Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, ni utaratibu gani unatumika kuajiri Watendaji kwenye Halmashauri nchini?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu hayo ya Serikali, kumekuwa na changamoto kubwa sana kwenye maeneo ya Mitaa, Vijiji na Vitongoji kuhusiana na Watendaji hawa kuonekana kufanya shughuli ambazo ni kinyume na utaratibu. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa semina ama mafunzo maalum kwa Watendaji hawa ili waweze kufanya kazi kulingana na malengo ambayo wamepelekwa kwenye maeneo hayo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Watendaji wengi wamekuwa wakijishirikisha na masuala ya kisiasa, hivyo kusababisha wananchi kupata mkanganyiko wa kujua Watendaji hawa ni wa Serikali ama ni wanasiasa? Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na Watendaji hawa ili wananchi waweze kujua Watendaji wako pale kwa ajili ya majukumu yapi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwaifunga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Maafisa Watendaji wa Vijiji, Maafisa Watendaji wa Kata ni Watumishi wa Serikali na wanaelekezwa kutumia utaratibu wa utendaji wao kwa kufuata taratibu za Utumishi wa Umma. Kwa hiyo, wale ambao wanakiuka kutekeleza majikumu yao, hatua za kiutumishi zitaendelea kuchukuliwa dhidi yao. Pia tutaendelea kuhakikisha tunawajengea uwezo kwa kuhakikisha kwamba tunawafanyia semina za mara kwa mara, tuna job training kwa Watendaji wetu.
Mheshimiwa Spika, pia jambo kubwa tumeshaelekeza kwamba Wakurugenzi Watendaji wanapoajiri Watendaji wa Vijiji na Watendaji wa Kata wawafanyie orientation ya majukumu yao lakini pamoja na kuwapa job description ili wajue majukumu yao na pia mipaka yao.

Mheshimiwa Spika, la pili kuhusiana na kujihusisha na siasa, kauli ya Serikali ni kwamba Watumishi wa Serikali, Watendaji wa Vijiji na Watendaji wa Kata wanatakiwa kufuata taratibu za Utumishi na kufuata miiko ya kazi zao, ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, ni utaratibu gani unatumika kuajiri Watendaji kwenye Halmashauri nchini?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Asilimia 50 ya Watendaji katika Wilaya ya Longido Mkoa wa Arusha wamekuwa wakifanya kazi kwa kujitolea, yaani wamekuwa wakikaimu kwa muda mrefu sana: Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha Watendaji hao wanapata ajira rasmi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika Halmashauri ya Longido na hata katika Halmashauri nyingine kote nchini wapo Watendaji wa Vijiji, wa Mitaa, wa Kata ambao wanajitolea na Serikali imeweka utaratibu, kila pale kibali cha ajira kinapotolewa, wale ambao wanajitolea katika maeneo hayo wanapewa kipaumbele; na kwa sababu ajira hizi zinatolewa katika ngazi za Halmashauri, kwa hiyo, nitumie fursa hii kuwasisitiza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kwamba wanawapa kipaumbele wale Watendaji wanaofanya vizuri ambao wanajitolea katika maeneo yao kila mara ambapo kibali cha ajira kinatokea, ahsante.

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, ni utaratibu gani unatumika kuajiri Watendaji kwenye Halmashauri nchini?

Supplementary Question 3

SPIKA: Hivi Mheshimiwa Waziri wa Utumishi, ule Mwongozo wa Ajira ambao mlisema, kwa wale watu wanaojitolea umeshakamilika ama bado? (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, tunaendelea, lakini tumeshamaliza na ninadhani tutakuja kutoa tamko hapa Bungeni. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, ni utaratibu gani unatumika kuajiri Watendaji kwenye Halmashauri nchini?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Watendaji hao wa Kata, Vijiji na hata wa Mitaa wanafanya kazi kwa mazingira magumu sana kwa kukosa vitendea kazi na hivyo kutokutoa huduma kwa ufanisi kwa wananchi. Napenda kujua ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wanapeleka vitendea kazi na hasa pikipiki kwa wale watendaji ambao wako kwenye maeneo ya vijijini?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Watendaji wa Kata na Vijiji wana changamoto ya vifaa na vyombo vya usafiri lakini Serikali na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshaelekeza, tumeanza kununua pikipiki kwa ajili ya Watendaji wa Kata na tunahakikisha kwamba tunatengea bajeti tayari wanalipwa shilingi 100,000 kila mwezi kwa ajili ya uendeshaji. Kwa hiyo, hatua hiyo tayari tumeanza kuichukua kama Serikali. Tunajua bado tuna kazi kubwa ya kufanya. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya utendaji ya Maafisa Watendaji wa Vijiji na Kata na hususan katika eneo hili la usafiri, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, ni utaratibu gani unatumika kuajiri Watendaji kwenye Halmashauri nchini?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Utumishi, alipokuja Iringa alikutana na tatizo la Watendaji ambao walikuwa wamejitolea muda mrefu na hawakupata ajira na aliwaambia kwamba wawaajiri na mpaka leo hawajaajiriwa: Je, ni kwa nini baadhi ya Wakurugenzi hawatimizi matamko yale ambayo Mawaziri wanatoa?

SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati alikuja Naibu Waziri wa Wizara gani?

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, alikuja Naibu Waziri wa Utumishi.

SPIKA: Mheshimiwa nani?

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, nilipokuwa kwenye ziara Mkoa wa Iringa kwenye Manispaa ya Iringa nilikutana na changamoto ya vijana ambao walikuwa wamejitolea ambao walikuwa wamefanya kazi kwa takribani miaka miwili, lakini pamoja na kwamba walikuwa wamefanya hivyo ilipofika kwenye jambo la ajira, walipokwenda kufanyiwa usaili walionekana kwamba hawafai, lakini Serikali kupitia taratibu zake ilijiridhisha kwamba kulikuwa na sintofahamu katika mchakato huo.

Mheshimiwa Spika, tulielekeza kwamba mchakato ule urudiwe tena lakini pia wale vijana waliokuwa wanajitolea ambao walionekana kuonewa warudishwe kazini mara moja. Sasa juzi nilikuwa naongea na Mheshimiwa Mbunge akanihakikishia kwamba wale vijana bado hawajaajiriwa. Sisi kama Serikali tumeshatoa maelekezo kupitia Ofisi ya Katibu Mkuu Utumishi kulishughulikia jambo hilo mara moja. (Makofi)

SPIKA: Hebu kidogo hapo kwenye hawafai, hebu fafanua kidogo kwenye “hawafai.”

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa taarifa tulizopewa pale, vijana wale walionekana kwamba wamefeli katika mtihani, lakini kiukweli ni kwamba kulionekana kuna figisu zimefanyika katika kuhakikisha kwamba wamefikia hayo matokeo na ndipo Serikali ilipoelekeza mchakato huo uangaliwe tena upya. Ndiyo maana mpaka sasa hivi tunapozungumza hapa hakuna majibu ya wale ambao wameshaajiriwa kwa sababu ziko taratibu zinazofanyika. (Makofi)