Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. JOHN aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaongeza gari la wagonjwa na mafuta ili kufanya huduma za kliniki katika maeneo hayo pamoja na huduma nyingine kuwaokoa kina mama na watoto?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Naomba kuuliza ni lini tunaweza kupata fedha za nyongeza kwa ajili ya mafuta ili watu hawa waweze kupata huduma ya kliniki kwenye maeneo hayo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama nilisema katika jibu langu la msingi kwamba, ni kweli Halmashauri ya Kiteto ina changamoto kubwa sana kijiografia na hili tunakiri wazi na ndiyo maana hata bajeti ukiipeleka wakati mwingine inakutana na changomoto kubwa sana! Kwa hiyo, maelekezo yetu kama Ofisi ya Rais TAMISEMI ni kwamba niwashauru wananchi wa Kiteto hasa ndugu zetu wa Halmashauri Wakurugenzi na timu yake wahakikishe kwamba wanaweka mkazo wa kutosha katika kipindi hiki cha mpito kabla hatuaanza mwaka mpya wa bajeti. Wafanye udhibiti wa kutosha katika own source ili wakikusanya mapato ya ndani, japo kipindi hiki kilichobakia cha kumaliza mwaka wahakikishe kwamba wanakusanya fedha nyingi ili gari muda wote ziweze kufanya kazi na akina mama waweze kupata huduma. Lakini nikiri ni kweli Halmashauri ya Kiteto ni moja ya Halmashauri ambazo tunatakiwa tuziangaliye karibu. Ahsante!

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. JOHN aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaongeza gari la wagonjwa na mafuta ili kufanya huduma za kliniki katika maeneo hayo pamoja na huduma nyingine kuwaokoa kina mama na watoto?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuuliza swali la nyongeza, kwa kuwa Kituo cha Afya cha Mlalo ndiyo kituo pekee kinachofanya huduma ya upasuaji katika Jimbo la Mlalo.
Je, ni lini Serikali itakipatia kituo hiki gari la wagonjwa ili pale ambapo upasuaji unakwama waweze kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Lushoto? Ahsante!

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshmiwa Naibu Spika, ni kweli Kituo cha Afya cha Mlalo kina changamoto ya gari. Lakini wiki iliyopita nilizungumza kwamba wakati mwingine hizi changamoto ni kweli, naomba ikiwezekana tuweke priority katika mchakato wa bajeti. Mheshimiwa Shangazi kwa sababu najua ni mfuatiliaji sana katika maeneo yako haya, tukiri kwamba mwaka huu Mlalo hawajapanga hii bajeti kwa ajili ya ununuzi wa gari, lakini naomba niwasisitize kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI itakuwa nanyi kwa karibu kuhakikisha katika bajeti ya mwaka wa fedha unaokuja Mlalo inapewa kipaumbele au tukipata fursa yoyote ya upatikanaji wa gari basi Mlalo iwe kipaumbele kwa sababu eneo lake na jiografia yake mpaka kuja huku Mjini changamoto yake ni kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba tulichukue hilo kama Ofisi ya Rais TAMISEMI tukishirikiana nanyi kwa pamoja kuhakikisha watu wa Mlalo baadaye wapate gari la wagonjwa ili akina mama na watoto waweze kupata huduma ya kutosha.