Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 4 2024-01-30

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:-

Je, ni utaratibu gani unatumika kuajiri Watendaji kwenye Halmashauri nchini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utaratibu unaotumika kuajiri Maafisa Watendaji wa Vijiji, Mitaa na Kata, ni kama ifuatavyo:-

Kwanza, Mamlaka za Serikali za Mitaa zinatenga fedha za mishahara kwenye Bajeti na kuomba Kibali cha Ajira Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Baada ya kupata kibali Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekasimiwa jukumu la kutangaza, kuwafanyia usaili waombaji, kuwaajiri na kuwapangia vituo vya kazi Maafisa Watendaji waliokidhi vigezo vya ajira. Utaratibu huu unashirikisha Halmashauri na Mamlaka za Ajira za Serikali Kuu.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka ya fedha ya 2020/2021 hadi 2022/2023 Serikali imeajiri Maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa 1,659 na Maafisa Watendaji wa Kata 394 na kuwapanga kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kulingana na mahitaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti na kutoa vibali vya ajira kwa Maafisa Watendaji wa Vijiji, Mitaa na Kata kulingana na mahitaji kote nchini, ahsante.