Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RIZIKI S. MNGWALI aliuliza:- (a) Je, Serikali ina utaratibu gani maalum wa kuwapangia na kuwahamisha sehemu za kazi watumishi wake? (b) Je, ni vigezo gani huzingatiwa katika kuwapanga au kuwahamisha watumishi sehemu za kazi? (c) Je, ni kwa namna gani Serikali inahakikisha watumishi wake wanafanya kazi kwa ufanisi katika maeneo waliyopangwa?

Supplementary Question 1

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Niseme tu majibu ya Serikali yamekuwa ni yale ya ought to be, rather than what is the real situation. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, je, Serikali inasema nini pale ambapo watendaji maalum kama DED, DAS, RAS na walimu wanapohamishwa kila baada ya muda mfupi katika Wilaya husika? Na mfano ni Wilaya Mafia ambapo katika miezi michache ma-DED walihamishwa na tukapata wapya kama watatu na hii ilitokana zaidi na jinsi walivyoendesha uchaguzi na kuusimamia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ufanisi sio tu kutunga sheria za kusimamia, hivi Serikali haioni kwamba masuala kama ya kuhakikisha watumishi wanapata makazi bora, wanalipwa stahiki zao ipasavyo na vilevile wana uhakika wa kuwa na periodic training za ku-upgrade zile nafasi zao ni namna za kujenga ufanisi katika utendaji kazi?Ahsante. (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kuzungumzia alipokuwa anasema kwamba tumejibu tu namna inavyotakiwa kuwa na siyo uhalisia. Sisi tunasimamia Menejimenti nzima ya Utumishi wa Umma na ndiyo maana tunatoa miongozo na taratibu mbalimbali na kuifuatilia. Ndiyo maana nimemueleza utaratibu kwa sababu yeye ameuliza utaratibu na vigezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali lake la kwanza kwamba ni kwa nini unakuta watumishi wengine wanahamishwa bila kufuata taratibu. Tumekuwa tukitoa nyaraka mbalimbali za kiutumishi, tumetoa Waraka kwa TAMISEMI mwaka 2006, tumetoa pia Waraka mwaka 2007 kwa Makatibu Tawala wa Mikoa kueleza ni namna gani na masuala gani yanayotakiwa kuzingatiwa wakati wanapohamisha watumishi. Pia katika jibu langu la msingi nimemueleza muuliza swali, lengo kubwa ni kuangalia manufaa ya umma, kuangalia uwiano katika Halmashauri zetu na katika sehemu zetu za kazi na si kwa kumkomesha mtu wala kwa lengo lolote, lakini kubwa zaidi ni kuhakiksha kwamba ikama na bajeti ya fedha imetengwa ili kuhakikisha kwamba mtumishi wa umma hapati usumbufu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumuongezea Mheshimiwa Mngwali, hata Mheshimiwa Rais ameweza kutoa msisitizo zaidi tarehe 1 Mei, 2017 wakati wa siku ya wafanyakazi. Maelekezo yamekuwa yakitoka lakini ameweka mkazo kwamba kuanzia sasa hakuna kumhamisha mtumishi yeyote wa umma kama gharama zake za uhamisho hazijatengwa na pia kama hakuna manufaa katika uhamisho huo na hakuna ufanisi wowote ambao unaenda kuongezeka katika kuboresha ikama hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la makazi pamoja na umuhimu wa mafunzo, niseme tu katika Sera ya Menejimenti ya Ajira katika Utumishi wa Umma pamoja na Sera ya Mafunzo, tunatambua umuhimu wa kuwa na mafunzo na watumishi wetu wa umma kuwa na makazi bora. Ndiyo maana kama Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania, Watumishi Housing, Shirika la Nyumba la Taifa, TBA na mashirika mengine tumekuwa tukiweka msisitizo na kuhakikisha kwamba nyumba zinajengwa kwa ajili ya watumishi wetu wa umma.
Vilevile katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wamekuwa mwaka hadi mwaka wakitenga fedha kwa ajili ya kujenga nyumba za watumishi wetu. Lengo kubwa likiwa ni kuwaboreshea watumishi wetu wa umma makazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini zaidi ya yote nitoe rai kwa waajiri wetu kuona ni namna gani wanaweza kuweka vivutio mbalimbali ili kuhakikisha kwamba wanavutia watumishi waweze kufanya kazi katika maeneo yao ya kazi. Zaidi katika mafunzo pia ni vema waajiri wakahakikisha kwamba kila mwaka wanatenga bajeti kwa ajili ya kuwapatia mafunzo watumishi wao na kuwaendeleza.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. RIZIKI S. MNGWALI aliuliza:- (a) Je, Serikali ina utaratibu gani maalum wa kuwapangia na kuwahamisha sehemu za kazi watumishi wake? (b) Je, ni vigezo gani huzingatiwa katika kuwapanga au kuwahamisha watumishi sehemu za kazi? (c) Je, ni kwa namna gani Serikali inahakikisha watumishi wake wanafanya kazi kwa ufanisi katika maeneo waliyopangwa?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Serikali kutoa miongozo na maelekezo mbalimbali kuhusu uhamisho wa watumishi, Halmashauri mbalimbali ikiwemo Halmashauri yangu ya Wilaya ya Ngara wameendelea kufanya uhamisho huo bila kulipa stahiki za uhamisho za watumishi hao na hivyo kuzalisha madeni. Je, Serikali inachukua hatua gani juu ya watendaji hawa ambao hawazingatii maelekezo wala mwongozo wa Serikali? (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza tumekuwa tukitoa maelekezo katika nyakati mbalimbali lakini nimefanya reference ya maelekezo ya mwisho ya Mheshimiwa Rais ya tarehe 1 Mei, 2017. Tumekuwa tukichukua hatua na mifano ya karibuni tu ni katika Halmashauri ya Kilombero na Bagamoyo ambapo wale ambao hawakuzingatia taratibu hizi waliweza kuchukuliwa hatua mbalimbali za kiutumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda tu kuwaeleza Wakurugenzi wetu na Mamlaka za Ajira wazingatie maelekezo haya. Ni lazima pindi wanapofanya uhamisho wawe wametenga fedha katika ikama, lakini vilevile wahakikishe kwamba lengo la uhamisho huo lina manufaa kwa umma na ni katika kuboresha ikama katika Halmashauri zetu.

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RIZIKI S. MNGWALI aliuliza:- (a) Je, Serikali ina utaratibu gani maalum wa kuwapangia na kuwahamisha sehemu za kazi watumishi wake? (b) Je, ni vigezo gani huzingatiwa katika kuwapanga au kuwahamisha watumishi sehemu za kazi? (c) Je, ni kwa namna gani Serikali inahakikisha watumishi wake wanafanya kazi kwa ufanisi katika maeneo waliyopangwa?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kutokupandisha madaraja kwa wakati, kutolipa na stahili za wafanyakazi kwa wakati na kufuta posho mbalimbali kumefanya ufanisi wa wafanyakazi kushuka. Je, Serikali ina mpango gani katika hilo? (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 13 Juni, 2016, tulitoa Waraka wa Utumishi kupitia kwa Katibu Mkuu tukitoa maelekezo mbalimbali. Lengo kubwa la Waraka huo tulikuwa na mazoezi mawili; zoezi la kwanza ni kupitia upya muundo wetu wa Serikali pamoja taasisi zetu kuhakikisha kwamba tuna muundo wenye ufanisi lakini zaidi kuhakikisha kwamba tuna muundo ambao unahimilika. Kama mnavyofahamu tumepunguza idadi ya Wizara kutoka 26 mpaka sasa tunazo 18 au 19.
Kwa hiyo, ni lazima pia na ni dhahiri kwamba baadhi ya taasisi ambazo zitakuwa na muingiliano wa majukumu nyingine itabidi ziweze kuunganishwa, lakini vilevile baadhi ya Idara na baadhi ya Vitengo vingine pia itabidi viweze kuunganishwa kuhakikisha kuwa tunaenda na wakati na tunaendana na mabadiliko.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kutokana na Waraka huo huo tuliahirisha zoezi la kupandisha madaraja pamoja na kupandisha watu vyeo. Napenda kumtoa hofu Mheshimiwa Mbunge kuanzia mwaka ujao wa fedha tutapandisha madaraja zaidi ya watumishi 193,166 na hakuna atakayepoteza haki yake.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RIZIKI S. MNGWALI aliuliza:- (a) Je, Serikali ina utaratibu gani maalum wa kuwapangia na kuwahamisha sehemu za kazi watumishi wake? (b) Je, ni vigezo gani huzingatiwa katika kuwapanga au kuwahamisha watumishi sehemu za kazi? (c) Je, ni kwa namna gani Serikali inahakikisha watumishi wake wanafanya kazi kwa ufanisi katika maeneo waliyopangwa?

Supplementary Question 4

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali na vigezo ambavyo vimetolewa vya upangaji na uhamishaji watumishi wa umma, je, Serikali haioni kuwa ulemavu nao uwe ni miongoni mwa vigezo ambavyo vimetolewa ili mtu mwenye ulemavu awe comfortable na hatimaye aweze kutimiza wajibu wake ipasavyo?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru kwa swali zuri au kwa ushauri. Hili ni eneo ambalo tutakwenda kuliangalia, tumekuwa tukiangalia sababu za kiafya, wengine kuwafuata wenzi wao, niseme na lenyewe tutalifanyia kazi ili kuona ni namna gani na hii pia inaweza kuwa ni moja ya kigezo.