Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Jimbo la Muheza lina kata 37 na vijiji 135, katika Awamu ya Kwanza na ya Pili ya Mradi wa REA ni vijiji vichache tu vilipata umeme. Je, utekelezaji wa REA III ni vijiji vingapi vinategemea kupata umeme ili wananchi wa maeneo haya waweze kujiandaa katika kujiendeleza kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ningependa kuuliza maswali mawili. Kwanza ningependa kuipongeza Wizara hiyo kwa sababu Waziri wake Profesa Muhongo alifika kwenye baadhi ya kata za Jimbo la Muheza ambalo liko jirani na power station ya Hale na akasikiliza kilio cha Wana-Muheza kwenye Kata hizo za Kwafungo, Songa, Bwembwera na Makole. Mheshimwa Mwenyekiti, sasa swali langu la kwanza ni hili, REA Awamu ya Pili na ya Kwanza iliweka mkandarasi, na mkandarasi yule alikuwa hatimizi wajibu wake kwa wakati, kwa sababu alikuwa ana kazi nyingi sana. Sasa Serikali itawahakikishiaje wanamuheza kwamba REA hii Awamu ya Tatu itakapoanza mkandarasi ambaye atateuliwa atadhibitiwa na atafanya kazi hizo kwa wakati? (Makofi) Swali langu la pili, ni kwamba REA Awamu ya Pili na ya Kwanza ilipitisha nguzo kwenye baadhi ya vijiji na vitongoji lakini vitongoji na vijiji vile havikupata umeme. Sasa kwenye hii Awamu ya Tatu vijiji ambavyo vilipitiwa na nguzo tu bila kupata umeme, vitongoji na vijiji vile Serikali inasemaje kuhakikisha kwamba vijiji hivyo na vitongoji hivyo na vyenyewe vinapata umeme badala ya kuona nguzo tu zimepita mbele yao?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Adadi Rajab anavyofatilia kwa kina sana kupatikana umeme katika katika Jimbo la Muheza. Nimpongeze sana tulipata orodha yako ya tarafa zako nne ikiwemo Tarafa ya Amani, Ngomeni, Bwembwera pamoja na Muheza yenyewe, kwa hiyo tunakupongeza sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati ya kumaliza kazi kwa haraka, katika utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu tumefanya maboresho katika usimamizi. Maboresho ya kwanza ni pamoja na kuweka msimamizi yaani supervisingengineer ambaye kazi yake ni kumsimamia mkandarasi ili amalize kazi haraka, hiyo ni kazi ya kwanza. Pili, tumeweka kila ofisi ya Wilaya kwa wasimamizi wa TANESCO, tumeteua Meneja Maalum atakayesimamia miradi ya REA yaani yeye akilala, akiamka anakumbuka REA, kwa hiyo tunaamini kwamba atamaliza kazi kwa haraka. Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ambalo ni muhimu sana kwa Waheshimiwa Wabunge ni kwamba tumeweka sasa kila mkandarasi akiingia site lazima kwanza amshirikishe Mheshimiwa Mbunge, kwa hiyo mtatusaidia sana kwenye usimamizi wa jambo hili. Kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi Rajab tuna hakika kwamba itakwenda kwa kasi. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na vitongoji, kwanza kama nilivyompongeza, tunajua vitongoji vyake 137 Mheshimiwa Mbunge Adadi Rajab vingi havijapata umeme, kama ambavyo nilikueleza, tunajua vitongoji vyetu tumeweka densification, mradi wa densification unaenda kwenye vitongoji vyote nchi nzima. Hivi sasa ninavyoongea katika Mkoa wa Tanga mkandarasi ameshaingia. Kwa hiyo, nikuhakikishie vitongoji vyako vyote ambavyo Mheshimiwa Mbunge unavifatilia sana ikiwemo Kitongoji cha Mambo leo, Mbwembeza, Msongambele, Mto wa Mbuzi, Kwambambere pamoja na kwa Mpota na Maramba vyote vitapata umeme.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Jimbo la Muheza lina kata 37 na vijiji 135, katika Awamu ya Kwanza na ya Pili ya Mradi wa REA ni vijiji vichache tu vilipata umeme. Je, utekelezaji wa REA III ni vijiji vingapi vinategemea kupata umeme ili wananchi wa maeneo haya waweze kujiandaa katika kujiendeleza kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii adhimu ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Manyoni Magharibi kuna vijiji vya Mbugani, Agondi, Mabondeni, Kitopeni, Ipande, Muhanga, Damwelu, Kitalaka, Kaskazi Stesheni, Kintanura, Lungwa na Kalangali havina umeme. Je, Serikali inaweza kutoa tamko kwamba REA Awamu ya Tatu wananchi wa vijiji hivi watafikiwa na umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa, nakupongeza sana juzi uliniletea orodha ya vijiji vyako vyote, kwa hiyo vijiji vyako vyote Mheshimiwa Mbunge ulivyotaja katika Awamu ya Tatu vyote vitapitiwa na umeme, na nikuhakikishie kwamba kufikia mwezi Machi kama ambavyo tumeeleza, vijiji vyote kwa nchi nzima wakandarasi watakuwa site ikiwa ni pamoja na Jimbo lako la Manyoni Magharibi.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Jimbo la Muheza lina kata 37 na vijiji 135, katika Awamu ya Kwanza na ya Pili ya Mradi wa REA ni vijiji vichache tu vilipata umeme. Je, utekelezaji wa REA III ni vijiji vingapi vinategemea kupata umeme ili wananchi wa maeneo haya waweze kujiandaa katika kujiendeleza kiuchumi?

Supplementary Question 3

MHE. MAFTAH A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru niweze kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kabisa kwamba Serikali iliweka mkakati wa kuhakikisha ya kwamba maeneo yote ambayo limepita bomba la gesi kitaalam wanaita mkuza wa gesi, kwamba vijiji vile na mitaa ile itakuwa imepatiwa umeme kupitia REA Awamu ya Kwanza, Pili na ya Tatu. Lakini mpaka sasa hivi ninavyozungumza maeneo mengi ya vijiji na vitongoji vya Mtwara Mjini na Lindi kwa mfano Dimbozi, Mbawala Chini, Mkunjanguo na Naulongo kule kote bado hakujapelekewa umeme. Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ukoje kuhakikisha kwamba wanamaliza tatizo hili katika ule mkuza wa gesi kwamba wapate umeme wale wananchi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Maftaha kwamba tunapotekeleza Mradi wa REA Awamu ya Tatu, awali ya yote tunaanzia kwenye vijiji ambavyo viko kwenye mkuza wa bomba la gesi. Kwa hiyo, nikuhakishie Mheshimiwa Maftaha na niombe tu kwamba tutakapomaliza Bunge kama una fursa basi tutapanga siku tupitie kijiji hadi kijiji ili kuhakikisha wananchi wako wanapata umeme.