Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 56 2016-11-07

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y MHE. RHODA E. KUNCHELA) aliuliza:-
Tatizo la umeme katika Mkoa wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda Mjini limekuwa kero kwa wananchi; tatizo hili linafanya maendeleo kuwa duni katika Manispaa ya Mpanda:-
(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuachana na matumizi ya jenereta ambalo ni bovu linalosababisha ukosefu wa umeme kila mara?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua kero hii ya umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rhoda Edward Kunchela, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutekeleza ujenzi wa Mradi wa Umeme wa Gridi ya Taifa inayounganisha Mikoa ya Rukwa, Katavi pamoja na Kigoma. Ujenzi wa mradi huo utasaidia mikoa hiyo kuondokana na matumizi ya mitambo ya mafuta pia na gharama kubwa. Kwa maana hiyo ujenzi huo unahusisha njia ya umeme msongo wa kilovolti 400; ambao pia ambao pia wameanza kuunganisha katika mikoa Mbeya - Sumbawanga - Mpanda - Kigoma hadi Nyakanzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kuhuisha upembuzi yakinifu wa mradi kutoka kilovoti 220 za awali na kuwa kilovolti 400 zinazoendelea hivi sasa inaendelea. Awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi (Mbeya - Sumbawanga) itakamilika mwaka, 2018 na awamu zote tatu za mradi zinatarajiwa kukamilika mwaka 2022; gharama za mradi huu zinakadiriwa kuwa dola za Marekani milioni 664.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu utakapokamilika utaupatia umeme wa uhakika Mji wa Mpanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa ujenzi wa umeme wa Gridi ya Taifa unaendelea, Serikali kupitia TANESCO imeanza ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia jenereta mbili zenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 1.25; kila moja katika Mji wa Mpanda kupitia mradi wa ORIO. Mradi huu unafadhiliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Uholanzi kwa gharama ya shilingi bilioni 12.21. Kazi za ujenzi wa kituo hicho zimeanza mwezi Oktoba, 2016 na zitakamilika mwezi Julai, 2017.