Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 264 2017-05-24

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:-
Kumekuwa na mpango kabambe wa Mfuko wa Afya wa Bima (CHF) ambao ni “Papo kwa Papo na Tele kwa Tele”’ na Watanzania waliopo Serengeti wamekuwa wakichangia huduma hiyo lakini kila waendapo kwenye matibabu hupewa cheti badala ya dawa.
Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la ukosefu wa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mala Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa dawa unategemea upatikanaji wa fedha kupitia Mfuko wa Afya wa Pamoja ambapo Halmashauri hiyo imeshapokea fedha zote kiasi cha shilingi milioni 826.4 zilizotengwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri imepanga kutumia shilingi milioni 843 kwa ajili ya upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya vilivyopo. Kupitia Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Halmashauri zinakusanya mapato yatokanayo na uchangiaji kwa kuzingatia sheria ndogo za Halmashauri ambapo kipaumbele ni upatikanaji wa dawa. Natumia fursa hii kuzikumbusha Halmashauri kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuendelea kuhamasisha wananchi kuchangia mfuko.