Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 111 2017-02-10

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Jimbo la Muheza lina kata 37 na vijiji 135, katika Awamu ya Kwanza na ya Pili ya Mradi wa REA ni vijiji vichache tu vilipata umeme. Je, utekelezaji wa REA III ni vijiji vingapi vinategemea kupata umeme ili wananchi wa maeneo haya waweze kujiandaa katika kujiendeleza kiuchumi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajab, Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya vijiji 37 ambavyo havijapatiwa umeme katika Jimbo la Muheza na vitongoji 137 vinatarajiwa kupatiwa umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu utakaoanza mwezi Machi mwaka huu. Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa Mpango wa Usambazaji Umeme Vijijini kwa nchi nzima unategemewa kufanya katika vipengele vitatu unaojumuisha densification, grid extension, pamoja na off-grid renewable. REA Awamu ya Tatu kwa ujumla wake katika nchi nzima ikiwa ni pamoja na Jimbo la Muheza itaanza mwezi Machi 2017. Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa mradi huu katika Jimbo la Muheza utajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovolti 33 yenye urefu wa kilometa 50; ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovolti 0.4 yenye urefu wa kilometa 82; ufungaji wa transfoma 41; pamoja na kuwanganishia umeme wateja 1025. Mradi huu utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 3.94.