Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y MHE. RHODA E. KUNCHELA) aliuliza:- Tatizo la umeme katika Mkoa wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda Mjini limekuwa kero kwa wananchi; tatizo hili linafanya maendeleo kuwa duni katika Manispaa ya Mpanda:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuachana na matumizi ya jenereta ambalo ni bovu linalosababisha ukosefu wa umeme kila mara? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua kero hii ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikiliza Waziri kwa majibu yake, amesema mwaka 2018 ndio mradi huo utakamilika, ni nini commitment ya Serikali kwa kuwa hadi kufikia mwaka 2018 na wananchi wanaihitaji nishati hii muhimu kwa ajili ya maendeleo. Je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kuangalia njia mbadala kuweza kusaidia wananchi hawa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa tatizo la nishati ya umeme katika Mkoa wa Katavi linafanana kabisa na matatizo ya umeme katika Mkoa wa Morogoro hasa katika Manispaa ya Morogoro katika Kata za Mindu, Kihonda na Mkundi ambapo wananchi hawa kwa muda mrefu hawana nishati ya umeme ingawa wanapitiwa na Gridi ya Taifa. Je, Serikali haioni kama kuna haja ya kuhakikisha wananchi hawa wanapata umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, commitment ya Serikali kwa Mkoa wa Katavi pamoja na Sumbawanga kwa kweli ni kubwa sana. Hadi sasa mbali na mradi huu wa kupeleka umeme wa kilovolti 400 hivi sasa Serikali imeanza kukarabati majenereta mawili yaliyokuwa na matatizo pale Mpanda. Yale majenereta yalikuwa na uwezo wa megawati 2.6 lakini yalikuwa yanatoa umeme wa megawati 2.3, ukarabati wa majenereta hayo umekamilika tarehe 5 mwezi huu kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa Mpanda pamoja na maeneo ya jirani umeme utapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hatua ya pili sasa hivi ujenzi umeanza kufunga jenereta mbili mpya ambazo pia zinatengenezwa, kama nilivyosema kwenye swali la msingi, kupitia mradi wa ORIO. Jenereta hizi zina uwezo wa kufua megawati 2.5 kwa ujumla wake kwa hiyo, Mji wa Mpanda pamoja na Sumbawanga sasa watakuwa na jumla ya megawati 5.1 ambapo matumizi yao kwa sasa hivi ni megawati 2.6. Kwa hiyo, vijiji vyote sasa vya Mchangani, Dilifu, Longililo, Mpakani, Gereza la Kakalankurukuru, pamoja na Kalamsenga vyote vitapata umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na vijiji vya Morogoro vikiwemo Mindu pamoja na Kihonda, vijiji hivi vinapelekewa umeme kupitia mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu unaoanza tarehe 15 Disemba, 2016. Na vijiji vyote vya Kihonda na maeneo ya jirani ikiwemo pamoja na Mindu vitapelekewa umeme wa uhakika mwaka huu.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y MHE. RHODA E. KUNCHELA) aliuliza:- Tatizo la umeme katika Mkoa wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda Mjini limekuwa kero kwa wananchi; tatizo hili linafanya maendeleo kuwa duni katika Manispaa ya Mpanda:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuachana na matumizi ya jenereta ambalo ni bovu linalosababisha ukosefu wa umeme kila mara? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua kero hii ya umeme?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa REA inafanya kazi nzuri sana na imesambaza umeme karibu nchi nzima na Mpwapwa kuna vijiji ambavyo havijapata umeme, kijiji cha Kibojani, Mgoma, Mzogole, Viberewele, Sazima, Mkanana, Igoji Kaskazini na Igoji Kusini pamoja na Iwondo.
Je, Mheshimiwa Waziri, utakuwa tayari kupeleka umeme katika vijiji hivi kwa sababu umeme ndio uchumi wetu na ndio maendeleo yetu katika nchi yetu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa tuko tayari kupeleka umeme kwenye vijiji vyote vya Mheshimiwa Lubeleje. Mheshimiwa Lubeleje ni Mbunge mkongwe, nadhani kati ya Wabunge wote ambao tuko hapa Mheshimiwa Lubeleje ni wa zamani sana kwa hiyo, hatuwezi kumuangusha. Kwa hiyo, Mheshimiwa Lubeleje nikuhakikishie vijiji vyako vyote vya Lugoma na Kiwelewele vitapelekewa umeme kupitia REA Awamu ya Tatu.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y MHE. RHODA E. KUNCHELA) aliuliza:- Tatizo la umeme katika Mkoa wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda Mjini limekuwa kero kwa wananchi; tatizo hili linafanya maendeleo kuwa duni katika Manispaa ya Mpanda:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuachana na matumizi ya jenereta ambalo ni bovu linalosababisha ukosefu wa umeme kila mara? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua kero hii ya umeme?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nilikuwa naomba kumuuliza Naibu Waziri kwa kuwa REA wamejitahidi sana kusambaza umeme vijijini, lakini TANESCO hawaingilii kwenda kuanza kusambaza umeme kwenye maeneo mengine ambayo yameanzishwa hasa ya uzalishaji, mfano Kata ya Gumanga kuna kiwanda cha kusindika nyanya, umeme haujapelekwa Mkalama. Nilikuwa naomba kuuliza ni kwa nini TANESCO sasa wasiende kuanza kusambaza umeme? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji alivyotaja Mheshimiwa Mlata kwanza kabisa viko kwenye Mpango wa REA, lakini sambamba na Mpango wa REA bado TANESCO wanapeleka nguzo. Nimhakikishie tarehe 15 mwezi uliopita Mheshimiwa Mlata tulimpelekea nguzo 20 za umeme ambazo zitafungwa kuanzia tarehe 20 mwezi unaokuja. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mlata vijiji vyako vyote vya Manga pamoja na ulivyotaja Mkarama vitafungiwa umeme kupitia REA pamoja na TANESCO.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y MHE. RHODA E. KUNCHELA) aliuliza:- Tatizo la umeme katika Mkoa wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda Mjini limekuwa kero kwa wananchi; tatizo hili linafanya maendeleo kuwa duni katika Manispaa ya Mpanda:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuachana na matumizi ya jenereta ambalo ni bovu linalosababisha ukosefu wa umeme kila mara? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua kero hii ya umeme?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa kunipa nafasi hii. Namuuliza swali Naibu Waziri, alipokuja Mpanda alituhakikishia wananchi wanaoishi vijiji vya Kabungu, Mchakamchaka, Ifukutwa na Majalila ambako ni Makao Makuu ya Wilaya kwamba ataleta umeme ifikapo mwezi wa tisa. Je, ni lini Serikali itathibitisha kauli yake ambayo aliitoa yeye mwenyewe alipofika huko?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nilitembelea maeneo mengi sana katika Jimbo la Mheshimiwa Kakoso na hasa kabla ya kutaja maeneo ya Majalila, Mheshimiwa Kakoso kwanza nikuhakikishie Gereza lako la Kakalankurukuru ambalo lina miaka 37 halina umeme litapatiwa umeme mwezi ujao kupitia Mradi wa REA unaoanza mwezi ujao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitembelea pia Kata ya Majalila ambako kuna mitambo na miradi ya maji. Nikuhakikishie Mheshimiwa Kakoso, mradi wa REA utakapoanza kufikia mwezi Januari hadi Februari mwaka unaokuja mradi wako wa Majalila utafungiwa jenereta za umeme, lakini pia jenereta ya umeme itaunganishwa na umeme ambao sasa unapitia mradi wa REA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kijiji cha Kabungu nilikitembelea pamoja na Mpanda Mji Mpya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Kakoso nikuhakikishie, vijiji vyako vyote 32 vilivyobaki vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA kuanzia Disemba na Januari mwaka unaokuja.