Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 31 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 245 2017-05-22

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:-
Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ni mpya na haina Hospitali ya Wilaya.
Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ili wananchi wa Wilaya hiyo waweze kupata huduma za afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga, Mbunge wa Itilima kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa jumla ya ekari 30 zimepatikana kwa gharama ya shilingi milioni 30 ili kupata eneo la ujenzi wa hospitali ya Wilaya. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri imetenga jumla ya shilingi milioni 159.6 kutoka mapato ya ndani na shilingi milioni arobaini na tano kutokana na ruzuku ya maendeleo (CDG) kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri imetenga kiasi cha shilingi milioni 371.16 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD). Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 169.9 zinatokana na mapato ya ndani na shilingi milioni 201.2 ni fedha za maendeleo kutoka Serikali Kuu (CDG).