Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Wilaya ya Bukombe ina mahitaji ya walimu wa shule za msingi 1,425; waliopo ni walimu 982 na upungufu ni walimu 443:- Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha kuondoa upungufu huo?

Supplementary Question 1

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake, lakini nimpe taarifa tu kwamba mahitaji ya walimu kwenye Wilaya ya Bukombe sasa yameshaongezeka mpaka mahitaji tuliyonayo sasa ni walimu 914 na siyo walimu 400 kama ambayo imeripotiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka tu nijue, huu mpango wa kuhamisha walimu walipo sekondari wa masomo ya sanaa ambao ni wa ziada, kuwarudisha shule za msingi umesemwa kuwa muda mrefu sana na inakaribia sasa mwaka unapita; namuomba Mheshimiwa Naibu Waziri aseme specifically baada ya muda gani? Kwa sababu hali ya mahitaji ya walimu kule siyo nzuri. Ukiwapata wale walimu wanaweza kusaidia kuziba hilo pengo. Nakushukuru.

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie kwamba walimu hawa wa shule ya msingi wapo na bahati nzuri tayari tumeshapitisha na kama nilivyoeleza awali, kibali kilishatoka. Sasa hivi tunaendelea tu na hatua ya awali ili wahusika waweze kutuletea majina yao wafanyiwe uhakiki na hatimaye TAMISEMI waweze kuwapangia vituo.
Kwa hiyo, nimhakikishie tu pamoja na Halmashauri nyingine na Halmashauri ya Bukombe nayo itaweza kupatiwa walimu wa kutosha.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Wilaya ya Bukombe ina mahitaji ya walimu wa shule za msingi 1,425; waliopo ni walimu 982 na upungufu ni walimu 443:- Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha kuondoa upungufu huo?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Tatizo la walimu ni kubwa na ndiyo maana linasababisha hata matokeo ya wanafunzi yanakuwa hafifu. Kwa mfano, Jimbo la Vunjo lina upungufu wa walimu 207, sasa mchakato huu ni lini utamalizika kwa sababu mitihani iko karibuni na hali inazidi kuwa mbaya?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimweleze tu kwamba tunatambua upungufu uliopo katika Wilaya ya Vunjo na nimhakikishie tu kwamba by tarehe 15 Julai, 2017 tunaamini tutakuwa tumefika katika sehemu nzuri. Ahsante.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Wilaya ya Bukombe ina mahitaji ya walimu wa shule za msingi 1,425; waliopo ni walimu 982 na upungufu ni walimu 443:- Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha kuondoa upungufu huo?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Pamoja na upungufu huu, kuna tatizo kubwa sana la mgawanyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua, ni kwa nini Wizara ya TAMISEMI inapanga moja kwa moja badala ya kuhakikisha kwamba Halmashauri ndiyo zinakuwa na huo utaratibu kwa sababu wao ndio wanajua upungufu wa Walimu? Kwa hiyo, nataka kujua na kazi za Maafisa Elimu sasa itakuwa nini?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kama ni wa sekta ya afya, basi Wizara ya Afya inaweza ikatoa tangazo na ikawaingiza kwenye ajira ya Serikali na baadaye taratibu nyingine za kiutumishi kufanywa na Wizara ya Utumishi na baadaye wale watumishi wanakabidhiwa TAMISEMI.
Mheshimiwa Naibu Spika, huko nyuma kulitokea matatizo kwamba tukiwapeleka huko hawafiki na ndiyo maana sisi TAMISEMI tukaamua kuwapangia mpaka na vituo vyao, lakini hatufanyi hivyo bila consultation na mamlaka husika, wanakuwa wanatuambia upungufu uko wapi na wapi na sisi tunaangalia kwa kuangalia ikama za shule husika au ikama za hospitali husika au zahanati au vituo vya afya husika ndiyo tunawapeleka. Ukiwaachia kule kinachotokea ni kitu cha ajabu kabisa cha tofauti sana na wengine hata hawafiki kule, ndio maana tulifanya hatua hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, endelea kutuamini tu kwa sababu bado tumefanya vizuri sana mpaka hao walimu wa sayansi ambao tumewapata, tulipowapangia, hawana option, wamekwenda mpaka kuripoti kwenye shule hizo. Ahsante sana.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Wilaya ya Bukombe ina mahitaji ya walimu wa shule za msingi 1,425; waliopo ni walimu 982 na upungufu ni walimu 443:- Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha kuondoa upungufu huo?

Supplementary Question 4

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Upungufu wa walimu umekuwa mkubwa sana kwenye Halmashauri za Wilaya ukilinganisha na Halmashauri za Mji. Je, ni lini Serikali itaweka mgawanyo sawa kwa walimu katika hizi shule zetu za msingi ili kuwe na usawa katika ufaulu wa wanafunzi? Maana yake ilivyo sasa hivi, kuna inequalities. Ukiangalia shule za mjini zinafaulisha vizuri zaidi kuliko za vijijini.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, suala la mgawanyo wa walimu lina mambo mengi, kuna scenario ambayo ipo na hapa tulitoa maelekezo mara kadhaa. Utakuta katika Halmashauri moja hiyo hiyo, walimu wamefika, lakini walimu wengi wanabakia katika vituo vya mijini na hii utakuja kuona sehemu ya vijijini kule walimu wanakuwa hawapo. Ndiyo maana sasa hivi TAMISEMI tunaangalia kwamba kila mikoa tupeleke idadi ya walimu na kila Halmashauri tupeleke idadi ya walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, napenda kutoa maelekezo mengine tena hapa kwamba Maafisa Elimu wote wa Wilaya wahakikishe wanafanya ile distribution ya walimu katika maeneo mbalimbali, wasiwaache walimu katika kituo kimoja cha mjini. Jambo hilo limejitokeza pale Mbeya. Nilipofika Mbeya, shule moja pale mjini ina walimu mpaka wanabadilishana vipindi, lakini shule nyingine ina walimu wawili peke yake. Hili jambo haliwezekani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili ni agizo kwa Maafisa Elimu wote wa Wilaya katika Halmashauri zote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wahakikishe wanafanya re-distribution ya Ualimu katika maeneo. Lengo ni kwamba hata kule vijijini walimu waweze kuwepo wanafunzi wapate taaluma inayokusudiwa.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Wilaya ya Bukombe ina mahitaji ya walimu wa shule za msingi 1,425; waliopo ni walimu 982 na upungufu ni walimu 443:- Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha kuondoa upungufu huo?

Supplementary Question 5

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Sambamba na hilo, tunajua walimu ni changamoto pamoja na kwamba Serikali imefanya kazi kubwa na nzuri katika jambo hili. Kwenye eneo la shule ya Kimambi; na shule ya Kimambi iko kwenye mpaka wa Liwale na Kilwa. Shule hii ina upungufu sana na walimu na sasa hivi kuna walimu wasiozidi watatu. Hata hivyo walimu wakipangiwa ndani ya Mkoa wa Lindi hasa kwenye vile vijiji wengi hawaripoti na hata wanaporipoti kinachojitokeza ni kutorudi kwenye maeneo yao. Serikali inasemaje juu ya jambo hili? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli shule anayozungumza mama yangu ni kweli shule ambayo kwa kweli ipo mpakani. Na mimi nilipokuwa nikisafiri, nikienda Liwale, nikizunguka Mkoa wa Lindi, ukiangalia kijiografia ni shule ambayo ipo mbali zaidi. Kama taarifa ya sasa, shule ya Kimambi ambayo inaonekana ina walimu watatu, naomba tulichukue hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo naomba niseme kwamba Afisa Elimu wa eneo hili sasa kupitia chombo hiki, leo tuko live, nimwelekeze kuhakikisha kwamba shule ile anaitembelea na by Ijumaa tupate status kwamba amefanya nini kuhakikisha shule hiyo inakuwa na walimu kama katika maeneo mengine yalivyokusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili tuondoe sana suala la uonevu katika maeneo mengine, wengine wanaonekana kama hawana thamani kuliko sehemu nyingine, sasa wale tuliowapa dhamana katika Wilaya zetu wahakikishe wanafanya kazi hiyo kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma inayostahiki katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, niwie radhi sana, nilitaka kuongezea kwenye jibu la Naibu Waziri kwamba ni kweli walimu hawa au watumishi hawa tunapowapangia wanakutana pia na changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli pia kwamba mazingira ya nchi yetu hayako sawa yote. Yako maeneo yana hali mbaya sana kimazingira, kimiundombinu na huduma nyingine; lakini kubwa ni nyumba za watumishi. Kusema ukweli ni jukumu la mamlaka hizi za Serikali za Mitaa kuangalia mazingira hayo na hata watumishi hao wanaporipoti kuwasaidia kwa kiasi kinachotosheleza ili waweze kukubali kwenda kukaa maeneo yale.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunaweza kuwapangia; lakini unampangia mtu anafika toka siku kwanza mtoto wa kike analia tu mpaka unashangaa amekonda, amepunguza, hata yaani alivyokuja ni tofauti na hawa ni watoto wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tuwe wakweli, Wakurugenzi wetu wakati mwingine wanayoyafanya siyo sawa. Hivi kumpatia usafiri binti mdogo au kijana mdogo anayeanza kazi na Halmashuri ina rasilimali ikampeleka na gari mpaka kile kituo wakampokea vizuri, lakini sehemu nyingine wanafanya na sehemu hawafanyi. Hili jambo ndilo linalopelekea kuwa na upungufu katika baadhi ya maeneo.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nisisitize na niseme hapa, sisi Wabunge ndio walezi, ndio viongozi kwenye maeneo husika. Tuwe karibu sana; tunaposikia watumishi wamepangwa, tujue hatma yao na mpaka siku watakapokwenda kuripoti kwenye vituo kama jukumu letu kama walezi lakini pia kama tunawajibisha mamlaka husika ili zitekeleze wajibu wao. (Makofi)