Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 02 2017-09-05

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:-
Shule ya Sekondari ya Wasichana Mpanda ilikuwa ya bweni kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, lakini sasa imekuwa ya kidato cha tano na sita tu.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuirejesha shule hiyo kama ilivyokuwa awali?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pudenciana Wilfred Kikwembe, Mbunge wa Kavuu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Shule ya Sekondari ya Wasichana Mpanda ilisajiliwa kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na sita pekee ili kukidhi malengo ya kuwa na shule za kutosha za Kitaifa katika Mkoa wa Katavi. Shule hii ni miongoni mwa shule saba za sekondari zenye kidato cha tano na sita kati ya shule 38 za sekondari zilizopo Mkoani Katavi. Kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi kwa kushirikiana na Serikali katika ujenzi wa shule za sekondari za kutwa za kidato cha kwanza hadi cha nne, Serikali imeona umuhimu wa kuongeza shule ya kidato cha tano na sita ikiwemo Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mpanda.
Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ni kuhakikisha kila Tarafa inakuwa na sekondari ya kidato cha tano na sita. Serikali inatambua nia njema ya Mheshimiwa Mbunge kwa watoto wa eneo hilo. Hata hivyo, kama kuna ulazima wa kufanya hivyo, inahitajika maombi yafanyike kupitia taratibu husika za usajili wa shule. Serikali inaendelea kuboresha shule za kata zilizoko Mkoani Katavi ili kupunguza msongamano na kutoa elimu bora.