Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 298 2016-06-03

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:-
Mradi wa REA unaendelea kutekelezwa katika vijiji 24 katika Jimbo la Sikonge lakini mradi huo ulisimamia kwa muda mrefu ambapo baadhi ya maeneo nguzo zilizoachwa barabarani zimeanza kufukiwa na mchanga kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha:-
(a) Je, Serikali itakamilisha lini mradi huo kwa Awamu ya Kwanza na Pili?
(b) Je, Awamu ya Tatu ya utekelezaji wa mradi huo itahusisha vijiji gani katika Wilaya ya Sikonge na ni lini utaanza na kukamilika?
(c) Je, Serikali haioni umuhimu wa kufikisha umeme wa REA kwenye mitambo ya kusukuma maji ya Ityatya, Uluwa, Makazi, Igumila, Majojolo na Kiyombo ili kupunguza gharama za dizeli ambazo zimekuwa zikiathiri upatikanaji wa maji kutokana na gharama kubwa za uendeshaji mitambo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Sikonge ilijumuishwa kwenye REA Awamu ya II ambayo inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2016. Kazi ya kupeleka umeme Wilaya ya Sikonge inajumuisha pia ujenzi wa umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 166.44 lakini pia ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 58.06. Kazi hii pia itajumuisha ufungaji wa transfoma 28 za ukubwa mbalimbali pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 1,704.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huo ambao unatekelezwa kupitia mkandarasi CHICCO umekamilika kwa asilimia 88 hadi sasa. Ujenzi wa njia ya msongo wa kilovoti 33 umekamilika kwa asilimia 86 na ujenzi wa msongo wa kilovoti 0.4 umekamilika kwa asilimia 89.3, lakini pia transfoma 15 zimeshafungwa na wateja 228 wameunganishiwa umeme. Kazi hii imegharimu shilingi bilioni 6.42.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini REA, Awamu ya III, unatarajiwa kuanza mwezi Julai, 2016. Mradi wa REA Awamu ya III unakusudia kupeleka umeme katika vijiji vyote vilivyobaki vya Mheshimiwa Mbunge pamoja na shule, zahanati na vituo vya afya. Kadhalika, kazi hii itajumuisha kupeleka umeme kwa wananchi wapatao 1,510. Kazi hii inagharimu pia jumla ya shilingi milioni 4.33.
(c) Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme kwenye pampu za kusukuma maji alizozitaja Mheshimiwa Mbunge za Ityatya, Makazi na Uluwa itafanywa na REA Awamu ya III. Kazi ya kupeleka umeme kwa vijiji na pampu hizi itahusisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa tisa, lakini pia ufungaji wa transfoma tatu pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 141. Kazi hii itagharimu shilingi milioni 317.14. Aidha, pampu za maji za Igumumila, Kiyombo na Magolo zitafanyiwa tathmini kubaini mahitaji yake ili na zenyewe ziweze kupatiwa umeme haraka iwezekanavyo.