Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 51 2017-04-12

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Mkoa wa Kilimanjaro una tatizo la uhaba wa magari ya zimamoto; gari linalofanya kazi mpaka sasa ni moja tu, hivyo kufanya huduma ya zimamoto kuwa duni sana.
(a) Je, ni lini Serikali itaongeza magari mengine mawili ili kusaidia shughuli za zimamoto na kuepusha hasara zinazowakabili wananchi wanaopata majanga ya moto?
(b) Je, Serikali haioni kwamba uamuzi wa kuhamishia Kitengo cha Zimamoto Wizara ya Mambo ya Ndani umeiongezea mzigo Wizara hiyo na kupunguza ufanisi wa shughuli za zimamoto?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Raphael Japhary Michael, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Mkoa wa Kilimanjaro una gari moja kubwa la kuzima moto ambalo lina uwezo wa kubeba maji lita 7,000 na dawa za kuzimia moto wa mafuta lita 400.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kwa sasa kuna magari mawili madogo ya kuzimia moto yasiyo na matanki ya kubeba maji na madawa. Pamoja na magari haya, hufanya kazi kwa kupata maji kutoka gari lingine au kutoka katika vituo maalum vya maji ya kuzimia moto (fire hydrant). Hata hivyo, kwa sasa ni gari moja tu linalofanya kazi na lingine linahitaji matengenezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango wa kununua magari ya zimamoto na uokoaji kwa ajili ya Mkoa wa Kilimanjaro pamoja na mikoa mingine. Katika kutekeleza mpango huo, Serikali inafanya mazungumzo na taasisi mbalimbali za nje ya nchi ambazo zimeonyesha nia ya
kutukopesha fedha kwa ajili ya ununuzi wa magari ya zimamoto pamoja na uokoaji na mazungumzo yatakapokamilika mkataba utasainiwa na kuanza utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhamishwa kwa Kitengo cha Zimamoto kutoka katika mamlaka mbalimbali na kuwekwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kulifanyika baada ya tathmini hususan ya utendaji kazi za kila siku, ambapo ilibainika kuwa utendaji kazi wa Vikosi vya Zimamoto
katika Halmashauri ulikuwa dhaifu kutokana na vikosi hivyo kuwa chini ya Wahandisi wa Majiji, Manispaa na Miji ambapo hawakuwa na utaalam wa masuala ya Zimamoto na Uokoaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ilibainika pia kuwa vikosi vikiwa chini ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege vihamishiwe Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ili kuleta ufanisi zaidi wa kazi na viwe chini ya kamandi moja ili viweze kupokea amri kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji. Napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba uamuzi huo uliongeza ufanisi na siyo mzigo.