Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Chunya.

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Serikali imekiri kwamba Chunya ni kati ya Wilaya kongwe nchini Tanzania, kwa kweli mwaka huu Chunya inafikisha miaka 75 ya kuwepo kama Wilaya, kwa hiyo kutokuwa na Mahakama ya Wilaya ni kama hatuitendei haki. Kwa hiyo, haya majibu ya Serikali nayashika mwaka kesho tukijaaliwa mwezi kama huu nitaionyesha Serikali jibu lake hili. Sasa naomba niulize swali moja la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuweka mkakati wa kujenga Mahakama ya Wilaya katika Wilaya ya Chunya, Serikali ina mpango gani wa kuweza kujenga Mahakama zingine kwenye Tarafa, kama Tarafa ya Kipembawe? (Makofi)

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa sasa wa Wizara, katika ujenzi wa Mahakama 15 za Wilaya na zingine Mahakama za Mwanzo na ukarabati wa baadhi ya majengo, tunakwenda awamu kwa awamu kutokana na upatikanaji wa fedha na bajeti. Hivyo, nimwondoe tu hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba pindi pale bajeti itakaporuhusu tutaangalia pia umuhimu wa kushuka ngazi za Mahakama za Mwanzo ili huduma hii iweze kuwafikia Watanzania wengi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa kwa hivi tunatumia teknolojia mpya ya ujenzi wa majengo ya Mahakama kwa gharama nafuu, tunaamini kabisa katika miaka michache ijayo kutokana na upatikanaji wa fedha itakuwa ni rahisi pia kuweza kuzifikia Mahakama za Mwanzo ili wananchi wa Jimbo la Lupa na wenyewe waweze kupata huduma hii kwa ukaribu kabisa.