Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 307 2017-05-31

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA (K.n.y. MHE. AISHAROSE N. MATEMBE) aliuliza:-
Watumishi wa sekta ya afya hususani madaktari wanatakiwa kuishi kwenye maeneo ya kazi ili inapotokea akahitajika inakuwa rahisi kuwahi kwenda kutoa huduma kwa wagonjwa. Hata hivyo, katika Mkoa wa Singida watumishi wengi wa sekta ya afya wanaishi mbali na eneo la kazi hivyo kuwa na changamoto kubwa na wakati mwingine kusababisha vifo vya wagonjwa wakiwemo wajawazito.
Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha watumishi wa sekta ya afya wanakuwa na makazi kwenye maeneo jirani ikiwa ni pamoja na kuboresha nyumba chache zilizopo pamoja na kujenga zingine mpya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aisharose Matembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Singida una jumla ya nyumba za watumishi wa sekta ya afya 345 kati ya nyumba 1,072 zinazohitajika. Hivyo, kuna upungufu wa nyumba za watumishi wa afya 737. Serikali inaendelea na ujenzi wa nyumba za watumishi 21 katika vituo vya afya na zahanati. Aidha, shilingi milioni 280.8 zimetengwa katika mwaka 2017/2018 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa nyumba za watumishi wa afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza kutoa ruzuku ya maendeleo (Local Government Development Grant) ambayo inatumika kumalizia maboma yaliyoanza kwa nguvu za wananchi katika sekta za afya, elimu na sekta nyingine. Kipaumbele cha matumizi ya fedha hizo kinapangwa na Halmashauri zenyewe kupitia Mpango wa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O&OD).