Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 74 2017-09-12

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:-
Je, gharama ya ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam ni shilingi ngapi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara na Songo Songo Mkoani Lindi hadi Dar es Salaam ulianza kutekelezwa mwezi Juni, 2013 na kukamilika mwezi Oktoba, 2015. Ujenzi wa mradi huu ulihusisha ujenzi wa mitambo ya kuchakata gesi asilia yaani Madimba (Mtwara) pamoja na Songo Songo (Lindi) kwa gharama ya dola za Marekani milioni 349.51 na pia ujenzi wa bomba la kusafirishia gesi asilia kutoka Mtwara na Songo Songo – Lindi hadi Dar es Salaam kwa gharama ya dola za Marekani milioni 875.72.
Mheshimiwa Spika, jumla ya gharama zote za mradi huu hadi kukamilika ni dola za Marekani milioni 1,225.23.
Mheshimiwa Spika, bomba lina uwezo wa kusafirisha gesi asilia futi za ujazo milioni 784 kwa siku na linaweza kufikia futi za ujazo milioni 1,002 kwa siku. Kwa sasa gesi inayosafirishwa ni futi za ujazo milioni 68.5 kwa siku.