Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwa na mpango kabambe wa Mfuko wa Afya wa Bima (CHF) ambao ni “Papo kwa Papo na Tele kwa Tele”’ na Watanzania waliopo Serengeti wamekuwa wakichangia huduma hiyo lakini kila waendapo kwenye matibabu hupewa cheti badala ya dawa. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya?

Supplementary Question 1

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kuna huu utaratibu wa MSD kwenda kwenda vituo vya Afya wamebeba, wanapeleka kondomu na mseto pakiti nane unaenda kwenye zahanati unakuta wamepeleka kondomu na mseto nane, huu utaratibu unasafirisha hivi vitu kutoka Mwanza mpaka kule Serengeti haukubaliki. Je, ninyi kama Wizara mnaona huu utaratibu uendelee?
Swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri umekuja pale Serengeti na Serengeti sasa ni Wilaya ya kitalii, tunapata watalii wengi lakini tulikupeleka kwenye ile Hospitali ya Wilaya ukaona umaliziaji wa ile OPD. Wizara mpo tayari kutoa fedha kwa ajili ya kumalizia ile OPD? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la upelekaji wa dawa MSD naomba nitoe ufafanuzi ifuatavyo:-
Ni kwamba dawa zinapofika kule kwanza kuna request ya kawaida inayopelekwa, lakini dawa zinapofika lazima Kamati ya Afya ya kituo husika lazima ihisike katika upokeaji wa dawa, lakini nitoe wito kwa Halmashauri ya Serengeti kwa sababu japo kuwa tumepeleka fedha nyingi pale kuna baadhi ya fedha zingine bado hazijatumika katika ununuzi wa dawa, kwa hiyo nikuombe Mheshimiwa Mbunge najua kwamba kwa sababu pale eneo lako lina changamoto kubwa tushirikiane vema kwamba kuhakikisha tunasukuma MSD dawa ambazo zimebakia karibuni za shilingi milioni 180 zifike pale site, lakini hali kadhalika mnao pesa nyingi zaidi za basket fund bado hazijanunua dawa, nitoe maelekezo hayo kwa Serengeti haraka iwezekanavyo dawa zipatikane kwa sababu tayari Serikali tumepeleka fedha.
Lakini katika suala la pili ni suala zima la hospitali tuliofika, ni kweli na mimi nimefika pale na tulivyoenda kuangalia tukasema ajenda ya Mheshimiwa Rais alipofika pale ni kuahidi kwamba atawahudumia wananchi na ndio maana katika kipindi cha sasa tumefanya commitment zile wodi mbili tutazifanya two wards in one, tutafanya zoezi kubwa pale la kupeleka takribani tutaweka nguvu karibu shilingi milioni 700 lengo kubwa ni kufanya ahadi ya Mheshimiwa Rais katika maeneo mbalimbali iweze kutekelezeka. Kwa hiyo hili ni jukumu la Serikali tunaenda kulitekeleza. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwa na mpango kabambe wa Mfuko wa Afya wa Bima (CHF) ambao ni “Papo kwa Papo na Tele kwa Tele”’ na Watanzania waliopo Serengeti wamekuwa wakichangia huduma hiyo lakini kila waendapo kwenye matibabu hupewa cheti badala ya dawa. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bima kwa Wote ni utaratibu ambao ungeweza kusaidia sana wananchi wanyonge kuweza kupata huduma nzuri za afya kwa gharama nafuu, lakini vilevile ingesaidia serikali kupata mapato ya kuendesha huduma za afya, sasa nataka kuuliza ni lini Serikali italeta Muswada wa Sheria wa Bima ya Wote (Universal Coverage) kwa ajili ya kujadiliwa hapa Bungeni?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili lipo katika negotiation ambapo wadau mbalimbali wameenda kushiriki na Wizara ya Afya na Wizara yetu inaangalia utaratibu mzuri, naomba niseme kwamba Serikali imejipanga katika hili na si muda mrefu baada ya wataalam kupita katika ngazi mbalimbali basi Serikali itakavyoona kwamba huu muswada sasa umeiva, basi utakuja hapa Bungeni kwa ajili ya kufanya maamuzi hayo.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwa na mpango kabambe wa Mfuko wa Afya wa Bima (CHF) ambao ni “Papo kwa Papo na Tele kwa Tele”’ na Watanzania waliopo Serengeti wamekuwa wakichangia huduma hiyo lakini kila waendapo kwenye matibabu hupewa cheti badala ya dawa. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa tatizo lililopo Serengeti linafanana kabisa na tatizo lililopo katika Tarafa ya Mtae, Shagayu, Sunga na Rangu, wananchi wamehamasika kuchangia huduma za CHF lakini wanapokwenda kwenye Kituo cha Afya cha Mtae huduma hakuna. Je, Serikali inawambiaje wananchi hawa wa Tarafa Mtae?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niweke rekodi sawa kwamba bahati nzuri tulikuwa na Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lake kipindi kile wakati nilipokwenda kutembelea Wilaya ya Lushoto. Ni kweli kwa sababu tumegundua changamoto ya afya ipo kubwa zaidi ndio maana katika vipaumbele vyetu tumeamua kukiteua hiki Kituo cha Afya cha Mtae ni miongoni mwa vituo ambavyo ndani ya mwezi huu mmoja unaokuja tutaenda kufanya ujenzi wa maternity ward pale na kufanya ukarabati mkubwa lengo kubwa wananchi wa Mtae na maeneo ya jirani waweze kupata huduma nzuri katika eneo lile.

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwa na mpango kabambe wa Mfuko wa Afya wa Bima (CHF) ambao ni “Papo kwa Papo na Tele kwa Tele”’ na Watanzania waliopo Serengeti wamekuwa wakichangia huduma hiyo lakini kila waendapo kwenye matibabu hupewa cheti badala ya dawa. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya?

Supplementary Question 4

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Ahsante Mwenyekiti, nipende tu kuuliza swali kwamba Wilaya ya Bunda ina hospitali moja ambao ni Hospitali ya Manyamanyama, na ile hospitali ya Manyamanyama inaitwa Hopsitali ya Wilaya, lakini haina hadhi kama Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Waziri, je, ni lini itakuwa na kiwango kama Hospitali ya Wilaya na dawa zipelekwe kama Hospitali ya Wilaya? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na tulipofika pale Bunda tulitembelea yale maeneo yote tukaona kwamba kuna changamoto kubwa na hili tulitoa maelezo katika maeneo mbalimbali, hata hivyo kwa ajili ya the backup strategy ya kufanya kwa Bunda na kwa sababu ukiangalia kwa ndugu yangu Kangi Lugola wagonjwa wote wanakuja pale, kwa ndugu Boniphace wagonjwa wote wanakuja pale, ndio maana sasa hivi kwa muda unaokuja na si muda mrefu sana japo tunaweka mikakti ya ile sehemu ya Manyamanyama pale lakini katika eneo la Mgeta tunakwenda kutengeneza kituo cha afya tunakwenda kukiimarisha kwa kiwango kikubwa lengo kubwa ni kupunguza idadi ya wagonjwa wanaokuja pale kuweza kuhakikisha kwamba akina mama na watoto afya zao tunazilinda vizuri.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwa na mpango kabambe wa Mfuko wa Afya wa Bima (CHF) ambao ni “Papo kwa Papo na Tele kwa Tele”’ na Watanzania waliopo Serengeti wamekuwa wakichangia huduma hiyo lakini kila waendapo kwenye matibabu hupewa cheti badala ya dawa. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya?

Supplementary Question 5

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Sera ya nchi na ya Serikali ni kuhakikisha kwamba kila kijiji na kila kitongoji kuna kuwa na zahanati, na katika mji wa Tunduma katika mtaa wa Makambini eneo la Sogea wananchi wameamua kujenga zahanati katika eneo ambalo lilikuwa limetengwa na Serikali, lakini kutokana na mgogoro uliokuwepo na ambao alikuja kuumaliza Naibu Waziri wa Ardhi, alitoa maelezo kwamba eneo hilo lisianze kujengwa mpaka atakavyotoa ruhusa ya wananchi kuendelea kujenga Zahanati pale. Je, ni lini atatoa ruhusa ili wananchi wa mji wa Tunduma eneo la Makambini waweze kuendelea na ujenzi wa zahanati kama ambavyo sera za nchi zinasema?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nadhani Mheshimiwa Waziri wa Afya alivyopita pale wananchi waliandamana katika suala zima katika kituo kile cha afya nadhani tutafanya utaratibu kupitia ofisi yetu ya TAMISEMI nini kifanyike, lakini kutokana na changamoto ya Tunduma kwa sababu ukipita pale siku niliyopita pale population ni kubwa sana na ndio maana tunaamua kwenda kukiimarisha kituo cha Chipaka na lengo kubwa ni kwamba angalau ile kituo cha afya cha Chipaka kiweze kuwa accommodate wagonjwa wengi na tunakwenda kufanya kazi hizyo muda si mrefu ndani ya mwezi mmoja ujao kwa ajili ya wananchi wa Tanzania lengo letu ni kuboresha maeneo yale.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwa na mpango kabambe wa Mfuko wa Afya wa Bima (CHF) ambao ni “Papo kwa Papo na Tele kwa Tele”’ na Watanzania waliopo Serengeti wamekuwa wakichangia huduma hiyo lakini kila waendapo kwenye matibabu hupewa cheti badala ya dawa. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY K. MOHAMED:Ahsante sana Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi bima za afya baadhi ya maduka na hospitali zinatumika vibaya, kuzidisha double allocation mtu anaenda kutibiwa anaweza akaandikwa double akaiga saini ya mteja au na zingine zinazidisha bei mara mbili, je, nani anazikagua bima ya afya kabla ya malipo, kwa kuwa zinaendesha wizi wa hali ya juu.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti ni kweli kwa kipindi kirefu sasa hata ukija kuangalia wakati mwingine kuna takwimu na kuna fraud inafanyika katika hizi document hasa za bima ya afya na ndio maana sasa hivi utaratibu wa bima ya afya imeweka sasa hivi document ambayo haijakaa vizuri hawawezi kuilipa, lakini hili sasa naomba niwa sisitize hasa katika wenzetu wa bima ya afya wahakikishe wanaweka mechanisim nzuri ya kuweza kuangalia tuna monitor hizi fomu zinajazwa vizuri, lakini sio kujazwa tu, iangalie ili mradi compliance kwamba fomu iliyojazwa ndio kweli iliyotoa matibabu.
Kwa hiyo Mheshimiwa Keissy naomba tuichukue hoja hii kwa sababu ni hoja ya msingi tunaenda kulinda fedha za wananchi, fedha za serikali tutaenda kulisimamia vizuri kwa kadri iwezekanavyo.