Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:- Kwa muda wa zaidi ya miaka miwili, Hospitali ya Wilaya ya Kibondo haina mganga wa meno licha ya hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi kwa sasa ikiwemo wakimbizi kutoka nchini jirani ya Burundi:- Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa meno katika hospitali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo ndiyo hospitali vilevile inayotumika kama Hospitali ya Rufaa kwa Wilaya ya Kakonko, lakini inatumika kama Hospitali ya Rufaa kwa wakazi kutoka nchini Burundi, kwa maana ya wakimbizi wapatao laki mbili. Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo kwenye hospitali hiyo ambayo hayajawahi kuongezwa kutoka mwaka 1971?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa sababu hiyo hiyo Serikali ina mpango gani wa kuongeza mgawo wa dawa ili kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wa Wilaya ya Kibondo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hospitali ya Mheshimiwa Mbunge ya kama Kibondo, ni kweli na mimi nilifika tulienda kukagua hospitali ile, kuna changamoto ya miundombinu pale na hata wenzetu wa Kakonko kwa mwalimu wangu pale, mara nyingi sana wanatumia kama ndio referral hospital yao katika eneo lile, changamoto hizo tumeziona. Siku ile nilivyokuwa pale site niliwaambia waangalie upungufu uliokuwepo (needs assessment) maana hata vifaa tiba na X-Ray lilikuwa ni changamoto na nilitoa maelekezo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, imani yangu ni kwamba wenzetu pale Halmashauri watafanya hiyo needs assessment ambapo mchakato utaanza katika vikao vya Halmashauri, tutaangalia nini kwa pamoja kitafanyika kwa ajili ya kuboresha hospitali ile kwa sababu idadi ya wagonjwa niliyoikuta pale ni kubwa sana na ni kweli anachosema Mheshimiwa Mbunge. Kwa hiyo, Serikali inasubiri jinsi gani michakato itawekwa katika kipaumbele cha Halmashauri yenyewe na sisi tutaweka nguvu kwa kadri iwezekanavyo ili hospitali ile iweze kutoa huduma vizuri.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:- Kwa muda wa zaidi ya miaka miwili, Hospitali ya Wilaya ya Kibondo haina mganga wa meno licha ya hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi kwa sasa ikiwemo wakimbizi kutoka nchini jirani ya Burundi:- Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa meno katika hospitali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Kigoma kwa muda mrefu umekuwa haupati watumishi kwa sababu upo pembezoni lakini pia wakimbizi wameingia kwa wingi katika Mkoa wa Kigoma pamoja na kwamba wana hospitali zao kwenye makambi lakini kutokana na binadamu wasivyoweza kuzuiliwa wanaingia kwa wingi katika miji yetu hali inayosababisha wagonjwa kuwa wengi kwenye hospitali zetu. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kulikuwa na suala la concern ya dawa katika Hospitali ya Kibondo ambalo mwanzo nilili-skip. Hata nilivyofika pale site Kibondo nilitoa maelekezo kuhusu matumizi mazuri ya Basket Fund. Maeneo yote nilikopita nimekuta kwamba japokuwa tumepeleka fedha za kutosha kwenye Basket Fund, lakini Waganga wetu wa Wilaya wameshindwa kuhakikisha zile fedha zinatumika kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wetu. Ndiyo maana nimetoa maelekezo kwamba itakapofika mwezi wa Sita, Halmashauri yoyote ambayo Serikali imepeleka fedha lakini zile fedha zimeshindwa kununua dawa na vifaa tiba kuwasaidia wananchi, tutasema kwamba, ma-DMO wao hawatoshi katika maeneo yetu hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la watumishi, japokuwa tatizo la watumishi ni tatizo kubwa sana, lakini ukiangalia katika mgawanyo wa Madaktari, Kigoma tumepeleka madaktari 10 lakini mikoa mingine imepata madaktari watano. Tunajua japokuwa Madaktari kumi wameenda katika Mkoa mzima wa Kigoma, bado hawatoshi, lakini tutakapokuja katika ajira mpya Mkoa wa Kigoma tutaupa kipaumbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba muelewe ndugu zangu, Kibondo pale kwa ndugu yangu Mheshimiwa Nditiye tumepeleka Madaktari watatu, Kasulu tumepeleka Madaktari wawili, halikadhalika Uvinza tumepeleka Madaktari na RAS Kigoma tumepeleka takribani Madaktari wanne. Lengo letu ni kuhakikisha Mkoa wa Kigoma na mikoa mingine ya pembeni iweze kupata…
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutawapa kipaumbele watu wa Kigoma kupata Madaktari wa kutosha.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:- Kwa muda wa zaidi ya miaka miwili, Hospitali ya Wilaya ya Kibondo haina mganga wa meno licha ya hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi kwa sasa ikiwemo wakimbizi kutoka nchini jirani ya Burundi:- Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa meno katika hospitali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ALMASI A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru sana kuniruhusu kuuliza swali. Kituo cha Afya cha Upuge ndiyo peke yake Hospitali ya Wilaya Jimboni kwangu, hakuna hospitali kabisa isipokuwa Kituo kile cha Upuge na hakina wataalam wa dawa za usingizi, wanaitwa anesthesia kitaaluma, kwa hiyo, hatuwezi kufanya operesheni. Je, Serikali inafikiria nini kupeleka mtaalam wa dawa za usingizi ili operesheni zifanyike? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kituo cha Afya cha mtani wangu pale, katika idadi ya wataalam ambao tutawaajiri hapa katikati kutokana na nafasi nyingi zilizotolewa na Mheshimiwa Rais tutaangalia mahitaji halisi ya kituo hiki then tutawapa kipaumbele ili mradi wampate mtaalam huyo wa usingizi.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:- Kwa muda wa zaidi ya miaka miwili, Hospitali ya Wilaya ya Kibondo haina mganga wa meno licha ya hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi kwa sasa ikiwemo wakimbizi kutoka nchini jirani ya Burundi:- Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa meno katika hospitali hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na tishio kubwa la ugonjwa wa sukari hapa nchini ambao umekuwa ukiwakumba watu wa rika mbalimbali na hatuna wataalam wa kutosha katika hospitali zetu. Vilevile hata dawa wanazopewa ikifikia hatua mgongwa wa sukari anatakiwa apate insulin dawa hizo zimekuwa zikiuzwa ghali, watu hawawezi ku-afford. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na tatizo hili?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso kuhusu upatikanaji wa dawa za kisukari na ongezeko la wagonjwa wa kisukari nchini. Ni kweli sasa hivi tunashuhudia ongezeko la wagonjwa wa kisukari lakini kwa sababu kwanza ya mfumo wa maisha ambao watu wanaishi, watu hawafanyi mazoezi, wanakula vyakula bila kuzingatia lishe lakini bila ku-check afya zao mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kubwa badala ya kujikita kwenye kutibu tumejikita kwenye kuzuia Watanzania wengi wasipate maradhi ya ugonjwa wa kisukari. Pale ambapo Mtanzania ana ugonjwa wa kisukari kwa mujibu wa Sera ya Afya dawa ya mgonjwa wa kisukari inatakiwa kupatikana kwa bei nafuu. Kwa hiyo, tunawaelekeza Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanapoandaa maoteo ya dawa basi wahakikishe pia wana-order dawa za kutosha kwa ajili ya wagonjwa wa kisukari. Kama hawawezi ku-order za kutosha sisi hatuwezi kuwapelekea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili la uhaba wa Madaktari wa Meno, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri na hata wakati wa bajeti ya Mheshimiwa Waziri wa Utumishi alitoa maelezo kwamba Mheshimiwa Rais ameridhia kuajiri watumishi wa Serikali takriban 52,000 na kati ya hao tunategemea kupata watumishi wa sekta ya afya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Savelina Mwijage tutakapopata kibali tutawapanga pia kwa ajili ya hospitali za Mkoa za Kagera. Ahsante sana.

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:- Kwa muda wa zaidi ya miaka miwili, Hospitali ya Wilaya ya Kibondo haina mganga wa meno licha ya hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi kwa sasa ikiwemo wakimbizi kutoka nchini jirani ya Burundi:- Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa meno katika hospitali hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa matatizo ya Kibondo ya Madaktari wa meno ni sawasawa na matatizo ya Wilaya ya Bukoba Vijijini ya Izimbya - Katekana hawana Daktari wa meno hata mmoja wakipata tatizo la ugonjwa mpaka waende Bukoba Mjini na ni mbali sana kutoka pale kwenda Bukoba Mjini. Ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuwaletea Madaktari wa meno wa kuwasaidia hao watu wa Bukoba Vijijini?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso kuhusu upatikanaji wa dawa za kisukari na ongezeko la wagonjwa wa kisukari nchini. Ni kweli sasa hivi tunashuhudia ongezeko la wagonjwa wa kisukari lakini kwa sababu kwanza ya mfumo wa maisha ambao watu wanaishi, watu hawafanyi mazoezi, wanakula vyakula bila kuzingatia lishe lakini bila ku-check afya zao mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kubwa badala ya kujikita kwenye kutibu tumejikita kwenye kuzuia Watanzania wengi wasipate maradhi ya ugonjwa wa kisukari. Pale ambapo Mtanzania ana ugonjwa wa kisukari kwa mujibu wa Sera ya Afya dawa ya mgonjwa wa kisukari inatakiwa kupatikana kwa bei nafuu. Kwa hiyo, tunawaelekeza Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanapoandaa maoteo ya dawa basi wahakikishe pia wana-order dawa za kutosha kwa ajili ya wagonjwa wa kisukari. Kama hawawezi ku-order za kutosha sisi hatuwezi kuwapelekea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili la uhaba wa Madaktari wa Meno, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri na hata wakati wa bajeti ya Mheshimiwa Waziri wa Utumishi alitoa maelezo kwamba Mheshimiwa Rais ameridhia kuajiri watumishi wa Serikali takriban 52,000 na kati ya hao tunategemea kupata watumishi wa sekta ya afya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Savelina Mwijage tutakapopata kibali tutawapanga pia kwa ajili ya hospitali za Mkoa za Kagera. Ahsante sana.