Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 27 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 226 2017-05-17

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:-
Serikali inapeleka umeme vijijini kupitia mpango wa REA lakini kuna maeneo mengi ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme kwenye kijiji cha Mlalo, Bagamoyo, Mngaza na Kieti kwenye kata ya Vugiri?
(b) Je, ni lini Serikali itafikisha umeme kwenye kata mpya ya Mpale?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stephen Ngonyani, almaarufu Maji Marefu, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa Mradi Kabambe wa REA katika nchi nzima kama nilivyosema umeanza tangu mwezi Machi, 2017. Mradi huu utajumuisha vipengele vya mradi vitatu katika mikoa yote, Grid Densification, Grid Extension na Off-Grid Renewable. Katika eneo la Mheshimiwa vijiji vya Bagamoyo, Kieti, Mlalo na Mganza katika Kata ya Buhuli vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu utakaokamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme maeneo hayo itajumuisha ujenzi wa njia ya msongo wa umeme wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 6.6; ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 19; ufungaji wa transfoma saba pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 350. Gharama ya kazi hiyo ni shilingi bilioni 940.9