Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, lini mradi wa kupeleka maji katika Kata Sita za Izimbya, Kyaitoke, Mugajwale, Ruhunga, Katoro na Kaibanja kutoka Ziwa Ikimba utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na kusema kweli napongeza kwa hatua ambazo zimefikiwa katika mradi huo, tunachosubiri ni utekelezaji hapo mwakani mwanzoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mradi mwingine wa maji pale Kemondo, Mradi wa Maji Kemondo umechukua miaka mitatu, karibia minne bila kukamilika. Kwa nini unachelewa hivyo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza na nipokee pongezi zake, ninakushukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kupokea namna ambavyo taratibu tumeendelea kuzifanya na kwa ushirikiano wako Mheshimiwa Mbunge ninakuhakikishia mradi huu utaenda kuanza mara moja kadri tulivyosema.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na mradi wa Kemondo umechelewa kwa sababu ya kusubiria pampu ambazo zilikaa muda mrefu pale bandarini kupia michakato mbalimbali ya kiutaratibu, lakini mpaka hivi ninavyoongea tayari zile pampu zimeshachukuliwa, anazo Mkandarasi, kupitia Bunge lako Tukufu naomba nimuagize huyu Mkandarasi mwenye pampu za mradi wa Kemondo mara moja kufika mwisho wa wiki hii lazima pampu hizo ziweze kufika kwenye mradi. (Makofi)

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, lini mradi wa kupeleka maji katika Kata Sita za Izimbya, Kyaitoke, Mugajwale, Ruhunga, Katoro na Kaibanja kutoka Ziwa Ikimba utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba kujua mradi mkubwa wa maji kutoka Momba kwenda Tunduma mpaka Mbozi umefikia hatua gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Fiyao, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi mkubwa anaouongelea ni mradi wetu wa kimkakati kama Wizara, tukitambua changamoto kubwa ya maji katika Mji wa Tunduma vilevile Mji wa Momba. Mradi huu tayari utekelezaji unaendelea na tutahakikisha unakwisha kwa wakati.