ya Mkoa ili kusaidia wagonjwa wanaofika hata usiku.
Je, ni lini sasa ombi hilo la Mkoa litaweza kutekelezeka ili wananchi wa Iringa waweze kupata haki ya kupata madaktari wakati wote?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Kabati kwa sababu wiki mbili zilizopita tulikuwa pale Iringa tukaenda mpaka Kilolo na miongoni mwa mambo tuliyopitia katika sekta ya afya kipindi cha nyuma tulifika mpaka Hospitali ya Frelimo kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma. Kwa jambo hili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa sababu Waziri wa Afya na Waziri wa Mambo ya Ndani wameshakaa tayari ku-discuss jambo hilo, usihofu kila kitu kitaenda vizuri lengo kubwa ni tuweze kuwapatia huduma wananchi wetu vizuri. Kwa hiyo, hilo jambo ondoa hofu kila kitu kitaenda vizuri Serikali itashughulikia.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA (K.n.y. MHE. AISHAROSE N. MATEMBE) aliuliza:- Watumishi wa sekta ya afya hususani madaktari wanatakiwa kuishi kwenye maeneo ya kazi ili inapotokea akahitajika inakuwa rahisi kuwahi kwenda kutoa huduma kwa wagonjwa. Hata hivyo, katika Mkoa wa Singida watumishi wengi wa sekta ya afya wanaishi mbali na eneo la kazi hivyo kuwa na changamoto kubwa na wakati mwingine kusababisha vifo vya wagonjwa wakiwemo wajawazito. Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha watumishi wa sekta ya afya wanakuwa na makazi kwenye maeneo jirani ikiwa ni pamoja na kuboresha nyumba chache zilizopo pamoja na kujenga zingine mpya?

Supplementary Question 4

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa tatizo la nyumba hizi za kukaa wahudumu wa afya hasa maeneo ya vijijini hasa Mikoa ya Lindi na Mtwara na Jimbo la Mtama ni kubwa sana. Pamoja na kazi nzuri sana inayofanywa na Taasisi ya Benjamin Mkapa ya ujenzi wa nyumba katika maeneo mbalimbali, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kuanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kulishughulikia tatizo hili ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi wetu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mkoa wa Lindi ni miongoni mwa maeneo ambayo yana changamoto kubwa sana ya afya. Mheshimiwa Nape ni shahidi kwamba katika jambo ambalo amekuwa akilipigia kelele sana ni hili la sekta ya afya na nimpongeze sana katika utekelezaji wa Ilani last week alienda kukabidhi ile ambulace, nadhani wananchi wa Mtama wana-appreciate kazi kubwa anayoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili alilotoa ni wazo zuri kwa sababu sasa hivi tunatumia fedha za Local Government Development Grants kwa ajili ya kuhakikisha miradi mingi hasa viporo inakamilika hasa katika ujenzi wa majengo mbalimbali ya afya na elimu. Ndiyo maana katika mpango wa bajeti ya mwaka huu tumetenga karibuni shilingi bilioni 251.18, lengo kubwa ni kuwezesha upatikanaji wa makazi kwa wataalamu wetu.
Kwa hiyo, jambo la kuanzisha mfuko, nadhani kwa sasa tutumie huu mfumo tuliokuwa nao lakini wazo ni zuri tutalifanyia kazi kama Serikali kuona nini tufanye, lengo kubwa tuweze kutatua matatizo ya afya kwa Watanzania wote kwa ujumla wetu.