Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 58 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 480 2017-07-03

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL aliuliza:-
Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji; hata hivyo Wenyeviti hao wamekuwa wakifanya kazi kwa kujitolea bila kulipwa posho za kujikimu na Serikali imekuwa ikiahidi kuangalia uwezekano wa kuwalipa posho za kujikimu viongozi hao:-
Je, ni lini sasa Serikali itaacha kuendelea kuahidi juu ya malipo hayo na kuanza utekelezaji kwa kuanza kuwalipa viongozi hao posho?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omary Ahmed Badwel, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inathamini na kutambua kazi kubwa na nzuri inayofanywa na viongozi wa vijiji na mitaa katika kusimamia shughuli za maendeleo katika ngazi ya msingi ya Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka utaratibu ambapo posho za viongozi wa Serikali za vijiji na vitongoji zinalipwa na Halmashauri kupitia asilimia 20 iliyotengwa kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri na kurejeshwa kwenye vijiji. Napenda kutoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge tushirikiane katika kuzisimamia Halmashauri kuhakikisha fedha hizo zinatengwa na kulipwa posho stahiki. Hata hivyo, kutokana na baadhi ya halmashauri kushindwa kutekeleza suala hili kikamilifu, suala la kutenga asilimia 20 litawekwa katika sheria kwenye Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa ambayo inatarajiwa kuletwa Bungeni ili kurekebisha kasoro zilizopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ni kuendelea kuimarisha makusanyo ya mapato ya ndani ili kujenga uwezo mkubwa zaidi wa kulipa posho hizo.