Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 2 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 23 2017-09-06

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Chunya.

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA K.n.y WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Chunya ni moja ya Wilaya za zamani ambazo mpaka sasa hazina majengo kwa ajili ya Mahakama ya Wilaya. Kwa sasa Mahakama inendeshwa katika majengo ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na nafasi ndogo sana kukidhi matumizi ya huduma za Mahakama.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mkakati wa maboresho ya huduma za Mahakama tumepanga kujenga jengo la Mahakama ya Wilaya ya Chunya katika mwaka huu wa fedha, 2017/2018. Hivyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Chunya kuwa na subira, wakati mipango inafanyika ya kujenga Mahakama hiyo.