Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Shule ya Sekondari ya Wasichana Mpanda ilikuwa ya bweni kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, lakini sasa imekuwa ya kidato cha tano na sita tu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuirejesha shule hiyo kama ilivyokuwa awali?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PUDENSIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kumweleza kwamba, pamoja na kwamba Serikali ina nia njema ya kuweka sekondari za wasichana kila tarafa na kwa sasa katika Jimbo langu ama Mkoa wa Katavi kila tarafa bado haijawa bado na Sekondari za form five na six.
Je, haoni sasa kuna umuhimu na ulazima wa hii Shule ya Sekondari ya Mpanda kuanza sasa kwa kidato cha kwanza mpaka cha sita ili tuweze kuzuia mimba za utotoni kama sera na Serikali inavyosema?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama Serikali, tunaona umuhimu hasa wa kupunguza mimba za utotoni na kwa wasichana ambao Mheshimiwa Mbunge amekuwa akiwapigania hapa.
Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, kama ikiwezekana basi mchakato huo utaanza katika vikao husika kuanzia Baraza la Madiwani then itaenda katika Kamati ya Ushauri ya Mkoa, then itafika kwa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya sekta ya elimu na hapo akiridhia jambo hilo basi litaanza. Kwa hiyo, hili jambo halina mashaka, ni suala zima la kuangalia ni jinsi gani tutafanya.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tunasisitiza na Serikali inaweka nguvu ya kutosha na kama kuna changamoto kubwa, tutaona jinsi gani tutafanya ikiwa hata kuanzisha shule nyingine mpya zenye ubora unaofanana na ule. Lengo kubwa ni kuhakikisha watoto wetu hasa wasichana waweze kusoma katika mazingira rafiki tupate viongozi na wataalamu wa baadaye.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Shule ya Sekondari ya Wasichana Mpanda ilikuwa ya bweni kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, lakini sasa imekuwa ya kidato cha tano na sita tu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuirejesha shule hiyo kama ilivyokuwa awali?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Na mimi napenda kuuliza swali la nyongeza.
Swali ambalo Mheshimiwa Kikwembe ameuliza ni kwamba katika shule nyingi ikiwemo Ndanda Sekondari, Loleza na shule nyingi ambazo zilibadilishwa, zilizokuwa za wasichana na wavulana zikawa za wavulana. Hata hivyo, hizo shule hazijai kwa sababu shule ambayo ilikuwa kidato cha kwanza mpaka cha sita, leo unaifanya ya kidato cha tano tu na cha sita. Mabweni ni mengi. Nenda Loleza, hayajai; Ndanda hayajai; Mtwara Girls na shule nyingine nyingi. Maombi tayari yalishakuwa yamefika TAMISEMI na mchakato wa kufanya tathmini ulishaanza.
Je, ule mchakato ulisimama kwa tatizo gani? Nilichokuwa namuomba Mheshimiwa bado warudi wakalifanyie tathmini suala hilo kwa sababu majengo mengi yako idle na wanafunzi hasa wa kike wanakosa pa kwenda?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa ku-raise concern ambayo na sisi Serikalini tunajaribu kuitafakari. Maamuzi haya yalipofanyika pengine hatukufanya uchambuzi vizuri. Kuna faida kubwa shule inapokuwa na O-level na A- level kwa pamoja kuliko unapoamua A-level wakawa peke yake na O-level wakawa peke yake.
Hata hivyo, tunaendelea kuwasiliana na wenzetu wa Wizara ya Elimu ili tuweze kuona namna ya kurudisha kwa haraka tu, kwa sababu ni suala dogo tu; kurudisha ile miundombinu ipo na pengine maeneo mengine miundombinu imekuwa ikiharibiwa kwa sababu haitumiki. Kwa hiyo, concern ya Mheshimiwa Hawa Ghasia ni ya kweli na tutajaribu kuchambua kwa shule zote nchi nzima tuweze kuona namna ya kuzirudisha shule katika mfumo ule wa zamani ulivyokuwa. (Makofi)