Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 59 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 489 2017-07-04

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:-
Wilaya ya Bukombe ina mahitaji ya walimu wa shule za msingi 1,425; waliopo ni walimu 982 na upungufu ni walimu 443:- Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha kuondoa upungufu huo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko, Mbunge wa Bukombe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua upungufu wa walimu uliopo nchini ambapo mahitaji ya walimu wa shule za msingi ni walimu 235,632; waliopo ni walimu 188,481 na upungufu ni walimu 47,151.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imejipanga kuajiri watumishi wa kada mbalimbali wakiwemo walimu wa shule za msingi ili kupunguza pengo lililopo. Aidha, Serikali inakamilisha mpango wa kuwahamishia shule za msingi walimu wa ziada wa masomo ya sanaa wanaofundisha shule za sekondari. Utaratibu huu utasaidia shule za msingi kupata walimu wa kutosha ili kuboresha taaluma.