Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Serikali inapeleka umeme vijijini kupitia mpango wa REA lakini kuna maeneo mengi ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme kwenye kijiji cha Mlalo, Bagamoyo, Mngaza na Kieti kwenye kata ya Vugiri? (b) Je, ni lini Serikali itafikisha umeme kwenye kata mpya ya Mpale?

Supplementary Question 1

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza kufuatana na Wizara hii kufanya kazi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, REA ya Awamu ya Pili ilikuwa ina sehemu ambayo imepima lakini sehemu hizo mpaka leo hii bado hazijapata umeme. Mfano ni katika kata ya Magoma katika kijiji cha Makangala na Mwanahauya na Pemba na katika kata ya Kerenge katika vitongoji vya Ntakae, Mianzini, Kwaduli, Migombani, Mfunte na Kiangaangazi. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka kuhakikisha kwamba vijiji hivi na ile vya Kata mpya ya Mpale vinapata umeme kwa haraka?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Ngonyani kwa jinsi ambavyo anashughulikia maendeleo ya umeme kwa jimbo lake, hongera sana Mheshimiwa Ngonyani.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuonesha tuna mkakati gani kwanza kabisa upatikanaji wa fedha ya mradi huu unakwenda vizuri na ni mkakati mzuri. Nimhakikishie Mheshimiwa Ngonyani vijiji vyake vitapata umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na kwamba ana wasiwasi na Kata ambazo ametaja za Magoma, Kelege pamoja na Mazizini lakini yako maeneo ya Foroforo pamoja na Majimoto Mheshimiwa Ngonyani atapata umeme kupitia mradi huu. (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Serikali inapeleka umeme vijijini kupitia mpango wa REA lakini kuna maeneo mengi ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme kwenye kijiji cha Mlalo, Bagamoyo, Mngaza na Kieti kwenye kata ya Vugiri? (b) Je, ni lini Serikali itafikisha umeme kwenye kata mpya ya Mpale?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Korogwe Vijijini linafanana sana na Jiji la Mbeya ambalo linapanuka kwa kasi, jiji hili kwenye kata za pembezoni ambazo ni Tangano, Iduda, Itezi, Iganjo, Nsomwa, Sanga, Mwasekwa na Msalaga hazina kabisa umeme na ni kwa muda mrefu sana. Kata hizi mazingira yake yamekaa kwa mfumo wa REA na tunashukuru kwamba REA Awamu ya Tatu ilishazinduliwa katika Mkoa wa Mbeya. Swali langu ni kwamba Serikali ina mkakati gani wa kuvipatia umeme vijiji hivi ambavyo kwa TANESCO inaelekea imeshindikana?Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Mwanjelwa kwamba hata TANESCO bado inapeleka umeme katika maeneo mbalimbali kufuatana na bajeti zake. Tumeshakaa na Mheshimiwa Mbunge na ni kweli kabisa yako maeneo yenye utata kidogo kama eneo la Uyole.
Hata hivyo, vijiji anavyotaja vya Idunda, Kasilanda pamoja na vingine baadhi yake vipo kwenye miradi ya REA. Kwa hiyo, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge tuone vijiji vinavyoingia mijini vitabaki TANESCO na vile ambavyo viko kwenye vijiji vitapelekewa umeme kupitia miradi ya REA.

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Serikali inapeleka umeme vijijini kupitia mpango wa REA lakini kuna maeneo mengi ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme kwenye kijiji cha Mlalo, Bagamoyo, Mngaza na Kieti kwenye kata ya Vugiri? (b) Je, ni lini Serikali itafikisha umeme kwenye kata mpya ya Mpale?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu la Bagamoyo, vijiji vya Kondo na Kongo vilikuwa kwenye REA Awamu ya Pili lakini miradi hii haikutekelezwa na katika REA Awamu ya Tatu miradi ya vijiji hivi haimo. Nilishamsikia Mheshimiwa Naibu Waziri akitamka hapa Bungeni kwamba miradi yote ile ambayo haikutekelezwa kwenye Awamu ya Pili ndiyo itapata kipaumbele katika Awamu ya Tatu.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anawaambiaje wananchi wa vijiji vya Kongo na Kondo waliokwemo kwenye Awamu ya Pili lakini wamefutwa kwenye Awamu ya Tatu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nipende kusema viko vijiji kwa nchi mzima ambavyo havikutekelezwa katika scope ya REA Awamu ya Pili lakini vilikuwa ndani ya mradi. Vijiji vyote ambavyo vilikuwa chini ya REA Awamu ya Pili vitaendelea kutekelezwa katika Awamu ya Tatu ya REA.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Kawambwa kwamba vile vijiji vyake vya Kondo na Kongo na vingine, viko kama vijiji vinane hivi viko katika mradi wa REA Awamu ya Tatu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Dkt. Kawambwa aamini tu kwamba vijiji hivyo vitapatiwa umeme katika mradi wa REA Awamu ya Tatu ambao umeshaanza na tayari katika Mkoa wake wa Pwani tumefanya uzinduzi.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Shukuru Kawambwa kama kuna shida tutakaa lakini tumhakikishie vijiji vyake vitapata umeme kupitia mradi wa REA.

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Serikali inapeleka umeme vijijini kupitia mpango wa REA lakini kuna maeneo mengi ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme kwenye kijiji cha Mlalo, Bagamoyo, Mngaza na Kieti kwenye kata ya Vugiri? (b) Je, ni lini Serikali itafikisha umeme kwenye kata mpya ya Mpale?

Supplementary Question 4

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nilikuwa nimeanza kukata tamaa kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mji wa Geita tuna shida sana ya umeme na asilimia 70 ya vijiji vinavyozunguka Mji wa Geita viko katika giza. Ni lini Serikali itapeleka umeme katika kata za Nyanguku, Ihanamilo, Shiloleli, Bulela na Bugwagogo ili kuweza kusaidia katika huduma za jamii ambazo ziko katika maeneo hayo? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli vipo vijiji ambavyo havijapata umeme kwa Mji wa Geita na ametaja vitatu lakini viko zaidi ya ishirini. Nimhakikishie Mheshimiwa Peneza vijiji ambavyo ametaja vya Nyanguku na vingine baadhi yake viko katika mradi REA lakini viko katika mradi wa TANESCO. Bahati nzuri sana nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Mkoa wa Geita na mikoa ya jirani iliyokuwa inapata umeme wa low voltage sasa tunakamilisha ujenzi wa mradi wa kusafirisha umeme mkubwa unaotoka Mbeya kwenda Sumbawanga mpaka Nyakanazi na baadaye utatoka Nyakanazi mpaka Bulyankulu na baadaye Geita. Kwa hiyo, wananchi watapata umeme wa kilovoti 400 lakini tutaanza na kilovoti 220.
Kwa hiyo, napenda nimjulishe Mheshimiwa Upendo Pendeza kwamba vijiji hivyo vitapata umeme kupitia miradi ya REA na baadhi yake vitaendelea kupata umeme kupitia miradi ya TANESCO.

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Serikali inapeleka umeme vijijini kupitia mpango wa REA lakini kuna maeneo mengi ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme kwenye kijiji cha Mlalo, Bagamoyo, Mngaza na Kieti kwenye kata ya Vugiri? (b) Je, ni lini Serikali itafikisha umeme kwenye kata mpya ya Mpale?

Supplementary Question 5

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa uzinduzi wa REA Awamu ya Tatu Mkoani Tanga, Naibu Waziri alikuja na mimi nilihudhuria. Tulipata orodha ya vijiji na Muheza tulipewa vijiji 44 kwenye REA Awamu ya Tatu. Baadaye orodha hiyo ilipunguzwa vijiji saba vikakosekana ambavyo ni Kwakopwe, Kibaoni, Magoda, Mbambara, Kitopeni, Masimbani na Msowero. Nataka kufahamu hatma ya vijiji hivyo kama vitarudishwa ili waweze kupata umeme kwa sababu wameshaanza kufanya matayarisho ya kuanza kufunga nyaya? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa wakati tunazindua katika Mkoa wa Tanga na tulifanya uzinduzi katika maeneo ambayo ameyasema na katika utafiti ikaonekana viko vijiji saba au vinane hivi ambavyo vitaingia kwenye densification stage ya pili.
Mheshimiwa Adadi Rajab vijiji saba vitaendelea kupatiwa umeme, kilichofanyika densification inaanza kwanza kwa miezi kumi na tano. Baada ya miezi kumi na tano tutaendelea na miezi mingine kumi na mitano mpaka tukapofikia hatua ya kukamilisha vitongoji vyote.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi Rajab vijiji vyake saba si kwamba vimeondolewa bali vimepelekwa mbele ili baada ya miezi kumi tano na vyenyewe vitaanza kupelekewa umeme kwa utaratibu huu wa REA. Kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi awape faraja wananchi wake wa Muheza kwamba bado watapelekewa umeme kupitia mradi huu.