Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, gharama ya ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam ni shilingi ngapi?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kutokana na ripoti ya CAG mpaka sasa hivi inaonekana ni 6% tu ya gesi inatumika, inayosafirishwa na hilo bomba na uwekezaji huu ni wa pesa nyingi. Nataka kujua Serikali imejipanga vipi kuhakikisha uwekezaji huu unaleta tija kwa Taifa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa kuna utata mkubwa katika uwekezaji huu kujua gharama halisi: Je, Serikali ipo tayari kumtaka CAG afanye special audit katika uwekezaji huu? Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza bomba la kusafirisha mafuta au gesi kwa sasa kutoka Madimba (Mtwara) hadi Dar es Salaam ndiyo bomba kubwa tulilonalo kwa upande wa gesi.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa sasa hivi gesi inayosafirishwa ni kati ya 6% hadi 10% ya uwezo wake na uwezo nimetaja ni milioni cubic feet 744. Sasa ni kwa nini? Bomba hilo lina upana wa inchi 36, ni kubwa; na mahitaji ya sasa ni megawati 668 tulizonazo kwa upande wa gesi, lakini miundombinu inayojengwa ndiyo mikakati sasa.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa tunajenga miradi miwili ya kusafirisha gesi Kinyerezi I na Kinyerezi II. Kinyerezi I tunafanya extension ya kuongeza megawati 185 ili katika Kinyerezi I pekee zifikie 335.
Mheshimiwa Spika, kadhalika tunajenga mradi mwingine katika Kinyerezi II ambao utaweza kutoa megawati 240. Sasa miradi hii miwili ikikamilika, mahitaji makubwa ya gesi yataongezeka. Kwa hiyo, itazidi 6% hadi 10% na tuna matarajio inaweza kufikia asilimia 20 hadi 30.
Mheshimiwa Spika, miundombinu inayojengwa kuhitaji gesi, bado ni mingi; tunahitaji umeme wa kutosha. Kwa sasa hivi umeme hautoshi. Ni matarajio yetu kwamba mara baada ya miradi mingine, tutakwenda Kinyerezi III utakaoanza mwaka 2018 utakaohitaji megawati 600. Kwa hiyo, mahitaji ya gesi bado yatakuwa ni makubwa.

Mheshimiwa Spika, lingine niseme mkakati mwingine, unapokuwa na gesi ya kutosha inakuruhusu kujenga miundombinu mingine kwa sababu una stock. Kwa hiyo, siyo hasara kuwa na gesi nyingi lakini kadhalika mikakati ya Serikali ni kuhakikisha kwamba hii gesi tunasafirisha kadri iwezekanavyo ili ichangie sana katika upatikanaji wa umeme. Mkakati wa Serikali ni kutumia gesi zaidi ili kuachana na mafuta ili kuwapunguzia mzigo wananchi, hilo ni katika ufafanuzi wa swali la kwanza.
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la ukaguzi, mahesabu ya Serikali hukaguliwa mara kwa mara, ni utaratibu wa kawaida. Kama ambavyo kila mwaka CAG hukagua, hata miradi hii ataendelea kuikagua.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niseme tu, suala la ukaguzi wa miradi ni endelevu, CAG ataendelea kukagua ili hali halisi iendelee kufahamika.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, gharama ya ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam ni shilingi ngapi?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini kuna suala moja hajatoa ufafanuzi wa kina.
Mheshimiwa Spika, mwekezaji analalamika kwamba 6% za uzalishaji na gesi inayochukuliwa haitamfanya aweze kurejesha gharama za uwekezaji kwa kipindi cha miaka 25 kadri walivyokubaliana na Serikali; na Mheshimiwa hapa anasema kwamba kadri siku zinavyokwenda basi gesi nyingine itahitajika.
Mheshimiwa Spika, nataka kufahamu, ni lini Serikali itamhakikishia mwekezaji kwamba bomba hili litatumika kwa asilimia 100 ili aweze kurejesha gharama zake ndani ya miaka 25, ikizingatiwa kwamba sasa hivi yupo kwenye mwaka wa 11? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa niseme mradi ule ni wa Serikali kwa asilimia 100, hilo ni la kwanza kabisa. Kwa hiyo, unamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100. Hata hivyo, kama nilivyosema, mwaka gani tutaweza kupata gesi asilimia 100 inayozalishwa pale? Ni mradi ambao ni endelevu. Iko miradi mingine inajengwa Mtwara ambayo inaanza mwezi Machi mwakani ambayo tutaanza kuzalisha megawati 500 kwa Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niseme tu kwamba bado kuna muda wa kutosha, ifikapo mwaka 2020/2022 tuna matarajio kwamba gesi inayozalishwa katika Madimba tutaweza kuitumia kwenye miradi yetu ya umeme.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwa sababu miradi ni mingi, ifikapo mwaka 2022 matarajio kati ya asilimia 80 hadi 100 tutaanza kutumia gesi yote asilia.