Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Wanawake katika Mkoa wa Simiyu wamehamasika sana kujiunga kwenye vikundi ili kukusanya nguvu za kiuchumi kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi zaidi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wanawake hawa mafunzo ya kimtaji ili waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi zaidi?

Supplementary Question 1

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Na mimi nina swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wanawake wa Simiyu wamehamasika vizuri sana na wanafanana kabisa na wanawake wa Mvomero na wanawake wa Sumve.
Je, Waziri atatueleza ni lini sasa katika suala zima la maendeleo zile shilingi milioni 50 zitakwenda Sumve na Mvomero kwa sababu wanawake wale wameshajiunga kwenye vikundi na vikundi vile vimeshasajiliwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimwambie wanawake wa Mvomero na wale Wasukuma wa kule hawawezi kufanana, hilo ni jambo la kwanza. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, naomba nimtoe shaka, najua Mheshimiwa Murad ni mpiganaji mkubwa sana, Serikali itahakikisha watu wa Mvomero, Bariadi, Sikonge na wa maeneo yote fedha zile zinapatikana na zinawafikia wananchi ili mradi wahakikishe wanajihusisha katika shughuli za ujasiriamali. Suala hili Serikali imelisikia ndiyo maana imeweka katika bajeti yake ya mwaka huu wa fedha.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Wanawake katika Mkoa wa Simiyu wamehamasika sana kujiunga kwenye vikundi ili kukusanya nguvu za kiuchumi kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi zaidi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wanawake hawa mafunzo ya kimtaji ili waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi zaidi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Ni ukweli usiopingika kwamba wanawake katika nchi hii ndiyo wanaolisha Taifa hili kwa sababu akina mama wengi wanajishughulisha na kilimo na biashara ndogo ndogo. Ni kweli pia kwamba katika baadhi ya Halmashauri akina mama wengi wananyanyasika sana na biashara zao kwa kutozwa kodi mbalimbali ambazo hazina tija.
Je, ni lini Serikali itatoa tamko kwa Halmashauri zote ikiwepo Halmashauri yangu ya Rombo waache kuwatoza akina mama zile kodi ambazo zinawaletea bugudha na hivyo kushindwa kuendesha biashara zao kwa ufanisi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika kufanya hili nadhani tunafanya rejea, hata Mheshimiwa Rais alipokuwa akizunguka sehemu mbalimbali alikuwa akisema kwamba akina mama hawa wasinyanyaswe.
Naomba niseme wazi kwamba kutokana na agizo hilo la Mheshimiwa Rais, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunaandaa marekebisho ya Sheria ya Serikali za Mitaa inayohusiana na mambo ya Kodi, Sura Namba 290 na hivi sasa ipo katika mchakato wa mwisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo ni kuondoa zile kero mbalimbali siyo za akina mama peke yake bali ni pamoja na walemavu na makundi mbalimbali. Katika mchakato huu tutakwenda kuhakikisha tunaondoa kero hii siyo kwa akina mama na vijana tu, lakini na group la walemavu lazima wawezeshwe na Halmashauri.
Hata hivyo, watakapowezeshwa kitafanyika nini ili mitaji yao iende vizuri, ndiyo hiyo sheria inakuja sasa hivi. Imani yangu ni kwamba Wabunge wote kwa pamoja sheria ile itakapokuja hapa tutashirikiana kuipitisha kwa sababu jambo hili lina maslahi mapana sana kwa wananchi wetu lakini kikubwa zaidi lina maslahi katika uchumi wa nchi yetu.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Wanawake katika Mkoa wa Simiyu wamehamasika sana kujiunga kwenye vikundi ili kukusanya nguvu za kiuchumi kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi zaidi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wanawake hawa mafunzo ya kimtaji ili waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi zaidi?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa wanawake wa Mkoa wa Simiyu ni wajasiriamali wazuri sana. Je, ni lini Serikali itaanzisha Benki ya Maendeleo ya Wanawake ili wanawake wa Mkoa wa Simiyu waweze kujikomboa na kujinufaisha na benki hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa ahadi ya Mheshimiwa Rais ni kupeleka kila kijiji na kila mtaa shilingi milioni 50 ili kuwawezesha wanawake na vijana. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweza kusimamia pesa hizo na kuhakikisha kwamba zimewafikia walengwa, zisije zikaishia mikononi mwa watu wachache, wajanja kama mapesa ya JK? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kumbukumbu ya Wabunge yote wakati Waziri wa Afya ambaye anahusika na mambo ya maendeleo ya jamii ambapo Benki hii ya Wanawake iko katika dhamana yake, nakumbuka katika bajeti ya mwaka huu alizungumza wazi kwamba suala la ufunguaji wa matawi ya benki hii utafanyika kwa kadri rasilimali fedha inavyopatikana. Imani yangu ni kwamba kauli ile ya Mheshimiwa Waziri itaendelea kusimamiwa na katika Ukanda ule wa Ziwa benki hii itafunguliwa lengo kubwa likiwa ni kufikisha huduma kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la shilingi milioni 50, ni kweli, sisi tunafahamu kwamba katika mchakato wa bajeti ya mwaka huu zile fedha zilitengwa na naamini Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inahusika na kusimamia jambo hili inapanga utaratibu mzuri na ndiyo maana wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu anapita maeneo mbalimbali alikuwa akitoa maelekezo kwamba watu waache kuunda vikundi vya kitapeli ambapo mwisho wa siku fedha zile zitakuja kupotea. Imani yetu ni kwamba katika kipindi tutashirikiana vizuri wananchi wote na Serikali ili tusifanye makosa yale yaliyojitokeza katika kipindi cha nyuma katika fedha zile za mamilioni ya JK, sasa tunasema hatutarudia tena utaratibu ule wa mwanzo.