Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SABREENA H. SUNGURA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza ajali za barabarani?

Supplementary Question 1

MHE. SABREENA H.SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini bado kuna mambo ya msingi ambayo yanapelekea ajali za barabarani kuendelea kutokea ambayo hayajakuwa mentioned katika majibu yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hususani njia inayoelekea Kigoma, kuanzia Itigi kwenda Tabora mpaka Kigoma, tumekuwa na railway cross nyingi sana katika eneo hilo, lakini nyingi katika hizo hazijawekewa alama kiasi kwamba msafiri anapokuwa anaendesha ama madereva wanapokuwa wanaendesha wanashindwa kutambua. Ni kwa mita chache sana alama hizo zipo na maeneo mengine alama hizo hakuna kabisa, kitu ambacho kinaweza kikapelekea sasa magari yetu na treni zije zisababishe ajali kubwa hapo baadaye. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba wana-fix vibao vinavyoonesha railway cross barabarani katika njia hiyo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa kumekuwa na shida kubwa sana hasa ya wafugaji, hususani wafugaji wa ng’ombe, hufuga maeneo ambayo ni pembezoni mwa barabara na wakati mwingine ng’ombe wale hupelekea ajili zisizokuwa za msingi na kwa kuwa kumekuwa na tendence ya traffic hasa katibu miji mikubwa kama Mwanza, Dar es Salaam, Dodoma na kadhalika, hususani Dar es Salaam ambapo taa za barabarani zinafanya kazi, hapo hapo na traffic wanafanya kazi, kitu ambacho kinapelekea ku-confuse madereva barabarani na kuweza kusababisha ajali.
Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya mambo haya mawili?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumekuwa tukikabiliana na changamoto za kukosekana katika baadhi ya maeneo alama za barabarani zinazotakiwa kuelekeza madereva kuona maeneo ambayo ni hatarishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kulitambua hilo ndiyo maana katika jibu langu la msingi nilieleza kati ya mikakati 14 moja katika eneo tulilokuwa tulifanyia kazi ni eneo hilo na kwamba tumejaribu kwa kiasi kikubwa sana kuweza kuwasiliana na kufanya kazi kwa karibu na mamlaka husika ili kuweza kudhibiti na kuweka hizo alama ambazo anasema kuwa zimekosekama. Bahati nzuri Makamu Mwenyekiti wa Baraza letu la Usalama Barabani ni Mheshimiwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, kwa hiyo tumelifanya hili kwa ufanisi mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa ambalo linasababisha alama hizi kupotea. Mara nyingi ni kutokana na tabia mbaya za baadhi ya wananchi ambao wamekuwa waking’oa kwa makusudi alama za barabarani na kuvitumia vyuma hivi kama vyumba chakavu. Naomba nitoe wito kwa wananchi kuacha tabia hiyo na kwamba mamlaka husika ziko macho kwa wale wote ambao watakiuka sheria za nchi, kwa kung’oa vibao vya alama hizi tutawachukulia hatua za kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili lilikuwa linahusiana na askari wa barabarani pamoja na taa za barabarani. Mara nyingi askari wa barabarani wanakaa wakati ambao kuna msongamano wa magari barabarani, hasa wakati wa asubuhi wakati watu wanakwenda kazini na wakati wa jioni wanapokuwa watoka kazini. Hii ni kwa sababu taa za barabarani zilipowekwa haziwezi kukidhi mahitaji ya nyakati husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo kuna wakati ambao kuna msafara mwingi unatokea katika upande mmoja, kwa hiyo kutegemea taa za barabarani peke yake kunaweza kusababisha msongamano mkubwa. Kwa maana hiyo hao traffic police wanakaa pale kwa lengo la kudhibiti na kuzuia msongamano huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaendelea kuhakikisha kwamba askari hao wanaendelea kutumika kusaidia kupunguza msongamano wa magari hasa katika nyakati hizo za watu ambao wanakwenda kazini na kurudi kazini asubuhi na jioni.

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. SABREENA H. SUNGURA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza ajali za barabarani?

Supplementary Question 2

MHE. RICHARD P.MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nina swali dogo kuhusiana na makazi ya Katumba, yaliyokuwa makazi ya wakimbizi. Makazi haya ya Katumba yana barabara takribani nne ambazo zinaingia kwenye eneo hilo. Tuna barabara kuu ya kijiji cha Msaginya ambako kuna geti ambalo limekuwa ni usumbufu mkubwa kwa wananchi wa Katumba hususani kuanzia saa 12.00 jioni kutokana na sheria za wakimbizi. Sasa kwa kuwa wananchi wa eneo hilo takribani asilimia 90 wameshapewa uraia na wengine hawaishi ndani ya eneo hilo.
Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka kwa lile geti la Msaginya kuendolewa au muda kuongezwa hata ikawa saa 24?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake tumelichukua na tutalitafakari tuone jinsi gani tutalifanyia kazi.