Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 12 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 98 2017-04-25

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SABREENA H. SUNGURA aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza ajali za barabarani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sabreena Hamza Sungura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeandaa mkakati wa kudhibiti makosa yanayosababisha madhara makubwa ambayo hupelekea ajali za barabarani kuongezeka. Mambo yaliyolengwa katika mkakati pamoja na mambo mengine ni:-
(1) Udhibiti wa madereva walevi na kuendesha kwa uzembe;
(2) Udhibiti wa mwendokasi kwa madereva na wamiliki wa magari , kuwa na madereva wenza kwa mabasi ya safari za zaidi ya masaa manane;
(3) Kuthibiti uendeshaji magari bila sifa/leseni za udereva ama Bima;
(4) Kudhibiti usafirishaji wa abiria kutumia magari madogo yenye muundo wa tairi moja nyuma;
(5) Kusimamia matumizi ya barabara kwa Makundi Maalum mfano watoto, wazee, walemavu na wasiotumia vyombo vya moto ikiwemo mikokoteni na baiskeli;
(6) Kudhibiti ajali za pikipiki za magurudumu mawili (bodaboda) na magurudumu dumumatatu (bajaji);
(7) Kuzishauri mamlaka husika kuweka alama za kudumu za utambulisho kwenye maeneo hatarishi ya ajali;
(8) Kusimamia utaratibu wa nukta (Point System) kwenye leseni za udereva;
(9) Marekebisho ya Sheria za Usalama Barabarani;
(10) Abiria kufunga mikanda ya usalama wanapotumia vyombo vya usafiri;
(11) Kubaini maeneo tete na hatarishi ya ajali za barabarani;
(12) Kuthibiti utoaji na upokeaji rushwa barabarani;
(13) Motisha kwa askari wanaosimamia vizuri majukumu yao; na
(14) Kuwajengea uwezo wa kiutendaji askari wa usalama barabarani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nidhahiri kwamba suala la usalama barabarani siyo la kundi au taasisi moja tu ila ni letu sote. Wabunge ni miongoni mwa wahusika wa suala la usalama barabarani, kwa maana kuwa nafasi yao kubwa ni katika kuelimisha umma na kusaidia katika ujenzi wa utamaduni wa kuheshimu alama za usalama barabarani nchini.