Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Mradi wa REA unaendelea kutekelezwa katika vijiji 24 katika Jimbo la Sikonge lakini mradi huo ulisimamia kwa muda mrefu ambapo baadhi ya maeneo nguzo zilizoachwa barabarani zimeanza kufukiwa na mchanga kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha:- (a) Je, Serikali itakamilisha lini mradi huo kwa Awamu ya Kwanza na Pili? (b) Je, Awamu ya Tatu ya utekelezaji wa mradi huo itahusisha vijiji gani katika Wilaya ya Sikonge na ni lini utaanza na kukamilika? (c) Je, Serikali haioni umuhimu wa kufikisha umeme wa REA kwenye mitambo ya kusukuma maji ya Ityatya, Uluwa, Makazi, Igumila, Majojolo na Kiyombo ili kupunguza gharama za dizeli ambazo zimekuwa zikiathiri upatikanaji wa maji kutokana na gharama kubwa za uendeshaji mitambo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza, wananchi wamekuwa wanalalamika sana kwamba vijiji ambavyo vimeshapatiwa umeme hadi sasa wanaopewa kipaumbele cha kuunganishiwa umeme ni wale tu wanaokaa kandokando ya barabara kuu. Je, ni lini wananchi wote ambao vijiji vyao vimeunganishiwa umeme watapatiwa umeme wanaohitaji?
Swali la pili, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri aliahirisha mwezi uliopita safari yake ya kuja Sikonge kujionea matatizo. Je, ni lini sasa atapanga ziara yake kuwatembelea wananchi wa Sikonge?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa REA Awamu ya II inayoendelea ambayo itakamilika mwezi huu, mpango wake mahsusi ulikuwa ni kupeleka umeme kwenye vituo vya vijiji na siyo kusambaza kwenye vitongoji. Sambamba na hilo, kabla hatujaanza Mradi wa REA Awamu ya III, kuna mradi mwingine unaosambaza umeme kutoka kwenye vituo na center mbalimbali na kuwapelekea wananchi kwenye vitongoji vyao.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi huu nimekuwa nikiusema, unaitwa Underline Distribution Transformer ambao unaanza Julai, 2016 na utakamilika ndani ya miezi 18. Mradi huu utasambaza umeme kwenye vitongoji vyote ambapo umeme wa msongo wa kilovoti 33 umepita.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili la Mheshimiwa Mbunge ni kweli tumekuwa tukiahidi kwamba tutapeleka umeme kwenye vitongoji. Nilimwomba Mheshimiwa Kakunda aniletee vitongoji vyake vyote, ameshaleta na namshukuru sana. Kwa hiyo, napenda kumwambia Mheshimiwa Kakunda vitongoji vyake ambavyo umeme umepita vitapatiwa umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ni lini tutatembelea, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge, kwa ridhaa yako nadhani tukishamaliza Bunge hili, niongozane na Mheshimiwa Kakunda na niwahakikishie Wabunge wa karibu na Sikonge nitawatembelea wote mara baada ya Bunge hili la bajeti.

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Mradi wa REA unaendelea kutekelezwa katika vijiji 24 katika Jimbo la Sikonge lakini mradi huo ulisimamia kwa muda mrefu ambapo baadhi ya maeneo nguzo zilizoachwa barabarani zimeanza kufukiwa na mchanga kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha:- (a) Je, Serikali itakamilisha lini mradi huo kwa Awamu ya Kwanza na Pili? (b) Je, Awamu ya Tatu ya utekelezaji wa mradi huo itahusisha vijiji gani katika Wilaya ya Sikonge na ni lini utaanza na kukamilika? (c) Je, Serikali haioni umuhimu wa kufikisha umeme wa REA kwenye mitambo ya kusukuma maji ya Ityatya, Uluwa, Makazi, Igumila, Majojolo na Kiyombo ili kupunguza gharama za dizeli ambazo zimekuwa zikiathiri upatikanaji wa maji kutokana na gharama kubwa za uendeshaji mitambo?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa vile Mradi huu wa REA katika Jimbo la Ulyankulu umekuwa ukisuasua na wakati mwingine unatia hofu kwa wananchi kwa sababu maeneo muhimu ya taasisi, zahanati na vituo vya afya mfano, kama Barabara ya Kumi pamoja na Shule ya Sekondari Mkindo na maeneo mengi tu yamekuwa yakirukwa. Serikali ituambie ni lini mradi huu utakamilika na umeme kuwashwa katika Jimbo la Ulyankulu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli umeme umekuwa ukirukaruka kama ambavyo wananchi wanasema na kama Mheshimiwa Mbunge anavyosema. Hata hivyo, kama nilivyokwishaeleza, maeneo yote ambayo yamekuwa yakirukwarukwa, siyo kwamba yalirukwa, kulikuwa na mpango madhubuti kwamba umeme mwingine utakuja chini kupita kwenye vitongoji vyote. Kwa hiyo, vitongoji vyote vya Mheshimiwa wa Ulyankulu vitapitiwa na umeme katika Awamu hii ya II.
Mheshimiwa Naibu Spika, Awamu ya II inakamilika mwezi Juni, 2016 kama ambavyo nimekuwa nikieleza na Awamu ya III inaanza mwezi Julai, 2016 na itakamilika baada ya miaka mitatu hadi minne. Kwa hiyo, vijiji vyote vya Ulyankulu vya Mheshimiwa Mbunge, ikiwa ni pamoja na eneo la Barabara ya Kumi, vituo vya afya, zahanati pamoja na shule zitapatiwa umeme chini ya mradi wa Underline Transformer na chini ya Mradi wa REA Awamu ya III unaoanza mwezi Julai, 2016.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Mradi wa REA unaendelea kutekelezwa katika vijiji 24 katika Jimbo la Sikonge lakini mradi huo ulisimamia kwa muda mrefu ambapo baadhi ya maeneo nguzo zilizoachwa barabarani zimeanza kufukiwa na mchanga kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha:- (a) Je, Serikali itakamilisha lini mradi huo kwa Awamu ya Kwanza na Pili? (b) Je, Awamu ya Tatu ya utekelezaji wa mradi huo itahusisha vijiji gani katika Wilaya ya Sikonge na ni lini utaanza na kukamilika? (c) Je, Serikali haioni umuhimu wa kufikisha umeme wa REA kwenye mitambo ya kusukuma maji ya Ityatya, Uluwa, Makazi, Igumila, Majojolo na Kiyombo ili kupunguza gharama za dizeli ambazo zimekuwa zikiathiri upatikanaji wa maji kutokana na gharama kubwa za uendeshaji mitambo?

Supplementary Question 3

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililojitokeza katika Wilaya ya Sikonge kama alivyoeleza Mheshimiwa Kakunda ndivyo ilivyo katika Wilaya ya Urambo. Namshukuru Naibu Waziri alifika Urambo ila wananchi wa Urambo wanasikitika alifika lakini vijiji vingi hawajapata umeme. Je, ni kwa sababu ramani ilikosewa na yuko tayari kumtuma mhusika aende kuangalia tena kwa kuwa wananchi wengi hawakunufaika na umeme huo unaokamilika wa awamu ya pili? Hata hivyo, bado wanamkumbuka na wanaomba arudi tena, je, atarudi tena awaone?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile maswali ni mawili, nachagua swali la kwenda pamoja na Mheshimiwa Mbunge. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuhusu suala la kwenda wala sitatuma mtu, nitakwenda mwenyewe na nitakwenda na Mheshimiwa Mbunge.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Mradi wa REA unaendelea kutekelezwa katika vijiji 24 katika Jimbo la Sikonge lakini mradi huo ulisimamia kwa muda mrefu ambapo baadhi ya maeneo nguzo zilizoachwa barabarani zimeanza kufukiwa na mchanga kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha:- (a) Je, Serikali itakamilisha lini mradi huo kwa Awamu ya Kwanza na Pili? (b) Je, Awamu ya Tatu ya utekelezaji wa mradi huo itahusisha vijiji gani katika Wilaya ya Sikonge na ni lini utaanza na kukamilika? (c) Je, Serikali haioni umuhimu wa kufikisha umeme wa REA kwenye mitambo ya kusukuma maji ya Ityatya, Uluwa, Makazi, Igumila, Majojolo na Kiyombo ili kupunguza gharama za dizeli ambazo zimekuwa zikiathiri upatikanaji wa maji kutokana na gharama kubwa za uendeshaji mitambo?

Supplementary Question 4

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali la nyongeza. REA Awamu ya II imebakiza siku 27, je, wameshafanya tathmini ya kutosha nchi nzima? Kama jibu ni ndiyo utekelezaji wake ni asilimia ngapi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nachagua swali la tathmini ya ujumla. Nimhakikishie Mheshimiwa Ndassa na nimshukuru tumeshirikiana, mpaka sasa tathmini tuliyofanya ukamilifu wa kazi ya REA Awamu ya II ni asilimia 91 ya kazi zote zilizokwishakamilika.