Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 5 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2016-04-25

Name

Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. JOHN aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itaongeza gari la wagonjwa na mafuta ili kufanya huduma za kliniki katika maeneo hayo pamoja na huduma nyingine kuwaokoa kina mama na watoto?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Papian John, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto inayo magari mawili ambayo yamekuwa yakitumika kubeba wagonjwa waliopewa rufaa ya matibabu. Magari haya pia hutumika katika huduma ya mkoba za kliniki za Afya ya Uzazi na Mtoto (RCH) kwa lengo la kuwaokoa akina mama na watoto. Katika Mpango wa Bajeti ya mwaka 2016/2017, Halmashauri haikuweka kipaumbele cha ununuzi wa gari la wagonjwa kutokana na ukomo wa bajeti. Tunaishauri Halmashauri iendelee kutumia magari mawili yaliyopo huku ikijipanga kuweka kipaumbele cha ununuzi wa gari kwa mwaka wa fedha 2017/2018
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bajeti ya mwaka 2015/2016, Halmashauri hiyo ilitengewa shilingi 43,283,040 kwa ajili ya mafuta ya gari na hadi sasa fedha zote zimeshapelekwa. Changamoto ya kijiografia ndiyo inaonekana kuwa tatizo linalosababisha bajeti iliyotengwa kutokidhi mahitaji.