Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ni mpya na haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ili wananchi wa Wilaya hiyo waweze kupata huduma za afya?

Supplementary Question 1

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante na ahsante kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri yetu ya Itilima kwa mwaka wa fedha 2017/2018 tulikaa na kupitisha katika bajeti makadirio ya shilingi bilioni 1.6 na kipaumbele chetu tukaweka shilingi milioni 650 iwe ndiyo sehemu ya ujenzi wa hospitali hiyo. Nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni kigezo gani kilichotumika kutoka kwenye shilingi milioni 600 na kurudi shilingi milioni 179?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Halmashauri yetu ya Itilima ina changamoto nyingi katika maeneo yetu, na tayari Halmashauri yangu kushirikiana na wananchi eneo tumeshalipata na tayari tumeshafyatua tofali zaidi ya 15,000 na hivi sasa tumekuwa tukitegemea mapato ya ndani yataweza kusaidia kusukuma uendeshaji wa jengo hilo pamoja ikiwa na zina ahadi ya Mheshimiwa Rais? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hoja inayozungumzwa na Mheshimiwa Njalu ni hoja ya msingi, na jambo hili Mheshimiwa Njalu alilizungumza mara kadhaa wakati tulipokuwa tukibadilishana mawazo, lakini jambo hili tulivyokuwa tukilifuatilia ilikuwa ni kuhusu mchakato na ilipofika decision ya mwisho, juzi nilikuwa naongea na Mkurugenzi wa Itilima kwamba nini kilijiri mpaka imefikia hapo; imeonekana kwamba baada ya kikao kile cha mwisho cha Baraza la Madiwani kulikuwa na makubaliano kutokana na fedha iliyotengwa kwamba milioni 169 iliekezwe katika suala hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ndiyo manaa Serikali Kuu ikaongeza shilingi milioni 200 na zaidi. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge anajua kwamba haja ya suala zima la Hospitali ya Wilaya sisi kupitia Ofisi yetu hata katika commitment tuliyoweka kwa ajili ya eneo lako la Itilima ukiangalia katika maeneo ambayo tunakwenda kuboresha vituo vya afya Itilima nako tutapeleka takribani shilingi milioni 700 Mungu akijaalia kwa lengo tu kubwa la kuhakikisha kwamba wananchi wa Itilima wanapata hospitali.
Kwa hiyo, jambo hili ni la msingi na sisi Serikali tunalichukulia kwa uzito wake mkubwa sana. Jukumu letu kubwa ni kuwasaidia wananchi wako wa Itilima ambao Mheshimiwa Mbunge unawapigania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kuongeza fedha katika kuhakikisha kwamba ujenzi huu ambao unaendelea katika maeneo mbalimbali, kama tulivyosema katika bajeti ya mwaka huu wa fedha 2017/2018 katika fedha zile za CDG tumeziweka katika mafungu ambayo yatamalizia miradi mbalimbali ambayo ime-stuck katika sekta ya afya na sekta ya elimu. Jukumu letu kubwa ni kuweza kuongeza nguvu za wananchi ili hii miradi iliyoanza iweze kumalizika, kwa hiyo, Mheshimiwa Njalu naomba uwe na imani kwamba Serikali yako iko nawe kuhakikisha kwamba maendeleo katika jimbo lako ambalo ni jimbo jipya yanaweza kufanikiwa kama ilivyokusudiwa.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ni mpya na haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ili wananchi wa Wilaya hiyo waweze kupata huduma za afya?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Matatizo yaliyopo huko Itilima yapo pia katika Halmashauri mpya ya Wilaya ya Itigi. Wananchi wa Itigi wanaitegemea sana Hospitali ya Mission ya Mtakatifu Gaspari hawana hospitali ya wilaya. Je, Sasa Serikali iko tayari kusaidia Halmashauri ya Itigi kujenga nayo hospitali ya Wilaya ili iondokane na gaharama kubwa wanazotumia wananchi wake ambao ni wapiga kura wetu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Itigi kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kuna changamoto, lakini mara nyingi ndugu zangu nilikuwa nikisema hapa kwamba hili suala la ujenzi wa hospitali, ujenzi wa vituo vya afya mara nyingi michakato hii inaanza kule site chini. Hata hivyo niseme kwamba kwa kesi ya Itigi Mheshimiwa unakumbuka kwamba umeuliza swali hili mara kadhaa na ndiyo maana kutokana kwamba umeliuliza swali hili mara kadhaa, hata Serikali sisi kupitia ofisi yetu iliona lazima iipe kipaumbele Itigi kwa sababu hakuna Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipokwenda kutembelea pale Itigi tulikuta kituo cha afya ambacho hali yake si shwari, tukasema tunaanza na hapa. Ndiyo maana muda si mrefu ujao tutakwenda kujenga centre ya upasuaji kubwa sana na kujenga wodi zingine. Lengo kubwa ni kukiboresha kile Kituo cha Afya cha Itigi angalau kiweze kutoa huduma ambayo inalingana lingana japo na hospitali ili wananchi wa Jimo lako waweze kupata huduma vizuri.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ni mpya na haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ili wananchi wa Wilaya hiyo waweze kupata huduma za afya?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.
Kama ambavyo Halmashauri ya Itilima ilivyokuwa na tatizo la Hospitali ya Wilaya, Wilaya ya Liwale ni Wilaya ya zamani sana na lile jengo lake la Hospitali ya Wilaya limeshachakaa na limezidiwa uwezo. Kwa kutambua hilo Halmashauri yetu ya Wilaya ya Liwale imetenga eneo kama hekari 50 hivi kwaili ya mradi wa hospitali mpya ya Wilaya ya Liwale. Je, Serikali ipo tayari kutuunga mkono katika mradi huu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulikuwa wote site siku ile Liwale na mvua ilikuwa kidogo inanyesha na tumefika Hospitali yake ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wao Liwale pale wana hospitali ya Wilaya, lakini ni hospitali ya muda mrefu sana. Kama wazo hilo zuri lilivyo ambapo mnafikiria kujenga hospitali mpya Serikali haitoshindwa kuungana nanyi, lakini hayo mawazo lazima yaanze kwenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndio maana kwa kuona umuhimu wa Serikali Mheshimiwa Rais alipita kule kutoa ahadi, na kwa sababu hiyo katika kile Kituo cha Afya cha Kibutuka kwa maagizo ya Mheshimiwa Rais, tutakifanyia ukarabati mkubwa Kituo cha Afya cha Kibutuka kwa kujenga theater pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo kubwa ni kwamba
kina mama wanaopatikana katika eneo lile waweze kupata huduma. Kwa hiyo, Serikali itakuwa tayari kushirikiana na mipango mizuri ya pale.