Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 27 2023-11-01

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: -

Je, lini mradi wa kupeleka maji katika Kata Sita za Izimbya, Kyaitoke, Mugajwale, Ruhunga, Katoro na Kaibanja kutoka Ziwa Ikimba utaanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa mradi wa maji wa Ziwa Ikimba uliopangwa kunufaisha Kata Sita za Izimbya, Kyaitoke, Mugajwale, Ruhunga, Katoro na Kaibanja zenye jumla ya Vijiji 17. Utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi Machi, 2024. Aidha, Serikali katika mwaka wa fedha 2023/2024 inaendelea na uchimbaji wa visima katika Wilaya ya Bukoba Vijijini ambapo uchimbaji wa visima virefu Sita utafanyika katika Kata za Ruhunga, Kaibanja, Mgajwale, Izimbya, Katoro na Kyaitoke. Kwa ujumla uchimbaji huo umefikia asilimia 60 na unatarajiwa kukamilika Mwezi Novemba, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Serikali inatarajia kutekeleza mradi wa maji mwingine katika Kata ya Katoro utakaohusisha, ukarabati wa tanki la lita 150,000, Ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 35, ulazaji wa miundombinu ya kusambaza maji kilometa 37, kujenga nyumba ya pampu, kufunga umeme na Kununua na kufunga pampu ya kusukuma maji. Mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo anatarajiwa kupatikana mwezi Januari, 2024.