Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Mbuga ya Akiba ya Uwanda katika Wilaya ya Sumbawanga Vijijini ilitengwa miaka ya nyuma wakati idadi ya watu ikiwa ndogo sana ikilinganishwa na sasa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipunguza pori hilo ili kunusuru shida inayowapata wananchi wanaozunguka eneo hilo ya kukosa maeneo ya kilimo na ufugaji? (b) Je, kwa nini wananchi wa maeneo hayo wanapigwa na Askari wa Wanyamapori na kunyang’anywa mali zao, wakati hakuna alama yoyote inayoonyesha mpaka katika mbuga hiyo? (c) Je, wananchi wa vijiji vinavyozunguka pori hilo wamenufaika na nini zaidi ya vipigo wanavyovipata?

Supplementary Question 1

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tangu kuanzishwa kwa pori hilo mwaka 1959 hadi sasa ni miaka 57; je, Serikali inaweza kusema kwa kipindi hicho, imepata faida gani zaidi ya Askari Wanyamapori kukodishia wafugaji na wakulima wasio na uwezo kuruhusiwa kulima halafu baadae wanagawana mazao?
Swali la pili, kwa majibu yaliyotolewa ninapata imani kuwa, Mheshimiwa Waziri anadanganywa na wataalam wa chini yake. Je, yuko tayari kuongozana na mimi kwenda kwenye Mbuga hiyo, ili akajionee changamoto zilizopo na baadae asiweze kudanganywa na watumishi wake?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza pori lina faida gani na zaidi ya miaka 50 iliyopita anataka kujua kuna faida gani imepatikana kutokana na uhifadhi huo?
Kwanza niseme tu kwamba faida za uhifadhi ziko zile ambazo unaweza ukazitazama kwa macho au ukazikamata mkononi ambazo ni za kifedha na pengine ni za kiuchumi moja kwa moja. Lakini uhifadhi hasa wa mapori wakati mwingine faida zake unaweza usizione kwa macho au ukakamata kwa mikono kwa sababu faida zake ni za kiikolojia zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, faida zake zinakwenda kuambukiza hata uwekezaji, hata shughuli zingine za kiuchumi, lakini pia hata uwepo wa dunia tunayoishi na nchi tunayoishi yakiwemo masuala ya hali ya hewa, upatikanaji wa maji, na mambo mengine ya namna kama hiyo. Kwa hiyo, faida zipo na ni nyingi, lakini kama alikuwa anakusudia za kiuchumi zinazohusiana na fedha, hilo ni suala la takwimu na kwa hiyo basi anaweza kutafuta fursa tukaonana na kwa kutumia wataalam ambao na wenyewe nitawasemea kwenye swali la pili basi tunaweza tukapata takwimu, kujibu vizuri zaidi kuhusiana na suala la faida za kifedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili la kuongozana, kwanza niweke sawa juu ya suala hili ambalo linajirudia mara nyingi sana la kwamba kuna kupata taarifa ambazo ni za uongo au za kudanganywa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna jambo niko makini nalo ni hilo na naomba Waheshimiwa Wabunge mnisaidie ili kwa upande wangu lakini nafikiri kwa Serikali nzima; ikiwa kuna majibu ambayo yanakuwa yanatia mashaka na pengine ni ya uongo; kwa sababu majibu ya uongo ni kama vile yamedhamiliwa. Kama kunajitokeza mazingira kama hayo, basi tuanze sasa kukataa namna hiyo ya kufanya kazi, kwa sababu hiyo ni namna ambayo haifai.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa upande wangu anayetoa jibu ninamfahamu, na anapotoa jibu namuambia anaweka saini kabisa kwenye jibu hilo analonipatia. Sasa baada ya hili kwa sababu tayari umeishanipa hiyo indication baada ya hapa, mimi na yeye tutakwenda kutafuta jibu sahihi ni lipi kulinganisha na hili ili yule aliyelitoa sasa kama kweli amedanganya, kwa sababu kudanganya ni dhamira, basi atachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni na taratibu, lakini kwa kawaida kila mmoja kila mtumishi wa Serikali, anao wajibu wa kutenda kazi zake sawa sawa na anao wajibu kwenye masuala ya kujibu maswali, anao wajibu wa kujibu maswali kwa niaba ya Serikali na kwa hiyo, anawajibika kutoa majibu ambayo ni sahihi.

Name

Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Mbuga ya Akiba ya Uwanda katika Wilaya ya Sumbawanga Vijijini ilitengwa miaka ya nyuma wakati idadi ya watu ikiwa ndogo sana ikilinganishwa na sasa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipunguza pori hilo ili kunusuru shida inayowapata wananchi wanaozunguka eneo hilo ya kukosa maeneo ya kilimo na ufugaji? (b) Je, kwa nini wananchi wa maeneo hayo wanapigwa na Askari wa Wanyamapori na kunyang’anywa mali zao, wakati hakuna alama yoyote inayoonyesha mpaka katika mbuga hiyo? (c) Je, wananchi wa vijiji vinavyozunguka pori hilo wamenufaika na nini zaidi ya vipigo wanavyovipata?

Supplementary Question 2

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nilikuwa naomba niulize Serikali na niulize Wizara ya Maliasili na Utalii, je, ni lini sasa italipa fidia au italipa kifuta jasho na kifuta machozi kwa wananchi katika hifadhi zote ambazo zinapakana na wanyamapori, leo ni mwaka wa tano fedha ambazo wananchi wamelipwa ukizingatia vijiji 16 Wilaya ya Babati Vijijini bado hawajalipwa wamelipwa shilingi milioni 12 tu kati ya shilingi milioni 100 na, na nikifuta jasho na wala siyo fidia.
Je, ni lini na ni lini sasa Serikali itakuja tulipendekeza hapa kwamba hifadhi husika ndiyo ziwe zinalipa hizo fidia badala ya Wizara ya Maliasili na Utalii ili iwe rahisi sasa hifadhi ambazo ziko jirani na hivyo vijiji waweze kulipa mara moja ili wananchi hao sasa wapate unafuu?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru na naomba nijibu swali la nyongeza moja au mawili pengine inaweza kuwa moja kwa mawili kadri alivyouliza Mheshimiwa Mbunge.
NAIBU SPIKA: Ujibu moja tafadhali kwa sababu ndiyo kanuni zinavyosema kwa hiyo, chagua moja.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Ahsante, suala la ulipaji wa kifuta jasho na kifuta machozi, yapo mambo mawili jambo la kwanza ni utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa kanuni kwamba ule ni lazima utimie ukamilike na ambao unaanzia kwenye ngazi ya kitongoji au kijiji kwenda wilaya kwenda mkoa halafu kwenda hifadhi inayohusika na mpaka kwenye Wizara. Yale maombi au madai yanayopata sifa za kuweza kulipwa sasa yataingia kwenye kikwazo kingine cha pili ambacho si kikwazo lakini ni utaratibu kwamba kuna suala pia la bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kuna suala la kutimiza vigezo halafu kuna suala la uwepo wa fedha. Sasa yale yanayohusiana na utaratibu kwa sababu unahusisha pia Wizara kama kuna madai ambayo yamekidhi vigezo lakini pengine yanachelewa kwa sababu tu ya procedure za kiofisi hayo tunakwenda kuongeza kasi kuharakisha ili yakae pending kusubiri uwepo wa fedha na fedha zitakapokuwa zimepatikana madai yote yanayohusiana na kifuta jasho, na kifuta machozi yatalipwa mara moja.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Mbuga ya Akiba ya Uwanda katika Wilaya ya Sumbawanga Vijijini ilitengwa miaka ya nyuma wakati idadi ya watu ikiwa ndogo sana ikilinganishwa na sasa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipunguza pori hilo ili kunusuru shida inayowapata wananchi wanaozunguka eneo hilo ya kukosa maeneo ya kilimo na ufugaji? (b) Je, kwa nini wananchi wa maeneo hayo wanapigwa na Askari wa Wanyamapori na kunyang’anywa mali zao, wakati hakuna alama yoyote inayoonyesha mpaka katika mbuga hiyo? (c) Je, wananchi wa vijiji vinavyozunguka pori hilo wamenufaika na nini zaidi ya vipigo wanavyovipata?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa wananchi wa Kasulu wengi wao kwa kutokujua mipaka inaishia wapi; wamekuwa wakilima mpakani mwa pori la Kagera Nkani na kwa sasa mazao yao yako tayari wanahitaji kuvuna.
Je, Serikali iko tayari kumuagiza Mkuu wa Wilaya awaruhusu wananchi waweze kuvuna mazao yao huku utaratibu mwingine ukiwa unaendelea?

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, maagizo yametolewa mahususi kabisa kuhusu suala hilo kwamba Wizara pamoja na Wakuu wa Wilaya wawaruhusu wananchi ambao wamelima ndani ya hifadhi zetu waweze kuvuna mazao yao kabla hawajaondoka katika maeneo hayo.
Kwa hiyo, nimkumbushe tu Mkuu wa Wilaya juu maagizo hayo na awaruhusu wananchi wachukue mazao yao.

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Mbuga ya Akiba ya Uwanda katika Wilaya ya Sumbawanga Vijijini ilitengwa miaka ya nyuma wakati idadi ya watu ikiwa ndogo sana ikilinganishwa na sasa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipunguza pori hilo ili kunusuru shida inayowapata wananchi wanaozunguka eneo hilo ya kukosa maeneo ya kilimo na ufugaji? (b) Je, kwa nini wananchi wa maeneo hayo wanapigwa na Askari wa Wanyamapori na kunyang’anywa mali zao, wakati hakuna alama yoyote inayoonyesha mpaka katika mbuga hiyo? (c) Je, wananchi wa vijiji vinavyozunguka pori hilo wamenufaika na nini zaidi ya vipigo wanavyovipata?

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona swali langu ni dogo tu ambalo linafanana na swali la msingi la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, utamaduni uliokuwepo wa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa miaka ya nyuma uliruhusu wananchi wanaoishi kando kando mwa maeneo ya hifadhi waliruhusiwa kuvua samaki kwenye mabwawa hususan wananchi wa Jimbo langu la Rufiji wa maeneo ya Luwingo na utaratibu huu ulienda sambamba na kata zote; kata ya Mwasenimloka, kata ya Ngolongo pamoja Kagira, naomba kufahamu Wizara ya Maliasili na Utalii inaweka utaratibu gani sasa ili kuweza kuwasaidia wananchi wa maeneo haya katika kuchimba mabwawa ya samaki ili wananchi hawa wawekeza kuuza samaki hizo kuwasaidia kwa ajili ya kuwapeleka watoto wao shuleni? Ahsante.

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu ya msingi ya Mheshimiwa Naibu Waziri alielezea kuhusu masuala ya kimkakati ambayo ni lazima tuyashughulikie katika kuendesha hifadhi hizi na kutokana na mabadiliko ambayo yametokea katika maeneo ya mipaka ya hifadhi zetu zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, suala hili ni moja ya masuala ya mkakati na tutajadiliana na wananchi na hasa kwenda kabisa katika maeneo hayo ili tukubaliane na wananchi namna ya kutumia maeneo hayo ya kuvua na pale inapowezekana tuwasaidie wananchi kuwa na mabwawa yao wenyewe ili kusiwe na sababu yao kwenda ndani ya hifadhi.