Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Mkoa wa Kilimanjaro una tatizo la uhaba wa magari ya zimamoto; gari linalofanya kazi mpaka sasa ni moja tu, hivyo kufanya huduma ya zimamoto kuwa duni sana. (a) Je, ni lini Serikali itaongeza magari mengine mawili ili kusaidia shughuli za zimamoto na kuepusha hasara zinazowakabili wananchi wanaopata majanga ya moto? (b) Je, Serikali haioni kwamba uamuzi wa kuhamishia Kitengo cha Zimamoto Wizara ya Mambo ya Ndani umeiongezea mzigo Wizara hiyo na kupunguza ufanisi wa shughuli za zimamoto?

Supplementary Question 1

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Serikali nilikuwa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Kitengo cha Zimamoto kikiwa kipo kwenye Mamlaka za Halmashauri za
Miji na Manispaa, Manispaa ya Moshi ilikuwa ina uwezo wa kuhudumia magari makubwa mawili na gari moja dogo ambalo tuliazima kutoka Japan. Tangu magari yale yachukuliwe na Kitengo cha Zimamoto Mkoa wa Kilimanjaro, leo tunahudumia gari moja tena tunahudumia kwa taabu na hicho kigari kimoja tulichokiomba Japan ndicho kinachofanywa kama ndiyo gari wanalotembelea Maafisa wa Zimamoto.
Je, Serikali imetumia kigezo gani kuonesha kwamba ufanisi umeongezeka baada ya kuhamisha kitengo hiki
kwenye Wizara ya Mambo ya Ndani tofauti na kilivyokuwa Halmashauri?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naomba kama Serikali haioni kwamba kuna haja sasa ya kusaidia Mkoa wa
Kilimanjaro kwa kuazima gari moja ya zimamoto kutoka KIA kwa sababu KIA wanaonekana wana magari ya ziada ili iweze kusaidiana na gari lililopo sasa hivi Mkoa wa Kilimanjaro ili kutoa huduma ya zimamoto kwa watu wa Mkoa wa Kilimanjaro? Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa jambo hili. Niseme tu kwamba vigezo vilivyotumika kwa sasa, moja tofauti na ilivyokuwa katika ngazi za Halmashauri, sasa hivi vipo dedicated kwa ajili ya masuala haya ya zimamoto na kutokuhudumia gari mbili ni kwa sababu tu gari yenyewe imeenda kwenye uchakavu. Ukipima kwa ujumla wake, ni kwamba ufanisi umeongezeka na utaona kwamba sasa kikosi kipo dedicated kwenye masuala ya zimamoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili la kuazima gari; gari za zimamoto zipo kwa ajili ya matukio na mara zote
katika maeneo yote panapotokea tukio la moto, gari zilizo karibu za kuzimia moto huwa zinaenda kutumika. Kwa hiyo, hilo hatuna tatizo nalo, lakini tunapanga kuimarisha hasa katika Miji ikiwemo hiyo ya Moshi kwa ajili ya ukubwa wa miji pamoja na uwepo wa uwanja wa ndege.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Mkoa wa Kilimanjaro una tatizo la uhaba wa magari ya zimamoto; gari linalofanya kazi mpaka sasa ni moja tu, hivyo kufanya huduma ya zimamoto kuwa duni sana. (a) Je, ni lini Serikali itaongeza magari mengine mawili ili kusaidia shughuli za zimamoto na kuepusha hasara zinazowakabili wananchi wanaopata majanga ya moto? (b) Je, Serikali haioni kwamba uamuzi wa kuhamishia Kitengo cha Zimamoto Wizara ya Mambo ya Ndani umeiongezea mzigo Wizara hiyo na kupunguza ufanisi wa shughuli za zimamoto?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuzingatia umuhimu wa magari ya zimamoto katika Mikoa yetu, lakini mikoa mingi mipya hususan Mkoa wa Songwe unakabiliwa na ukosefu wa magari ya zimamoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kupata kauli ya Serikali kwamba je, Serikali ina mpango gani wa kutuletea
magari ya zimamoto katika Mkoa mpya wa Songwe? Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa
ufuatiliaji wake na siyo tu jambo la zimamoto, bali masuala mazima yanayohusu idara zilizopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ikiwemo Makao Makuu ya Polisi katika Mkoa mpya wa Songwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu Songwe ni moja ya mikoa mipya, lakini una bahati ya kuwa karibu na uwanja
wa ndege. Tutaupa kipaumbele kama Mkoa mpya lakini pia kama mahitaji ya Mji ambao upo karibu na Mji wa Tunduma ambao unakua kwa kasi, ambao mara nyingi sana Mheshimiwa Juliana Shonza amekuwa akitetea masuala ya maendeleo ya mkoa huo na miji hiyo.

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Mkoa wa Kilimanjaro una tatizo la uhaba wa magari ya zimamoto; gari linalofanya kazi mpaka sasa ni moja tu, hivyo kufanya huduma ya zimamoto kuwa duni sana. (a) Je, ni lini Serikali itaongeza magari mengine mawili ili kusaidia shughuli za zimamoto na kuepusha hasara zinazowakabili wananchi wanaopata majanga ya moto? (b) Je, Serikali haioni kwamba uamuzi wa kuhamishia Kitengo cha Zimamoto Wizara ya Mambo ya Ndani umeiongezea mzigo Wizara hiyo na kupunguza ufanisi wa shughuli za zimamoto?

Supplementary Question 3

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi naomba niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mkoa wa Kilimanjaro matatizo yake yanafanana kabisa na Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Morogoro unakua
sana na viwanda vipo vingi na vingine vinaendelea kujengwa, lakini Kikosi cha Zimamoto katika Manispaa ya
Morogoro kinafanya kazi nzuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, kutokana na uchakavu wa magari katika Manispaa ya Morogoro, je,
Serikali iko tayari kushirikiana na Manispaa ya Morogoro kupata magari mapya katika Manispaa ya Morogoro?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli alichosema Mheshimiwa Murald na
nimpongeze sana kwamba maeneo ambayo yana viwanda gharama za bima huwa zinakuwa juu sana kama magari ya zimamoto ama huduma za zimamoto zisipokuwa karibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nature ya Mkoa wa Morogoro Serikali iko tayari kushirikiana na Mkoa na Mji wa
Morogoro kuweza kupata magari mapya. Kwenye taratibu hizi tunazoendelea nazo za upatikanaji wa magari mapya,
tutazingatia maombi na ushauri wa Mheshimiwa Mbunge.