Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:- Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji; hata hivyo Wenyeviti hao wamekuwa wakifanya kazi kwa kujitolea bila kulipwa posho za kujikimu na Serikali imekuwa ikiahidi kuangalia uwezekano wa kuwalipa posho za kujikimu viongozi hao:- Je, ni lini sasa Serikali itaacha kuendelea kuahidi juu ya malipo hayo na kuanza utekelezaji kwa kuanza kuwalipa viongozi hao posho?

Supplementary Question 1

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ni muda mrefu sasa Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa wamekuwa wanadai fadha zao na hawajui ni lini watalipwa malimbikizo haya. Je, sasa Serikali iko tayari kuziagiza halmashauri kupitia Wakurugenzi kuandaa idadi ya fedha ambazo kila halmashauri inadaiwa na viongozi hawa ili Serikali baadaye itoe maelekezo ya namna ya kuwalipa viongozi hawa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa sina hakika kama katika maelekezo haya ya kuwalipa Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa kama pako mahali panaeleza wanalipwa kiasi gani. Je, Serikali sasa iko tayari kutamka hapa kwamba hizo asilimia 20 ambazo zinapelekwa hao Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa watalipwa kiasi gani kila mmoja kwa mwezi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna halmashauri zingine zinafanya vizuri lakini kuna zingine ni changamoto kubwa. Ukipita huko kwenye halmashauri nyingine utaona kwamba zile asilimia 20 marejesho hayajarudi vijijini. Hata hivyo, tumetoa maelekezo mbalimbali, lakini naomba tutoe maelekezo tena na tutatoa maelekezo kwa waraka maalum kwamba jinsi gani sasa halmashauri hasa Wakurugenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapokaa katika Kamati ya Fedha katika ajenda ya mapato na matumizi sisi tukiwa wajumbe lazima tuangalie ile compliance ya kurudisha zile fedha katika halmashauri zetu. Bahati mbaya sana katika sehemu nyingine utakuta Ma- DT wanakuwa kama Miungu watu, hawafanyi maelekezo ya Kamati zao za Fedha wanapofanya maamuzi. Kwa hiyo, jambo hili tutatoa maelekezo mengine ya ziada ili asilimia 20 ya fedha hizi ziwewe kurudi vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo katika suala zima la kupeleka hizi asilimia 20 mara nyingi zina-differ kutoka halmashauri kwa halmashauri, ndiyo maana tumesema kwamba tunafanya marekebisho ya Sheria ya Fedha ambayo humpa Waziri mwenye dhamana katika kifungu maalum, nadhani katika ibara namba 45, dhamana ya kutoa maelekezo maalum ya namna ya kufanya. Jambo hili lisiwe ni jambo la hiari isipokuwa liwe ni kwa mujibu wa sheria. Lengo kubwa ni kuwasaidia Wenyeviti wetu wa Serikali za Mitaa na Vijiji. (Makofi)

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:- Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji; hata hivyo Wenyeviti hao wamekuwa wakifanya kazi kwa kujitolea bila kulipwa posho za kujikimu na Serikali imekuwa ikiahidi kuangalia uwezekano wa kuwalipa posho za kujikimu viongozi hao:- Je, ni lini sasa Serikali itaacha kuendelea kuahidi juu ya malipo hayo na kuanza utekelezaji kwa kuanza kuwalipa viongozi hao posho?

Supplementary Question 2

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Nadhani wote tunatambua umuhimu wa Wenyeviti wa Mitaa na kazi wanazozifanya, lakini kumekuwa na kilio cha muda mrefu sana kuhusiana na maslahi yao kwa kazi kubwa wanayoifanya. Je, Serikali sasa iko tayari kutenga bajeti kwa ajili ya kuwalipa mishahara Wenyeviti wa Mitaa pamoja na Madiwani?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili nililijibu takribani wiki mbili zilizopita na nikasema kwamba kwa jambo la kulipa mishahara utaratibu wa sasa ni kulipa posho. Pale Bunge litakapoamua vinginevyo, tutaangalia jinsi ya kufanya. Kikubwa zaidi ni kwamba tutaendelea na utaratibu huu, lakini tujue kwamba endapo jambo hili litaingia katika mshahara maana yake ni kuwa wage bill lazima itabadilika katika utaratibu wa kiserikali, ambayo vile vile ina changamoto yake. Kwa hiyo lazima tufanye analysis ya kutosha juu ya namna ya kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa utaratibu
wa sasa hivi tutaendelea kwa mujibu wa sheria inavyozungumza. Bunge litakapoamua hapo baadaye tutaenda na maamuzi hayo ambayo Bunge litakuwa limeamua hapo baadaye.

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:- Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji; hata hivyo Wenyeviti hao wamekuwa wakifanya kazi kwa kujitolea bila kulipwa posho za kujikimu na Serikali imekuwa ikiahidi kuangalia uwezekano wa kuwalipa posho za kujikimu viongozi hao:- Je, ni lini sasa Serikali itaacha kuendelea kuahidi juu ya malipo hayo na kuanza utekelezaji kwa kuanza kuwalipa viongozi hao posho?

Supplementary Question 3

MHE. ZITTO Z. R. KABWE: Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma-Ujiji tuliamua kutumia sehemu ya ushuru ambao manispaa inakusanya kwa ajili ya kuongeza fedha za kuwalipa watu hawa, Wenyeviti wa Mitaa pamoja na kuwalipia Bima ya Afya. Hata hivyo, kutokana na hatua ambayo Serikali Kuu imechukua, mmechukua kodi ya majengo, ushuru wa mabango, haya maelekezo mnayoyatoa kwamba halmashauri ziwalipe hawa watu hizi 20 percent zitatoka wapi wakati ushuru wote, mapato yote Serikali Kuu inayachukua? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nasema hiyo ni the best practice ambayo mmeifanya na tunataka innovative idea kama hizo wakati mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, suala la kuchukua fedha Serikali kupitia Wizara ya Fedha, Waziri wa Fedha alizungumza wazi, kwamba kinachofanywa na Serikali Kuu ni kukusanya baadaye inarudisha katika halmashauri husika; hii ilikuwa ni wazi kabisa, utaratibu wote ambao Mheshimiwa Waziri wa Fedha alizungumza, kutokana na hamasa nzuri, ndiyo maana leo hii tunaona jinsi ambavyo watu wanapanga foleni TRA kwenda kulipa kodi ya majengo. Kwa hiyo kikubwa zaidi naomba tukubaliane na Serikali, lengo la Serikali ni kusukuma mambo yaende vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunachokihitaji ni kwamba tufike Taifa ambalo linaweza kuamua kufanya mambo vizuri zaidi. Kwa hiyo, tutachukua zile best practice ambazo sehemu mbalimbali zipo. Hata hivyo niseme kwamba Serikali haikuwa na nia ya kunyang’anya authority ya halmashauri katika kuchukua mapato, isipokuwa ni utaratibu tu unawekwa halafu baadaye tutaona nini faida ya jambo hili ambalo ni jipya, lakini ambalo kwetu lina msingi mkubwa sana.